Blogger Widgets

Celebrity Story from Different Place

Entertainment story of Bongo land and their work.

Story za wakali wa majuu

Burudani| Video| Tracks na Maisha yao.

Bongo Movie na wasanii wake kwenye maisha yao

News Movie| New Story| New Skendo.

Mafanikio

Story za walio vuka boda na mafanikio yao kama wajasiria-mali.

Elimika na Burudika

Life ya wasio na skendo na wenye skendo| Mafanikio yao na vioo wa jamii.

Friday, June 28, 2013

SABABU 5 ZINAZOKUFANYA UOE AU KUOLEWA NA MTU AMBAE SI CHAGUO SAHIHI KATIKA MAISHA YAKO


KUNA baadhi ya sababu zinazosababisha watu kuoana pasipo kufanya maamuzi sahihi. Wanandoa wengi huingia katika ndoa wakitegemea mambo mengi kubadilika, kitu ambacho ni makosa yanayosababisha ndoa nyingi kuvunjika.
Kabla ya kuoa/kuolewa unapaswa Ujitambue Kwanza na ujiulize maswali kadhaa, kwanza jiulize; (1) Je huu ni wakati sahihi? (2) Kwa nini mtu huyu? na (3) Unamuoa au kuolewa na mtu atakaye  kuwa sambamba na malengo yako katika maisha yako yote?

Wakati kuna sababu kadhaa za kumuoa/kuolewa na mtu sahihi, pia upande mwingine kuna sababu kibao zinazopelekea watu kuoa watu wasio sahihi kwao. Kabla ya kusema "Ndiyo" zingatia sababu tano hapa chini zinazokufanya uoe au kuolewa na mtu ambaye si sahihi ambae baadae hupelekea kutengana na kupeana taraka.

(1) Tumekuwa katika mahusiano kwa muda mrefu. Kuwa katika mahusiano kwa kipindi kirefu sio sababu pekee ya kufanikiwa kumpata mwenye mafanikio katika maisha yako, unaweza ukawa umemvumilia kwa muda mrefu na sasa ukaamua tu kwasababu umekwisha zoea tabia yake na kufuata usemi wa "maji ukisha yavulia nguo sharti uyaoge".
(2) Msukumo wa Marafiki - Rafiki zangu wote wamekwisha OA/KUOLEWA....... itabidi na mimi nioe/niolewe. Kufuata mkumbo wa makundi katika jamii sii kitu kizuri, kwani ndoa siyokitu cha kubeep na kuacha. Jipange kwanza na muda ukifika basi itaingia katika ndoa yenye mpangilio mzuri wa maisha.
(3) Sidhani kama nitaweza. Usipo jiamini na kujipenda mwenyewe sidhani kama itakuwa rahisi kumpenda mtu mwingine unayetegemea kuwa nae maishani.
(4) Mategemeo ya kuboresha tabia ya mwenza wako. Tukisha oana nitambadilisha tabia. Cheti cha ndoa siyo leseni ya kumrazimisha mwenzi wako kubadilika kwa lazima. Jaribu kuwa na subira na kumtafuta mwenzi mnae endana nae kitabia.
(5) PESA - Anakazi nzuri naamini ataleta pesa au anatoka katika familia ya kitajiri. Kunaukweli mkubwa katika misemo ya wahenga yani "kama ukiowa kwaajili ya pesa, basi utazilipa" japokuwa kuwa na pesa sio vibaya, lakini hii haitazuia pia haizuii kuwa na muunganiko mbaya wa ndoa.

Wanandoa wengi huingia katika dimbwi hili ambapo wengine hushinikizwa kuoa kulingana na taratibu za kimila au kidini. Lakini pia wazazi wakati mwingine huchangia ndoa nyingi kuvunjika, ikiwa ni kwa kuwachagulia wananandoa mke au mume.

Vijana ambao bado hamjaoa au kuolewa "Jitambueni Kwanza", fikirini kwa kina kabla ya kufanya maamuzi yasiyo sahihi ambayo yatawagharimu muda wenu na kupata mateso ya muda mrefu.

