Blogger Widgets

Celebrity Story from Different Place

Entertainment story of Bongo land and their work.

Story za wakali wa majuu

Burudani| Video| Tracks na Maisha yao.

Bongo Movie na wasanii wake kwenye maisha yao

News Movie| New Story| New Skendo.

Mafanikio

Story za walio vuka boda na mafanikio yao kama wajasiria-mali.

Elimika na Burudika

Life ya wasio na skendo na wenye skendo| Mafanikio yao na vioo wa jamii.

Sunday, March 31, 2013

TOUR YA DIAMOND KANDA YA ZIWA YAFIKIA BUKOBA, BARABARA ZAFUNGWA, HUU NDIO UMATI WA WATU ULIOMPOKEA


kanga moja pia walikuwa ndani...
haatariiii














waacheni watoto waje kwangu..












 

HAWA HAPA WALE MACHANGUDOA DODOMA WALIOKAMATWA NA VIDONGE VYA ARV'S, WAPENDA MACHANGU KUWENI MAKINI SANA


WANAWAKE watatu raia wa Rwanda wanaosadikiwa kuendesha biashara ya ukahaba mjini Dodoma wamekamatwa na kupewa siku tatu kuondoka nchini, huku wawili kati yao wakikutwa na vidonge vya kupunguza makali ya virusi ya Ukimwi (ARVs).

Kukamatwa kwa wanawake hao ambao ni Esperance Hagenimana (28), Vestina Zaninika (27) na Ziada Mukamurera (25), kunafuatia mmoja wao Esperance kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi kuwa alikuwa ameibiwa fedha taslimu Sh 800,000 na hati ya kusafiria.

Lakini, Polisi walipofika nyumba ya kulala wageni waliyofikia iliyopo eneo la Area D walikuta wanawake wengine wawili ambao walikuwa wakikaa chumba kimoja na Esperance.

Uchunguzi wa Polisi ulibaini kuwa mwanamke huyo hakuibiwa na kubaini wote si raia wa Tanzania. Hata hivyo kilikosekana kifungu cha kuwashitaki ndipo waliamua kupeleka sakata hilo Uhamiaji ili liweze kushughulikiwa.

Kulingana na maelezo yao, Esperance alitangulia kuja nchini kisha kuwaita wenzake ambao ilikuwa ni mara ya kwanza kuja nchini, lakini hata hivyo alisema kuwa, kumekuwa na makundi ya wanawake kutoka Rwanda wanaokuja nchini kipindi cha Bunge na hata mwaka jana kuna kundi lilikuja wakati wa mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Kulingana na uchunguzi uliofanywa na Uhamiaji, wanawake hao waliingia nchini na kujitambulisha kuwa walikuja Dodoma kufanya biashara ya vitenge, lakini hawakuwa hata na kitenge kimoja ambacho kingeweza kuwaonesha kuwa walikuwa wakifanya biashara hiyo.

Juhudi hizo za Uhamiaji zinadaiwa kuwafikisha hadi klabu moja maarufu ya usiku iliyopo eneo la Area D ambapo walinzi wa Kimasai walikiri kuwafahamu wanawake hao na walikuwa wakiwafuata nyumba ya wageni waliyofikia kama mtu alikuwa akiwahitaji na walikuwa na ni wateja wa klabu hiyo ya usiku.


Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Naibu Kamishna wa Uhamiaji, Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Dodoma, Norah Massawe alikiri kukamatwa kwa wanawake hao na polisi na kukabidhiwa Uhamiaji.

Alisema mwanzoni wanawake hao walidai kuwa walikuja Dodoma kwa ajili ya kununua vitenge kwa ajili ya biashara na waliposhikiliwa na Polisi kwa siku kadhaa waliomba kurudishwa nchini kwao.

Alisema wawili kati yao walikutwa wakiwa na vidonge vya ARVs, lakini haijafahamika moja kwa moja kama walikuwa wagonjwa au la.

“Siwezi kusema walikuwa ni makahaba bali wanahisiwa hivyo kutokana na biashara waliyosema wanafanya kutoeleweka na hata maelezo ya walinzi wa klabu ya usiku kuwa walitambuliwa kama wateja wao, kwa kweli hilo siwezi kulithibitisha,” alisema.

Aliwataka wananchi kuwa makini na watu wasiowafahamu kwani hivi sasa Mkoa wa Dodoma umekuwa na mwingiliano mkubwa wa watu hasa katika kipindi cha Bunge.

Mwandishi wa habari hizi, alimtafuta Mratibu wa Ukimwi Mkoa wa Dodoma, Audrey Njelekela ambaye alisema kuwa, wamekuwa wakitoa elimu kuanzia ngazi ya Mkoa hadi mtaa ambapo kuna timu ya Mkoa ya Ukimwi na hata kwenye halmashauri kuna waratibu ambao wamekuwa akitoa elimu juu ya masuala mbalimbali yanayohusu Ukimwi.

Alisema kuwa kwa sasa kiwango cha maambukizi kwa Mkoa wa Dodoma ni asilimia 2.9 kwa takwimu za mwaka 2011 na 2012 ikilinganisha na takwimu za mwaka 2007 hadi 2008 ambapo kiwango cha maambukizi kilikuwa asilimia 3.3.

Alisema kuwa waratibu wa ngazi ya halmashauri wamekuwa wakitoa elimu juu ya kujikinga na maambukizi ya Ukimwi kwenye maendeleo mbalimbali ikiwemo klabu za usiku.

Alisema kwa kuwa kondomu zinasambazwa maeneo mbalimbali yakiwemo ya starehe ni vyema wananchi kuhakikisha wanazitumia. “Matumizi ya kondomu ni muhimu sana kwani maeneo ya klabu za usiku na maeneo mengine ya starehe watu wengi wanachukuana tu lakini wanakuwa hawafahamiani,“ alisema.

Alisema kuwa kutokana na mwingiliano mkubwa wa watu katika Mkoa wa Dodoma hasa kipindi cha Bunge, umakini zaidi unahitajika.

CHANZO: HABARI LEO

MAGAZETI YOTE YA LEO YAKO HAPA, TAZAMA YALICHOANDIKA MWANZO NA MWISHO

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.