Blogger Widgets

Celebrity Story from Different Place

Entertainment story of Bongo land and their work.

Story za wakali wa majuu

Burudani| Video| Tracks na Maisha yao.

Bongo Movie na wasanii wake kwenye maisha yao

News Movie| New Story| New Skendo.

Mafanikio

Story za walio vuka boda na mafanikio yao kama wajasiria-mali.

Elimika na Burudika

Life ya wasio na skendo na wenye skendo| Mafanikio yao na vioo wa jamii.

Thursday, February 28, 2013

Wanawake wenye sura hii hawawezi kumuuwa nyoka akafa….!

Sura hiyo hapo ni ya mwanamke. Bila shaka umeshwahi kukutana na sura kama hii katika maisha yako. Kama hujawahi kukutana nayo huenda kuna siku utakutana nayo. Jaribu kuzingatia mdomo, meno, macho na paji la uso. Zingatia baadaye, sura nzima kwa ujumla.
Mwanamke mwenye sura kama hii ana tabia zifuatazo:
Ni mwanamke mcheshi na anayependa kujichakesha. ni mwanamke ambaye ana uwezo na ufahamu mkubwa kiakili. Anajua sana kujiuliza maswali kabla hajafanya jambo lolote kuhusiana na namna anavyohusiana na watu wengine. Ni mwanamke mvumilivu na mwenye subira kubwa kwa wengine, hasa wanaomhusu.
Nikisema ni mvumilivu na mwenye subira, nina maana kwamba, anapokerwa na mpenzi, ndugu au rafiki, huchukua muda kufanya uamuzi, hakurupuki tu. Hujiuliza maswali ya hekima kabla hajafanya jambo. Lakini ni mwanamke ambaye hawezi kuuwa nyoka akafa. Ina maana kwamba, akitendewa ubaya leo, ataendelea kuukumbuka kwa muda mrefu sana. Hatalipa kisasi, lakini itakuwa ngumu kwake kusahau.
Mwanamke mwenye sura kama hiyo, hakawii kubadilika. Anaweza kuonekana amekata tamaa kabisa katika jambo au mambo fulani, lakini akitiwa nguvu kidogo anabadilika kabisa na kujipa nguvu ya kuweza na akaweza hasa. Mwanamke mwenye sura hii ana juhudi ya kujenga maisha yake kwa kiwango chenye kushangaza. Anapoamua kufanya hivyo, hufanya kweli na hana mzaha na kile anachofanya.
Ni rahisi kwa mwanamke mwenye sura hii kuvunjwa nguvu, lakini sifa moja kubwa kwake itakuwa ni ile hali ya kujiambia kwamba, ana maisha yake. Lakini kuna bahati mbaya kwamba, wanawake wenye sura kama hii, huwa wanaingia kwenye uhusiano wenye mashaka kirahisi. Wanatokea kupenda kama vipofu na kushikwa kirahisi na wanaume ambao wameingia nao katika uhusiano. Huwa wanasaidia sana kama wamempenda mtu na kusaidia huku hufikia hatua ya utumwa na siyo upendo.Wenye sura hii wanavyoonekana sivyo wanavyojibu kwenye ombi la tendo la ndoa. Wanaweza kuonekana kama wako tayari kushiriki tendo la ndoa kwa kuonesha dalili zote muhimu, lakini majibu yakaja tofauti kabisa, hadi mwanaume akashangaa.
Hii inatokana na ucheshi wao, kuwa huru katika kujadili mambo na kuchelea kuwakera wengine. Kwa hali hiyo, huwa wanajenga uadui na wanaume au watu wengine ambao hushindwa kuwaelewa. Uzuri wao mwingine ni kujiamini, kusimama kama wao. Kama nilivyosema, mara nyingi hujihesabu kama wao na sio kama watu wengine. Mara nyingi sana ni watu wasiojali sana wengine wanasema kitu gani juu yao.
Chanzo:- Utambuzi na kujitambua.

Dola 377,000 zatumika kununua iPad bungeni

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni. 
 
BUNGE nchini Uganda limetumia zaidi ya  dola 377,000 kununa kompyuta aina ya iPad kwa ajili ya wabunge wote .
Maofisa wa bunge hilo walisema kuwa mbali na kuwaweka wabunge hao karibu na  ulimwengu wa teknolojia, wanatarajia kuwasaidia kupunguza gharama za fedha zinazotokana na matumizi ya uchapishaji wa nyaraka mbalimbali.
Kamishna wa bunge hilo Elijah Okupa alisema kuwa kompyuta hizo ni bora na zinafaa kwa matumizi hivyo ni vyema zikatumiwa vizuri.
Alisema  iPad hizo zitakuwa ni mali ya wabunge lakini kama mtu atatumia kwa muda wa miaka mitano asitegemee itakuwa na ubora uleule wa kumwezesha mwingine atumie kwa miaka hiyo alisema Okupa
Kwa mujibu wa takwimu kutoka katika bunge hilo zilionyesha Serikali imekuwa ikitumia zaidi ya dola 12 katika miaka miwili sasa kwa ajili ya mahitaji ya kama kompyuta, uchapishaji wa nyaraka, mbalimbali kwa ajili ya kuwezesha mawasiliano kuwa bora katika bunge.
Kwa mujibu wa mbunge kutoka mashariki, Medard Segona alisema kuwa kutokana na uwepo wa ipad hizo wanategemea kupunguza matumizi ya fedha zilizokuwa zikipotea hapo awali.
‘’Vifaa hivyo vitapunguza sana matumizi ya fedha kwa kuwa hapo awali wizara ya fedha ilikuwa ikichapisha zaidi ya nyaraka 400 kwa kila mbunge na maofisa wengine waliopo ndani ya bunge hilo’’alisema
Aliongeza kuwa komputa hizo ni muhimu kwa utendaji kazi hasa katika kipindi hicho cha kuendeleza matumizi ya teknolojia.
Hata hivyo taarifa zilisema kuwa wabunge hao bado hawana uelewa mzuri juu ya matumizi hayo licha ya kuwa kampuni imeahidi kutoa  mkataba wa mafunzo ambayo pia yatasaidia kupunguza gharama za matumizi.