WEMA SEPETU AFUNGULIWA MASHITAKA!!

MMILIKI wa Kampuni ya Filamu ya Endless Fame, Wema Sepetu hivi karibuni amejikuta kwenye wakati mgumu baada ya majirani zake kumshitaki kwenye serikali ya mtaa kufuatia tabia ya wafanyakazi wake kutiririsha maji machafu mtaani.     Taarifa iliyolifikia inadai kuwa, majirani wa Wema katika eneo analoishi, Kijitonyama jijini Dar wamekuwa wakimlalamikia msanii huyo kwa kitendo hicho lakini imeonekana uvumilivu umewashinda.     “Mara kwa mara wafanyakazi wake wamekuwa wakitiririsha maji hapa mtaani sasa leo tumeona tukamshitaki serikali za mitaa ili sheria ichukue mkondo wake,” alisema mmoja wa majirani wa staa huyo aliyeomba jina lake lisiandikwe .   Juni 26, mwaka huu Ijumaa lilifika kwenye nyumbani kwa Wema na kushuhudia maji yakitoka kisha kuzagaa mtaani na muda mfupi baadaye alifika Afisa Mtendaji wa Kata ya Makumbusho (jina halikufahamika mara moja) ambaye aligonga kwenye nyumba ya Wema, baada ya muda alitoka binti wa kazi aitwaye Bite.     Katika mazungumzo yao, Bite alionekana kujitetea lakini baadaye ilibainika wana makosa na akatakiwa kwenda ofisi za kata kwa maelezo zaidi.     Amri hiyo ilionekana kuwa ngumu kwa Bite na wafanyakazi wenzake ambapo busara zilitumika na kiongozi huyo wa serikali akataka walipe faini na kuwaonya waache tabia hiyo.     Kufuatia hatua hiyo, Bite aliingia ndani (inadaiwa alikwenda kumtonya Wema) ndipo alipotoka akiwa na fedha ambazo Ijumaa halikujua ni kiasi gani, wakasainishana kisha mchezo ukaishia hapo.  Jitihada za kumpata Wema kuzungumzia sakata hilo ziligonga mwamba kutokana na msanii huyo kutopokea simu na hata mwandishi alipofika nyumbani kwake aliambiwa hayupo.

JAQLINE WOLPER GAMBE AFUNGUKA:MAPENZI YA KWELI NDIO MPANGO MZIMA PESA BAADAE

Nyota katika tasnia ya filamu Swahiliwood Jaqueline Wolper ‘Wolper Gambe’ amedai kuwa hawapendi sana wanaume wenye fedha kwani wengi wao ni waume za watu, kwa hiyo kwa kuwa nao si rahisi kuonyesha mapenzi yao ya dhati kwake kwani mapenzi yao ni chumbani tu, lakini hawezi kutembea nao hadharani kwa kuhofia ndoa zao.Unajua unapokuwa na mtu mwenye fedha zake alafu mtu mzima hivi unakosa penzi la kweli kwani mapenzi yenu ni chumbani tu, hamuwezi kutembea pamoja kukaa kama vile ni wapenzi lakini ukiwa na kijana ambaye ni rafiki hana pesa na wewe una kazi lazima akuonyesha jinsi mapenzi yalivyo kwa kukuweka karibu kimahaba na wewe ukafaidi penzi kutoka kwake”,

“Wengi watu wenye pesa zao kuna wakati wananiona nina dharau lakini mimi ni binadamu nahitaji haki yangu kama mwanamke ya mtu anayenijali na kuwa karibu na mimi sasa kuna watu wanaamini pesa zao ndio kila kitu, kiukweli kwangu siyo hivyo ukileta mapenzi hayo lazima unione nina dharau”,anasema Wolper Gambe.

Aidha kuna watu ambao uwanyooshea vidole wasanii maarufu kama yeye kwa kuwaona kama vile ni Malaya lakini wanasahau kama nao ni binadamu na wanaroho kama wanadamu wengine wao si malaika wanapenda na kupendwa, kwa hiyo ukimuona ana kijana Serengeti boy ujue ni kwa ajili ya kupata penzi nzito na kusikilizwa haja zake.

ANGALIA PICHA YA DIAMOND PLATNUM AKIWA NA UMRI WA CHINI ya MIAKA 5

KAJALA ATAKIWA KUACHA UNAFKI

   

Na Mwandishi Wetu
BAADHI ya wasanii wa filamu Bongo wamemtaka mwenzao, Kajala Masanja (pichani) kuwa mkweli kuhusiana na ushosti wake na Wema Sepetu kwani kudai kwamba wako sawa wakati ukweli unajulikana ni unafiki.
Wakizungumza na Ijumaa juzikati, baadhi ya wasanii hao walioomba majina yao yasiandikwe gazetini walisema wameshangazwa na maneno ya Kajala kwenye mtandao kuwa hana tatizo na Wema wakati wao wanajua wametofautiana.

“Mlipoandika kuwa Wema na Kajala wametibuana sikushangaa kwani ndiyo ukweli lakini nikaona kwenye mtandao Kajala anasema eti yuko sawa na Wema, aache unafiki, awe mkweli tumsaidie maana sisi tunamjua vizuri Wema. Ili uwe rafiki yake ufunge mkanda,” alisema mmoja wa wasanii hao ambaye pia ni rafiki wa karibu wa Kajala. NA GPL

Thursday, June 27, 2013

Baada ya ile drama ya promota wa kike kumponda Prezzo, na kusema Diva alimlipia gharama zote alipokuja Tanzania ili aonekane naye, Diva afunguka

Well, jana (June26) tuliandika story juu ya mwanamke mmoja mKenya aliyejitambulisha kuwa ni promota anayeishi Ujerumani anayeitwa Ashley Toto, ambaye aliandika status katika ukurasa wake wa facebook akimponda Cash Money Brother Prezzo na kumpa misumari ya moto ikiwa ni pamoja na kusema Prezzo hana cash ya kutosha na anawezeshwa na wanawake. Hapo ndipo alitajwa Diva (japo hakumtaja kwa jina) na kusema alimgharamia kila kitu Prezzo alipokuja Tanzania ili tu aonekane naye au kwa lugha nyingine ‘kujipendekeza’ (maneno yangu).
PREZZ
Sasa Diva Loveness Love “The Bawse” mtangazaji wa Clouds FM hajachukua muda mrefu kujibu baada ya kuisoma story hiyo hapa Bongo5. Diva amemjibu Ashley Toto kupitia twitter, wait a minute! kabla sijakuwekea alichomjibu Toto kwanza nikujuze kuwa amefanya Interview na rapcellency Prezzo, ametweet kuwa atai upload leo, is it to say the dude is in the city (Dar) already ?? tutayajua hayo tukishaisikia hiyo Interview ambayo nahisi itakuwa na majibu ya mambo mengi kuhusu drama zilizoishajitokeza hapa katikati…….by the way na Huddah anaingia Dar kesho Ijumaa (jiongeze kujua sababu za mimi kugusia ujio wake hapa!) Well, back to the story.
Diva Loveness Love baada ya kuisoma habari ya promota huyo mKenya aishiye Ujerumani hapa bongo 5, alitweet kumjibu Toto kuhusiana na Prezzo aliyemshutumu kuwezeshwa na wanawake ili kulinda image yake na kumsema Diva alimgharamikia Prezzo alipokuja Tanzania ili aonekanane naye, haya ndiyo majibu ya Diva…..
‏-@DivaTheBawse: Duh… That woman who is busy dissing @AMB_Prezzo I feel sorry for you. Matter of fact u need to get yo facts right. Shame man.
-“you know. She is crazy. He is The CMB. I just lol’d after that story, saw it @bongofive and I was like whaaat lmaoo!”.
‏- I just saw the story late as I was at the village. Back in town and am like Owkay. This woman man, she is insane!. Wtf
- Lol. Prezzo is The President. She nids to leave him alone , she is a hater ”
- You give some to prezzo? Does it make sense guys? How hard he need so called money? Has she ever thought the meaning of CMB?
‏-Been told I just gave Prezz some what?! Hahaa … Talking really is cheap. Muacheni @AMB_Prezzo plizzz. #President truly is a trend setter
‏- Had interview wit @AMB_Prezzo will Upload it tomorrow thou!. #Cloudsfm #AlaZaRoho #DivaTheBawse thank you