MWANANCHI

HATARII........KIJIJI CHA UKAHABA CHAGUNDULIKA MBAGALA


watuhumiwa wakiwa chini ya ulinzi wa wananchi
SIKU  chache baada ya kuibua danguro la vigogo maeneo ya Kinondoni jijini Dar es Salaam na wahusika kutiwa mbaroni na polisi, mwishoni mwa wiki waandishi wetu wamekifumua kijiji cha ufuska.


  Kijiji hicho kilichogunduliwa Mbagala Zakhem, jijini Dar, wasichana na wavulana walinaswa wakifanya vitendo vya ngono kwenye moja ya mabanda ambayo yametengenezwa maalumu kwa shughuli hiyo.
Awali, waandishi wetu walipata taarifa kutoka kwa wasamaria za kuwepo kijiji hicho pembezoni mwa barabara ya kwenda Kiburugwa, hivyo kuamua kufuatilia.
Operesheni hiyo ilifanywa na waandishi wetu kwa kushirikiana na jeshi la polisi Jumamosi iliyopita usiku ambapo ilifanikiwa kuwanasa baadhi ya vijana akiwemo mwanamke mmoja aliyekutwa akifanya ngono na wanaume wawili (walio pichani).
Hata hivyo, kundi la watu kama wanane wakiwa na nguo mikononi walitimua mbio baada ya kuona polisi wamevamia chumba kimoja kilichotengenezwa kwa uzio wa vipande vya magunia chakavu na makaratasi walichokuwa wakikitumia kufanyia ngono.
 Aidha, wana usalama walifanikiwa kuwakamata watu watatu, wanaume wawili pamoja na mwanamke aliyejitambulisha kwa jina moja la Semeni waliyekuwa wakifanya naye mapenzi.
Baada ya kuwatia mbaroni watu hao na kuwafanyia upekuzi, walikutwa na kondomo na vipisi vya bangi.
 Gesti bubu inayotumika
Maafande walipomhoji Semeni alisema vijana hao walimlipa shilingi 5,000 kila mmoja na mmiliki wa eneo hilo aliyemtaja kwa jina moja la Babu walimlipa shilingi 2,000.
Mtu mmoja aliyeshuhudia tukio hilo, aliwapongeza polisi kwa kufanikiwa kuwakamata baadhi ya vijana hao.
 “Kwa kweli sehemu hii ni kama kijiji cha ngono maana hata wanafunzi huchukuliwa
  na kuingizwa kwenye vibanda hivi kwa ajili ya kufanya ufuska, tunashukuru kwa kuamua kukisambatisha,” alisema jamaa huyo aliyeomba hifadhi ya jina lake.
Asubui mpa saa 11 ni hoteli

Salama Jabir achafukwa na roho ‘uchizi’ wamtanda, baada ya katakata ya umeme, MMCHEKI HAPA

484946_146643805496139_968742939_n


Siku za hivi karibuni kumekuwepo na katizo la umeme la mara kwa mara katika maeneo mengi ya jiji la Dar es Salaam (hatuna uhakika mikoa mingine mambo yakoje) kiasi cha kuathiri shughuli nyingi za kiuchumi.
Kufuatia tabia hiyo ya Tanesco kufanya yao kila siku na kuwaweka wajasiriamali wanaotegemea umeme kwenye mawe, mtangazaji wa kipindi ca Mkasi, Salama Jabir, ameamua kuzipunguza hasira zake kwenye Twitter kwa kuandika:
Kazi inabidi ziende jamani…The f**k is wrong na hii nchi?!Umeme tu?????!Shida isotatulika miaka nenda rudi?!Tunachoshaaaana. F**k that shit!! Taarifa hakuna…kuunguziana mali tu,kulipa hamlipi,kauli nzuri hamna!! Who does that?! Well..Mnatufunza sana,Asanteni!!
Watu wakiamua kuishi nje serikali inalalamika Ooh vijana hawana upendo na nchi yao!!Utapendaje nchi inayokurudisha nyuma? What the f**k?! Well KZMZ!!! Alosema bora mthamini mbwa naona hakuwa mbali na Ukweli..Ki ukweli misemo ya wahenga yote ni ukweli mtupu, again…KZMZ.
Nimejipigapiga mwenyewe nikanunua kaTV ka kitundika ukutani kama tunazoziona kwenye TV mkaunguza,nikarudisha dukani watengeneze.