ANGALIA PICHA ZA WEMA ALIVYOZUA TIMBWILI

Wema Isaac Sepetu akiwa amefura kwa hasira.
Na Siafel Paul
STAA wa filamu za Kibongo asiyekaukiwa vimbwanga, Wema Isaac Sepetu amezua bonge la timbwili kwa wafanyakazi wake wa ndani wa kiume na kike akiwemo mlinzi, Amani linakuletea kisa na mkasa.
Tukio hilo lililonaswa na vifaa vyetu vya kisasa vya kunasia matukio ya mnato na video, lilijiri juzikati nyumbani kwa mwanadada huyo, Kijitonyama, jijini Dar na kusababisha majirani kufaidi sinema ya bure ya matusi ya nguoni.
ILIKUWAJE?
Ilikuwa majira ya asubuhi ambapo Miss Tanzania huyo wa mwaka 2006/07, akiwa ametinga dela, nywele bandia nyekundu na miwani nyeusi, alikuwa amejiandaa kwa ajili ya mtoko lakini alipoingia kwenye gari lake aina ya Toyota Lexus Harrier ndipo akagundua tatizo.NA GLOBAL PUBLISHER

...Akimfukuza mlinzi.
Cha kwanza alichogundua ni kwamba gari hilo lilikuwa limeibiwa power window (mashine ya kushusha na kupandisha kioo) zote.
Cha pili ni kwamba alipopiga ‘stati’ gari hilo lilikataa kuwaka kutokana na kuchokonolewa kwenye betri.
Baada ya kuona hivyo, Wema aliwaita wafanyakazi wake wawili, mmoja wa kiume na mlinzi na kuanza kuwawashia moto kuwa walikuwa wakijua kilichoendelea.

...Akimmwagia maji mlinzi.
APANDWA NA HASIRA
Wema alianza kuwahoji kuwa walilifanya nini gari hilo, waliponyamaza kumjibu ndipo akapandwa na hasira na kuanza kutoa mkong’oto kwa kutumia chochote alichokutana nacho mbele yake.

MITUSI MIZITO
Huku akimmwagia maji machafu yule mlinzi wa kiume na kumpiga kwa dekio la plastiki, Wema alikuwa akimwaga mitusi mizito ya nguoni isiyoandikika gazeti kutokana na ukali wake.

...Housigeli akishangaa timwili hilo.
“My friend ninyi ni mabogasi kabisa, nawaambia mtaozea Segerea, mnafanya nini hapa ninyi wa…(tusi) au mna…(tusi kali).
“Ninyi ni …(tusi kubwa likihusisha mama zao), mnakaakaa tu hapa wa…(tusi tena), mnajua bei ya power window? Mnadhani hili ni Toyota? Kwa taarifa yenu hili ni Lexus …(tusi) zenu,” alisikika Wema akitumia lugha ya matusi ambayo asilimia kubwa hayaandikiki kwa namna yoyote kutokana na kupitiliza.
Wema aliendelea kuwakimbiza ndani ya fensi akiwapiga huku sauti ya Martin Kadinda (yule meneja wake) ikisikika, ‘Mwache ataruka ukuta, nenda karipoti polisi’.

...Mlinzi akiwa hoi baada ya mshikemshike.
AMGEUKIA FIONA
Huku akiwa mbogo, Wema alimgeukia mmoja wa mbwa wake aitwaye Fiona na kumuwashia moto huku akimmwagia mitusi: 
“Na wewe Fiona unakaa hapo hapo unamuuzia nani sura badala ya kulinda mlinzi, sipendi mambo ya ki… (tusi).

NI HUJUMA?
Mkurugenzi huyo wa kampuni ya kufyatua filamu ya Endless Fame Production alikwenda mbali na kuwatuhumu wafanyakazi hao kuwa kuna uwezekano wanatumiwa kumhujumu akiahidi kuwakomesha.
“Mnatumwa mnapewa pesa ili mnifanyie hivi…gari litaibiwaje power window likiwa ndani na ninyi mkiwepo? Wa…(tusi) sana ninyi,” alisikika msanii huyo.