Meli ya Titanic kuingia majini tena, tiketi moja itauzwa kwa karibu tshs bilioni 1.5

Palmer akizungumza katika uzinduzi wa mradi huo
Palmer akizungumza katika uzinduzi wa mradi huo


titanic-2jpg-5e542fec88b87b16 (600x338)


Bilionea wa nchini Australia Clive Palmer ametangaza mipango yake ya kujenga meli pacha ya Titanic lakini hii ikiwa na lifeboats za ziada ili kuwa na usalama zaidi kuliko ya mwanzo.
Zaidi ya karne baada ya Titanic original ambayo ilidhaniwa kuwa haitaweza kuzama baharini lakini ikagonga jiwe la barafu la kuzama kwenye bahari ya Atlantic katika safari yake ya kwanza, Palmer anasema anadhani muda umefika kumalizia safari hiyo ambayo haikumalizika kuelekea New York.
“Titanic ilikuwa ni meli ya ndoto. Titanic II ni meli ambayo ndoto zitakuwa kweli,” alisema Palmer said jijini New York wakati wa uzinduzi wa mradi huo.
Meli hiyo itakuwa na madaraja yale yale matatu kama meli ya kwanza iliyotengenezwa mwaka 1912, daraja la kwanza, la pili na la tatu na abiria hawatakuwa na uwezo wa kuingiliana kwenye madaraja hayo.
Titanic ya pili itakuwa na uwezo wa kubeba abiria 2,600 na wafanyakazi 900 na safari itaanzia Southampton hadi New York ifikapo mwaka 2016 katika safari itakayokuwa kama ile ile ya mwanzo na bila shaka bila kuzama tena.
Kwa mujibu wa ripoti ya Mashable, Palmer ameshaanza kupokea ofa za tiketi moja itakayouzwa kwa dola milioni moja.

Polisi wamuongezea ulinzi Rick Ross baada ya maisha yake kuwa hatarini tena, ANGALIA HAPA.

Rick+Ross+Backstage+BET+Rip+Runway+Show+m6WNbNdVxn7l
Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, polisi wamekuwa wakimlinda Ross aliyefikia kwenye hoteli ya The London kwa siku za hivi karibuni. Vyanzo vimeuambia mtandao huo kuwa vitisho vipya dhidi ya rapper huyo mwenye makazi yake jijini Miami, Florida hajavichukulia kawaida.
Mwezi uliopita Ross akiwa anaendesha gari lake aina ya Rolls-Royce alinusurika kupigwa risasi huko Ft. Lauderdale muda mfupi baada ya kutoka kwenye party ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa. Hata hivyo yeye na msichana aliyekuwa naye hawakujeruhiwa.

KAMA ULIJIULIZA KWA NINI PREZZO HAKUONEKANA KTK MSIBA WA GOLDIE, JIBU LAKO HILI HAPA

Prezzo anaonekana akiwa amevaa nguo nyeusi zote, hii ilikua ni ibada ya kumuombea Goldie ambayo ilifanyika siku kadhaa kabla ya Prezzo kuondoka Nigeria kurudi Kenya.

Ni watu wengi wanajiuliza imekuaje CMB Prezzo hajaonekana kwenye msiba wa mpenzi wake ambae walikua na plans za kuoana, Mnigeria Goldie aliefariki muda mfupi tu baada ya kufika Nigeria akitokea Marekani.
Kwa sababu nimeamua kumuacha Prezzo apumzike kwa sasa, ili kujua angalau hata kwa muhtasari niliamua kumtafuta Arthur Samwel ambae ni Dj wake na msimamizi wa kazi nyingi anazofanya Prezzo.
Andrew Harvey akimuaga mke wake Goldie siku ya maziko.

Najua siku chache kabla ya Goldie kuzikwa, vyombo vya habari kadhaa vya Nigeria viliandika kwamba mume wa Goldie, Andrew Harvey ambae ni raia wa Uingereza alimtumia ujumbe Prezzo akiwa Nigeria kwamba alichofanya basi inatosha, hatotaka kumuona tena akiwa karibu na familia ya Goldie.
Alichosema Arthur kuhusu Prezzo kutomzika Goldie ni hiki “Prezzo alirudi Nairobi wiki iliyopita, ilikua ni weekend na mpaka anatoka Lagos alikua hajui ni siku gani Goldie atazikwa kwa sababu Wanigeria wanatabia ya kuchelewa kuzika, sasa mtu kama uko ugenini huwezi kukaa muda wote…….. kwa bahati mbaya Prezzo akiwa amesharudi Nairobi alipigiwa simu kwamba Goldie ameshazikwa hivyo ikawa ni ngumu kurudi tena Lagos, sasa hivi yuko Eldoret Kenya kwenye ishu za kampeni”

Wednesday, February 27, 2013

HUYU HAPA YULE MSANII ALIYEMTELEKEZA MTOTO STENDI YA UBUNGO


MREMBO aliyewahi kupamba video kadhaa za wasanii wa Bongo Fleva ukiwemo wimbo wa Kidato Kimoja ulioimbwa na J.I, anayekwenda kwa jina la Maya Silemwe, amedaiwa kumtelekeza mwanaye wa kumzaa aitwaye Junior Justine (3).   Tukio hilo la kusikitisha lilitokea hivi karibuni katika kituo cha mabasi yaendayo mikoani, Ubungo jijini Dar es Salaam ambapo mtoto huyo aliokolewa na msamaria mwema.  Akisimulia mkasa mzima ulivyokuwa, shangazi wa mtoto huyo aliyejitambulisha kwa jina moja la Monalisa, alisema wao kama familia wameumizwa sana na kitendo kilichofanywa na Maya.

HII HAPA SASA ILE VIDEO YA WIZKID – AZONTO




Ni mkali wa Nigeria ambae amekuwemo kwenye headlines kwa kipindi kirefu kidogo sasa hivi kutokana na stori zake za kuachana na lebo iliyokua inamsimamia na kuanzisha lebo yake mwenyewe, pamoja na hayo… mpaka sasa sijaelewa ile dili yake ya kuwa chini ya Akon iliishia wapi lakini theHOODinfotainment iko kwa ajili yako tunaakika tutaifanyia kazi hii ishu.

HIVI UNAUJUS UHUSIANO ULIOPO BAINA YA SHAA NA MASTER J ? Soma haps

Shaa na Master J.

Hii interview ya Shaa kwenye Leo Tena ya Super Brand Clouds FM 
Ni kuhusu alichosema kuhusu taarifa za uhusiano wake na Producer Legend Tanzania Master J, ilikua ni interview ambayo  watu wengi walienjoy kuisikiliza manake Dina Marios na Shaa na wengine waliokuwepo studio walikua wamechangamka sana alafu Shaa alijiachia vizuri pia.
Alichojibu Shaa kwenye maswali ya ndio au hapana ni hapana, akisema “Ndugu mtangazaji hapana, hatuna uhusiano wowote”
Kwenye mstari mwingine Shaa alisema mpenzi wake atatambulika baada ya wazazi wake kumfahamu na kupokea mahari, baada ya hapo sasa kadi za mwaliko ndio zitaweka ukweli ambao wengi wanataka kuujua.

HUYU NDIYE MTANZANIA ALIYEPEWA UWAZIRI NCHINI RWANDA,AUKANA UTANZANIA

Mtanzania apewa uwaziri nchini Rwanda!

- RAIS Paul Kagame wa Rwanda amemteua Mtanzania, Prof. Silas Rwakabamba kuwa Waziri wa Miundombinu wa nchi hiyo
- Ni mzaliwa wa Kijiji cha Bushagara, Wilaya ya Muleba mkoani Kagera
- Amelazimika kuukana uraia wa Tanzania kwa kuwa katiba ya nchi hairuhusu uraia wa nchi mbili

Endelea kusoma zaidi -> http://j.mp/ZJgTRK
RAIS Paul Kagame wa Rwanda amemteua Mtanzania, Profesa Silas Rwakabamba kuwa Waziri wa Miundombinu wa nchi hiyo katika mabadiliko ya Baraza la Mawaziri yaliyofanyika Jumatatu iliyopita.

Kabla ya uteuzi huo, Profesa Rwakabamba alikuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Rwanda. Ni mmoja wa mawaziri wanaoingiza sura mpya katika Baraza la Rais Kagame ambalo amelifanyia mabadiliko kwa kuunda wizara nyingine mpya.


Sura nyingine mpya katika Baraza hilo ambalo liliapishwa juzi Ikulu ya Rwanda ni pamoja na Seraphine Mukantabana (Wakimbizi na Menejimenti ya Maafa) na Oda Gasinzigwa (Ofisi ya Waziri Mkuu- Familia na Jinsia).


Akizungumza kwa simu na mwandishi wetu jana, mdogo wa Profesa Rwakabamba, Timothy Rwamushaija anayeishi Dar es Salaam, alisema ndugu yake alizaliwa katika Kijiji cha Bushagara, Wilaya ya Muleba mkoani Kagera.


Alisema Profesa Rwakabamba alikuwa Mtanzania aliyeamua kuchukua uraia wa Rwanda na wote baba yao ni Mzee Titus Rwamushaija... “Huyu ni kaka yangu wa tumbo moja na kwa kweli tumefurahi sana kwa mafanikio yake sisi kama wanafamilia.”


Naibu Makamu Mkuu - Taaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM), Profesa Makenya Maboko alisema Profesa Rwakabamba alifanya kazi katika chuo hicho na aliondoka akiwa Mkuu wa Kitivo cha Uhandisi.


“Aliondoka wakati Kagame alipoingia madarakani na alikwenda kuongoza Taasisi ya Teknolojia ya Kigali (KIST) kabla ya kwenda katika Chuo Kikuu cha Kigali,” alisema Profesa Maboko.