...Wema akiporomosha matusi.

Katika hali ya kushangaza, badala ya kumuwashia moto mlinzi anayehusika na usalama nyumbani hapo, Wema ‘alidili’ na wafanyakazi wa ndani tu huku mlinzi naye akishindwa kumuamulia na kubaki kumtazama tu namna alivyokuwa akikimbizana na wafanyakazi hao.

NENO LA MAJIRANI
Kwa upande wao majirani walikuwa wakila chabo na kusikitishwa na mvua ya matusi aliyokuwa akiitoa msanii huyo ambaye ni kioo cha jamii.

...Akiliangalia gari lake.
“Jamani jamani, hivi hajui tuna watoto wadogo ambao hawastahili kusikia matusi makubwa kama anayomwaga?
“Ukweli Wema anatusikitisha sana kwa sababu watoto wanajifunza nini kutoka kwake?” alihoji mmoja wa majirani hao aliyeomba hifadhi ya jina ili na yeye asije akawashiwa moto na msanii huyo.




AMANI LAFUNGASHA VIRAGO
Hadi Amani linafungasha virago maeneo hayo mwanadada huyo alikuwa akijiandaa kwenda kuripoti tukio hilo polisi hivyo tunaendelea kufuatilia kilichojiri. 

Sunday, June 23, 2013

EMBU ONENI UAMUZI HUU WAPENZI HAWA WALIO AMUA KUUCHUKUA BAADA YA KUKATALIWA WASIOANE

Hivi ndivyo walivyoamua kujitoa uhai wapenzi hawa baada ya wazazi wa mvulana kukataa katakata asimuoe msichana ambaye waliapa kuoana.baada ya juhudi zao kugonga mwamba suluhisho ikawa hivi.kisa hiki kimetokea huko congo.je wazazi mna la kusema ikifikia hapa?IKIPENDA ROHO HULA NYAMA MBICHI.NA MAPENZI SIKU ZOTE NI YA WAWILI. kwa kisani ya RAJAB KAMANZA



  

MAAJABU: MTOTO AZALIWA NA MKIA, MAMA YAKE ALIA AKIOMBA MSAADA..Angalia PICHA

Maajabu  ya  uumbaji  yamemfanya  mama  mzazi  wa  Xiao Wei  ambaye  ni  mchina amwage  machozi  akiomba  msaada  wa  kunusuru  maisha  ya  mwanae   mwenye  umri  wa  miezi  7 aliyezaliwa  na  mkia...
Kalio  la  tatu  lipo  kama  mkia  mfupi, wenye  urefu  wa   sentimita  8  ( 8 cm ), katikati  ya  makalio  mengine  mawili.
Akiongea   kwa  uchungu, mama  mzazi  wa  mtoto  huyo  amedai  kuwa  kwa  muda  mrefu  amekuwa  akiwaomba  madaktari  wafanye  upasuaji  wa  tako  hilo  lakini  wao  wamekuwa  wakimjibu   kuwa  hiyo  si  kazi  nyepesi  kama  anavyodhani....
"Tukilikata  litaota  tena, hivyo  hatutakiwi  kukurupuka  na  badala  yake  tutakiwa  kupata  muda  wa  kupitia  vitu  vingi  ukiwemo  mrija  wa  uti  wa  mgongo  ambapo  MKIA  huo  umejiegesha"...Alisema  daktari  mmoja  akimjibu  mama  huyo

ANGALIA PICHA MSANII DIAMOND AKILA BATA NCHINI COMORO



MwanaFA..AJUTA KUANZISHA BIFU NA JIDE,,APOTEZA MASHABIKI,HANA RAHA AAMUA KUFUNGUKA..SOMA ALICHOKIANDIKA HAPA


Kutokana na hilo FA aliamua kufunguka; “Tunaishi na watu hivyo lazima mtagongana, hata mapacha wanakosana na kusameheana, lakini wakati mwingine shida inawafanya mnapatana,” alisema Mwana FA.
 