Msomi huyo alikwenda Rwanda mwaka 1997, baada ya kuombwa na Rais Kagame ambaye alikwenda UDSM kuwaomba baadhi ya wahadhiri kwenda Kigali kufungua chuo kikuu katika taifa lake baada ya kumalizika vita ya wenyewe kwa wenyewe mwaka 1994.


Profesa Rwakabamba alikuwa Mkuu wa kwanza wa KIST na kukifanya kuwa miongoni mwa vyuo bora barani Afrika kwa masuala ya teknolojia jambo lililomfurahisha Rais Kagame.


Baada ya mafanikio hayo, Rais Kagame alimteua kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Rwanda, Butare ambako pia alijizolea sifa baada ya kusimamia vyema ujenzi wa mabweni kwa wingi na kiongozi huyo alimtunukia uraia wa nchi hiyo kama zawadi.


Hata hivyo, Profesa Rwakabamba atakuwa amelazimika kuukana uraia wa Tanzania kwa kuwa katiba ya nchi hairuhusu uraia wa nchi mbili.


Profesa Rwakabamba alipata elimu ya msingi huko Muleba na akajiunga na Shule ya Sekondari ya Ihungo.


Baada ya hapo, alijiunga na Chuo Kikuu cha Leeds, Uingereza na kupata Shahada ya Uhandisi mwaka 1971 na 1975 alipata Shahada ya Uzamivu katika fani hiyohiyo.


--------

JAMIIFORUM, kuliwahi kuwa na mjadala juu ya mwanazuoni huyu hapa ---> Yupo wapi Professor Silas Lwakabamba Mtanzania Mwanzilishi wa Kigali Institute-KIST

ANGALIA VITUKO VINNE VYA MASANJA MKANDAMIZAJI KWENYE FACEBOOK LEO, VINACHEKESHA MNO

Kumbuka mjane ni aliefiwa na mwenzi wake.
.
.
.

Video za hip hop za mtoto wa miaka 9 ‘Lil Poopy’ zazua mjadala Marekani, polisi yapanga kumkamata baba yake. ANGALIA HAPA

Mtoto mwenye umri wa miaka 9, Luie Rivera Jr., ambaye jina lake la kisanii ni “Lil Poopy,” ameonekana kwenye video anazozipost online hususan kwenye mtandao wa YouTube, akicheza muziki na wasichana wakubwa kwa umri wake, akiendesha magari ya kifahari kama Ferrari na akirap maneno kama “coke is not a bad word.”
lil poopy

Katika video nyingine mtoto huyo anaonekana akicheza na msichana katika pozi chafu huku watu wakimtupia hela.
poopyladies

Idara ya polisi ya Brockton, Massachusetts, imewasiliana na ofisi inayoshughulikia masuala ya watoto na familia nchini humo baada ya kupokea simu nyingi kutoka kwa watu walioguswa kufuatia kuona video zake.
lil-poopy-584x350

Baba wa rapper huyo Luie Rivera ameajiri mwanasheria kujilinda na uwezakano wa kukamatwa kwa kosa la jinai.

Madee HAKANA usanii wake soma hapa

 
Rapper wa kundi la Tip Top Connection Hamad Ally aka Madee amedai kuwa yeye sio mwana Hip Hop na wala sio shabiki wa muziki huo.
madee
Madee ambaye aliwahi kuachia wimbo uitwao Hip Hop Hailipi amefunguka kupitia Clouds FM kuwa haimbi hip hop bali ni rapper.
“Watu wanashindwa kutofautisha, mimi sio mwana hip hop mimi ni ‘rapper’ ndio maana naweza kuweka michano kwenye beat yeyote na nikafanya poa,” alisema Madee. “Nakumbuka nilipatwa na mambo mengi sana baada ya kutoa ile ngoma Hip Hop Haiuzi, sikuchukia kwa sababu nilijua kuwa waliokuwa wakinilaumu walikuwa hawajui lolote kuhusu muziki lakini walionielewa nadhani walipata picha ya kile nilichokua nikisema na kile ninachokifanya, nasisitiza mimi sio mwana hip hop na sijawahi kuwa mfuasi wa muziki huo.”

 

ALIPOANZA KUTOKA DIAMOND KIMZIKI NI HAPA

We started from the bottom naw we here....!!!
 

Ray: HAYA NDIO MAJIBU ALIYOYATOA KWANINI AMEKONDA, AMEULIZA SWALI MOJA KWA MASHABIKI WAKE SOMA HAPA "Jamani siumwi bali nafanya mazoezi tu"

Muigizaji aliyepo kwenye list A ya waigizaji wa filamu Tanzania, Vincent Kigosi aka Ray ameamua kuzungumza baada ya watu kuanza kumzushia anaumwa kutokana na kupungua mwili wake kwa kiasi kikubwa.
Ray before and after

Picha hiyo ya juu inamuonesha alivyokuwa mwanzo (kushoto) na jinsi alivyo sasa (kulia).
Ray amezikanusha tetesi hizo zilizoanza kusambaa kwa haraka ambapo gazeti la udaku la Kiu wiki hii lilikuwa na habari isemayo, ‘Ray apukutika mwili’ – Kitambi chote kwishnei! Ukimuona unaweza kumpita bila kumtambua, maombi ya wakatoliki yahusishwa.
Hata hivyo Ray amesema hali hiyo imetokana na kufanya mazoezi zaidi siku za hivi karibuni. “Jamani kwani unene ndio afya au kupungua ndio ugonjwa,” ameuliza Ray.

Cpwaa: I’m about to kiss Bonga Flava goodbye

cpwaa3

Kutokana na posts mbalimbali anazoziandika kwenye Facebook na Twitter, crunk master huyo anaonesha atakuwa chini ya menejimenti mpya itakayosimamia kazi zake. Akiwa chini ya menejimenti hiyo mpya, Cpwaa anadai ataiiaga rasmi Bongo Flava na kuanza kudondosha ngoma kwaajili ya mashabiki wake wa crunk.
“So am about to kiss Bongoflava goodbye in the next few months, before the new management Chain me to some serious shiit…I wanna do it once more for the street and my crunk fans,,#TrapMusic….If u got some beats inbox me,” ameandika.

ALIPOANZA KUTOKA DIAMOND KIMZIKI NI HAPA

We started from the bottom naw we here....!!!
 

HUU NDIO UTHIBITISHO WA KWANZA WA CHRIS BROWN KURUDIANA NA RIHANNA, KAULI YA CHRIS MWENYEWE..

.
Kwa wanaopenda mapenzi ya hawa mastaa hii post najua hii post itawahusu sana na kuwapa furaha.
Kwa kipindi kirefu toka wamerudiana kimapenzi na Rihanna Chris Brown sijawahi kumsikia au kumuona akizungumzia huu uhusiano manake kwanza stori zilikua zinasikika kama fununu tu.
Sasa juzi kwenye usiku wa Oscar, Chris amethibitisha rasmi uhusiano wao wa kimapenzi kurudi ambapo amekaririwa akiongea na Page Six akisema “ni kweli tumerudiana, She is the most beautiful girl in the world, nilikua niwe nae hapa ila imeshindikana sababu anajiandaa na Tour yake”

Tuesday, February 26, 2013

Wanajeshi wa Marekani wakiri kubaka. soma hapa ujue ni kwanini walibaka


Wanajeshi wa jeshi la wanamaji la Marekani, wamekubali mashtaka ya kumbaka mwanamke mmoja katika kesi ambayo imeibua hisia kali dhidi ya Marekani.
Wanaume hao. Walimvamia mwanamke huyo, wakati wa ziara yao fupi katika kisiwa cha Okinawa, makao kwa kambi kubwa ya jeshi la Marekani barani Asia.
Sheria ya kutotoka nje iliyowekewa wanajeshi karibu elfu hamsini kufuatia tukio hilo Okotoba mwaka jana
Kumekuwa na hali ya wasiwasi kati ya majeshi ya Marekani na wenyeji wa Okinawa.
Manamo mwaka 1995, genge la wanajeshi wa Ulaya, lilimvamia na kumbaka msichana mwenye umri wa miaka 12 na kuzua maandamano makubwa.
Source: BBC SWAHILI
USArmy

UMESHAWAHI KUMUONA MKE WA OBAMA AKICHEZA HIVI? angalia hapa.


Michelle Obama ni mama mwenye umri wa miaka 49 akiwa ni mke wa rais wa 44 wa Marekani pia akiwa ni first African-American First Lady of the United States, mtazame kwenye hii video akionyesha uwezo wake mwingine wa kudance kwenye Evolution Of Mom Dancing.

HII HAPA STORI KAMILI KUHUSU CHRIS BROWN NA RIHANNA KUFUNGA NDOA

RiRi na Chris Brown.

Jarida maarufu (Star Magazine) limeripoti kwamba mastaa wa muziki Chris Brown na Rihanna wanampango wa kufunga ndoa mwishoni mwa July 2013 nyumbani kwa kina Rihanna huko Barbados.

Jarida hili limeendelea kutiririka kwamba kwenye ndoa hiyo wamepanga kusherehekea na watu mbalimbali wakiwemo wanaoamini kwamba Chris Brown amebadilika kitabia.

Ni harusi ambayo watu wote walioalikwa watakua wamesimama na wahudumu watakuepo kumfata kila mtu alipo, pia wale wachoraji wa tattoo watakuepo pia.

ADHABU ALIYOPEWA KOCHA WA AZAM FC BAADA YA KUVUA BUKTA UWANJANI, SOMA HAPA ADHABU HIYO NA KWANINI ALIIVUA BUKTA HIYO.


.
Kocha wa club ya soka ya Azam FC Stewart Hall amefungiwa mechi tatu na kupigwa faini ya Sh 500,000 kwa kushusha bukta aliyokua ameivaa wakati akimlalamikia mwamuzi msaidizi kwenye mechi ya Azam na Kagera Sugar kwenye ligi kuu ya Tanzania bara January 26 2013 Chamazi, Mbagala Dar es Salaam.

Adhabu imetolewa na TFF baada ya kukutana  na kupitia ripoti za michuano ya Ligi kuu na Ligi Daraja la Kwanza.