Mwanamuziki Hamis Mwinjuma, maarufu Mwana FA, amepata wakati mgumu kwa kulazimishwa na mashabiki kutaja jina la Lady Jay Dee, baada ya kuliruka jina hilo alipokuwa akiimba wimbo wa Mabinti ambao ndani yake
kuna jina la Jay Dee.

Tofauti na ilivyozooeleka katika wimbo wa Mabinti, kwa mara ya kwanza Mwana FA aliruka jina la mwanamuziki Lady Jay Dee ‘Anaconda’, hali iliyowafanya mashabiki wamtake arudie tena na kutenda haki.

Mwana FA alisita kwa muda na baadaye aliamua kurudia wimbo huo na alipofika katika kipengele cha kumtaja Jide aliimba kwa kumtaja, hali iliyoufanya ukumbi huo ulipuke kwa shangwe na mashabiki kumtaka arudie tena na tena.

Kutokana na hilo FA aliamua kufunguka; “Tunaishi na watu hivyo lazima mtagongana, hata mapacha wanakosana na kusameheana, lakini wakati mwingine shida inawafanya mnapatana,” alisema Mwana FA.

Awali shoo ilitangazwa kuwa ingekuwa ya watu 400 tu. Lakini mpaka inafika saa nne kasoro usiku, muda uliotangazwa kuanzwa kwa shoo hiyo watu waliokuwa wamefika walikuwa kama 250 tu.