Kocha Msaidizi wa Mgambo Shooting Denis Mwingira ametozwa faini ya Sh 500,000 kwa kumtolea lugha chafu mwamuzi wa mechi na Mtibwa Sugar october 2012.

Ally Jangalu akiwa ni kocha msaidizi wa Polisi ya Moro nae amepigwa faini ya laki tano baada ya kutolewa kwenye benchi kwa kupinga kwa sauti kubwa maamuzi ya refa November 2012.

RAY AKONGOROKA GAFLA AIBUA MASWALI KWA WADAU WAKE, ANGALIA PICHA ZAKE HAPA

MWIGIZAJI Vincent Kigosi ‘Ray’ amezua hofu kwa ndugu, jamaa, marafiki na mashabiki wake baada ya kukongoroka ghafla akihisiwa anaumwa, Ijumaa Wikienda limemfuatilia hatua kwa hatua.
 
Vincent Kigosi ‘Ray’ alivyo kwa sasa.
KWENYE ‘BETHIDEI’ YA BATULI
Wiki kadhaa zilizopita paparazi wetu alishtuka alipomuona Ray kwenye ‘bethidei’ ya mwigizaji sistaduu Yobnesh Yusuph ‘Batuli’ ndani ya Hoteli ya Shamoll iliyopo Sinza ya Lion, Dar akiwa amekongoroka na kuibua maswali kwa wahudhuriaji.
 
Akiwa ukumbini hapo, minong’ono ilienea kuwa Ray alionekana kukondeana katika kipindi kifupi huku baadhi ya watu wakisikika wakiulizana kulikoni kwani alikuwa meza moja na bonge la mtu, Jacob Steven ‘JB’ hivyo kumfanya kuonekana mdogo mno.

                               Vincent Kigosi ‘Ray’ alivyokuwa mwaka jana.

VIWANJA VYA LEADERS
Akiwa kwenye Viwanja vya Leaders, Kinondoni, Dar wiki iliyopita, Ray aliibua mshtuko kwa mara nyingine hadi jamaa mmoja anayedhaniwa kutokuwa vizuri kichwani kumfuata na kumuwakia akimuuliza kwa hasira kuwa kulikoni akondeana kiasi hicho.

UZINDUZI WA WEMA
Kwa mara nyingine, Ray alizua hofu alipohudhuria kwenye uzinduzi wa ofisi ya Wema Sepetu uliofanyika maeneo ya Kinondoni, Dar ambapo alipoingia watu walipigwa butwaa wakimtazama na wengine kumuonea huruma wakidhani anaumwa.

IJUMAA WIKIENDA LATAKA MAJIBU
Kwa nyakati tofauti, wanahabari wetu walizungumza na Ray ambaye alitoa majibu ya kukinzana na kuzidi kutia shaka.
Ray alimwambia mmoja wa waandishi wetu kuwa kilichosababisha akongoroke kiasi hicho ni mazoezi makali anayofanya ili kupunguza unene.
Katika majibu mengine kwa mwandishi wetu mwingine, Ray alidai kuwa anafanya ‘dayati’ ikielezwa kuwa ikishafika saa 11:00 jioni ndiyo mwisho wake wa kula msosi lengo likiwa ni kupunguza mwili uliokuwa umefumuka.
Kama mtu alimuona Ray kwenye Matamasha ya Serengeti Fiesta mwishoni mwa mwaka jana, akikutana naye lazima amtazame mara mbilimbili hivyo Ijumaa Wikienda lipo mzigoni kutafuta undani wa madai kuwa huenda staa huyo mkubwa anaumwa kufuatia majibu tofauti aliyoyatoa.
                               CHANZO CHA HABARI NI GLOBAL PUBLISHERS

WAJUE NA KUWATAMBUA FREEMASON, HAWA HAPA.

Historia ya Freemason imegawanyika katika Nyakati kuu mbili tofauti, Yaani Kabla na baada ya Grand Lodge of England on 24th June 1717. Baada ya kutengenezwa kwa Grand Lodge huko Uingereza ambazo zilikuwa maalumu kwa Freemason, Freemason walianza kuenea Duniani kote kwa kutengeneza Lodges za mtindo huohuo katika nchi nyingine, na sasa ikafika hadi Tanzania, Kabla ya ukoloni. Marekani ilifika Mwaka 1775.
Ningependa kuwapa kazi ambazo wao huwa wanazifanya na Tabia za watu hawa ambao wapo kwenye Dini hiyo ya Kishetani.
1. Kusaidia watu wote wenye matatizo mbali mbali, Mfano majanga kama kwetu hapa Gongolamboto, Mbagalia Mabomu, Mafuliko, Kuunguliwa Moto nakadhalika 
2. Kusaidia vituo vya watoto yatima, Kuandaa sikukuu au mikutano ya vilema na wamama wajane.
3. Wanatoa misaada ya kupata kazi na awakati mwingine facilities na njia mbadala za kupata kazi.


Tabia zao 
1. Kwanza ni wapole na wanyenyekevu sana kwa watu na hawapendi makundi yenye kujitoa kimbelembele.
2. Wengi wao ni matajiri na watu maarufu, na wenye Heshima kubwa sana kwenye nchi husika, na wafanyabiashara. 3. Watu wanaopenda kujitolea kwa hali na mali katika jamii, ikitokea tatizo lolote la kitaifa. 4. Wanaopenda kuanzisha mifuko mbalimbali kwaajili ya jamii Fulani, Lengo ni kupata 5. Hawapendi ugomvi au machafuko ya aina yoyote, ni watu wa Amani. 6. Hutumia Ufreemason wao kupata wateja kwenye biashara zao, au kupata watu wengi kwenye majukwaa ya kisiasa kwa lengo la kushinda chaguzi mbalimbali, kwa wanamuziki Ili miziki yao ipendwe na kupata watu wengi kwenye shoo zao. Wachezaji kwa Fowadi waweze kushinda magoli wawapo kwenye mechi, na Waigizaji kazizao zipendwe na wao wawe na followers wengi.

Alama zao

Hizi ni alama wanazo tumia Mara kwa mara wakiwa kwenye shugulizao kwaajiri ya kuleta mvuto kutoka kwa watu wanao wasikiliza au wanaofuata Burudani kwa Wanamuziki Kama Michael Jackson.
Pia kwa Wachezaji wanaishara ya Vidole Viwili kuonesha chini (cha pili na cha tatu kutoka dole gumba) wakati wa kupiga faulo, na Penalt. au wakikaribia Goli wakati wa Kufunga ( Messi, Ronaldo ) ni mifano mzuri.

Freemason in Tanzania
Mpaka sasa Dini hii ya kishetani inamiaka zaidi ya 79, toka ilipoingia hapa nchini Tanzania na member wake wamezidi kuongezeka na kuwa wengine sana kati ya miaka ya 1985- 2000 kwa kutaka kupata Mvuto kisiasa, Kiutamaduni, Kimichezo, Kimuziki, Uigizaji na wengine katika biashara na mambo mengine. Lakini hili la Siasa ndo limeshika hatamu sana, Tafadhali Fuatilia Mikutano ya Bunge na uone Je Ishara hizo hapo juu hazitumiki? Jibu unalo wewe!!!


Hili ni Hall lililoko Mtaa wa sokoine Liko mkabala na Hotel ya Kilimanjaro Kempisky, na wageni wengi hufikia Hotel hiyo kwa urahisi wa Mikutano yao, kwani mambo yao huendeshwa kwa usiri mkubwa sana.

Hawa ni Mafreemason Wakishiriki kwa Pamoja katika shughuli ya upandaji wa Miti, Nadhani sasa utaanza kuelewa Kazi na shughuli wanazo jishughulisha na hawa watu,, NAOMBA TUWE MAKINI SANA NA HAWA WATU, AMBAO HUFANYA VITU VINGI VIZURI ILI KUKUVUTA NA WEWE UJIUNGE. FUMBA MACHO MKUMBUKE MUNGU WAKO KISHA WAKEMEE.


Huyu Jamaa ANAITWA Sir Andy Chande Mtanzania wa kwanza kukiri kuwa Yeye ni Mwanachama wa Freemasons

Hawa jamaa hapa Tanzania wamesaidia kituo cha watu wenye ukoma cha kindiwi wilayani Utete; Kituo cha watoto cha Mama Theresa; shule  ya Vipofu ya Pongwe, mkoani Tanga; Kituo cha yatima cha Arusha, Hospitali ya Mnazi mmoja kula Zanzibar; na Shule ya Viziwi ya Buguruni.


Hiyo ni Form Maalumu ya kujiunga na Hao watu na ukisha jiunga situation inakuwa kama hivyo hapo kwenye picha.

Wanahitaji nini 1. Kujua siri ambazo Mungu amezificha kuhusu Binadamu, na Umungu, na kuisambaza dini yao Duniani kote kwa kupaza sauti yao, ili sikumoja Shetani atawale Dunia 2. Wanataka Dunianzima waabudu Mfumo wa Sayari (Pentagram Cycle of Venus. )ambao wao ndo Mungu wao 3. Kudesign and kujenga miji Muhimu na mikubwa duniani kama Washington 4. Na kuiteka Dunia ili wawe na wafuasi Wengi kuliko wanao Muabudu Mungu

Ushauri Wangu.
Jamani Hawawatu wanatumia njia nyingi sana kuwarubuni watu Duniani Kote, Na mara nyingine hutuma Messages kwa Hardcoppy au Emails kudanganya kuwa Wao walifanikiwa kwa kusambaza ujumbe huo kwa watu wengi (huwa inakuwa kuanzia 7 hadi 14)
Hawamuabudu Mungu na wanamuabudu shetani, na Dini yao inanguvu sana imewateka Watu wazito wote unaowajua wewe Tanzania, Kenya Uganda na Duniani kote, Kama unavyoona Picha hapo juu


Freemason wanaabudu hiki hapo juu.

Nadhani sasa nimejibu maswali mengi ya watu na kama kuna kingine kunahitaji kujua basi tuulizane tu kwa kutumia Address Hiyo hapo chini.