Saturday, June 22, 2013

FILAMU YA MWISHO KUIGIZA MAREHEMU MANGWEA HII HAPA

Marehemu Magwair mwigizaji na mwanamuziki UNAPOONGELEA moja kati ya filamu bora ni filamu ya Copy iliyotwaha tuzo tano, leo tunaongelea filamu hiyo ikiwa ni katika kumuenzi mwanamuziki na mwigizaji wa filamu Bongo Albert Mangweha ‘Ngwair’ aliyefariki nchini Afrika ya kusini, na kuzikwa siku ya alhamisi mkoani Morogoro katika makaburi ya Kihonda.
Albert MangwehaNgwair enzi mwigizaji aliyeshiriki filamu ya Copy.
Msanii huyu pamoja na kuvuma sana katika muziki wa kizazi kipya lakini pia alikuwa mahiri katika uigizaji wa filamu lakini si watu wengi wanalijua hilo Mangweha alishiriki katika filamu ya Copy iliyoshinda tuzo tano zilizoandaliwa na kampuni ya One Game Promotion ya Jijini Dar es Salaam.Baada ya kufanya vizuri katika filamu ya Copy niliwahi kuongea na mpiga wa filamu hiyo kuhusu marehemu Mangweha kutokana na umahiri alionyesha katika filamu ya Copy, kwani hakupenda kushiriki katika zingine mara kwa mara pamoja na watayarishaji wa filamu hiyo kummwagia sifa kuwa ni mwigizaji mwenye uwezo mkubwa tofauti na msanii yoyote unayemjua, naye alisema.
.
ahmed KhalfanKelvin mtunzi na muongozaji wa filamu ya Copy.
“Najua kama nina uwezo wa kuigiza lakini najali sana taaluma na kuheshimu kazi ya mtu mwingine sipendi kushiriki kila filamu kutokana na hadithi husika, lazima nisome Script na kuielewa kama ni nzuri hilo ndio lilotokea katika filamu ya Copy niliipenda story yake ilikuwa nzuri na ya kuvutia,”alimnukuu Rashid Mrutu.Mangweha atakumbuka sana katika tasnia ya filamu kwani inaaminika kuwa filamu ya Copy aliyoigiza akiwa kama mwigizaji msaidizi akiwa na Kelvin ambaye ni kinara wa filamu hiyo mchango wake ulisaidia filamu hiyo kushinda tuzo tano na kuwa filamu bora kwa 2007/ 2008 kama mshindi wa jumla baada ya kushinda tuzo nyingi.
.
Albert MangwehaNgwair katika pozi la picha.
Rashid MrutuRashid Mrutu mpiga picha mahiri aliyerekodi filamu ya Copy
“Mangweha ni zaidi ya msanii wa filamu, mara nyingi unapomshirikisha katika filamu msanii ambaye hajawahi kuigiza na kumpa nafasi kubwa kazi huwa ngumu na kuchosha lakini, Mangweha hatukuwa na muda wa kurudi scene, kwani alishika script vema na hakukosea wala kuongeza maneno ambayo hayakuwepo katika script,”anasema mtunzi wa filamu hiyo ya Copy Kelvin.Rashid Mrutu ambaye alikuwa mhariri na mpiga picha wa filamu hiyo amesema kuwa Mangweha alivaa uhusika katika filamu hiyo na kumfanya mshiriki mwenzie ambaye ni Kelvin kuigiza kwa hisia zaidi na kuifanya kazi hiyo kuwa bora na kuibuka mshindi hizo tuzo tano.
.
Joel Bendera, Ahmed Khalfan, Elizabeth KijumbaKelvin akiwa na mkewe nikita wakipokea moja ya tuzo za Vinara.
“Albert ni mwigizaji wa aina yake katika waigizaji ambao wanamuziki niliofanya nao kazi za filamu hakuna kama yeye, naamini kabisa kama angeamua kuingia moja kwa moja katika filamu basi angewafunika wasanii nyota, kwani anatii muongozaji na kufuata script huku akivaa uhusika,”anasema Mrutu.
Mangweha katika filamu ya Copy aliigiza kama rafiki wa Kelvin ambaye alikuwa mchumba wa Janeth (Elizabeth Chijumba), akipata upinzani kutoka kwa mwigizaji Richie Richie ambaye kutokana na fedha anamtaka Janeth bila mafanikio na kujikuta akitumia nguvu za giza ili ampate Janeth anayempenda Kelvin rafiki wa Mangweha.
Katika filamu hiyo JB ameigiza kama baba yake mzazi wa Janeth ambaye pia anamtaka Ritchie na si Kelvin kwa sababu anahisi kuwa hana fedha na mwanaye asingependa aolewa na maskini mtafaruku unaanzia hapo na kuingia nguvu za giza.
Pamoja na kukutana na nyota wa filamu Bongo kama vile JB, Mzee Olotu, Mama Njaidi, Kelvin, Single Mtambalike, Aunt Fifi, Muhogo Mchungu, lakini ngweiar alionyesha uwezo mkubwa na kuwa kivutio kwa wasanii hao ambao walitamani kumshirikisha katika filamu zao lakini kutokana na msimamo wake ilikuwa ngumu.
Katika filamu ya Copy msanii mwingine kutoka kundi la Chemba Squad ambaye naye alishiriki katika filamu hiyo kama mlinzi wa kimasai alikuwa ni Dack Master, ambaye naye alionyesha umahiri katika nafasi hiyo hata baadhi ya watu kuwashawishi kama muziki wakiona unawasumbua basi waigie katika uandaaji wa filamu na kuwashirikisha wanachemba wote.
Jambo lilojitokeza ni toka siku iliyotokea kifo cha msanii huyo tarehe 28 mwezi May mwaka huu, nakala ya filamu hiyo imetafutwa katika maduka maarufu ya uuzaji wa filamu haipatikani, awali ilikuwa ikisambazwa na kampuni ya Kapico baadae iliuzwa na kampuni ya Steps ambao wamesimama kuizalisha.Filamu ya Copy ilinyakua tuzo ya kuwa filamu bora ya mwaka 2007-2008, katika shindano la tuzo za vinara wa filamu Tanzania Katika hafla ya utoaji wa tuzo hizo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee.
.
Albert MangwehaMarehemu Ngwair enzi za uhai wake.
Filamu hiyo ilinyakua tuzo tano kupitia kwa Khalfan Ahmed ‘Kelvin’ aliyenyakua tuzo mbili za Mtunzi bora na Muongozaji Bora, Rashid Mrutu aliyenyakuwa tuzo mbili za mpiga picha Bora na Mhariri Bora na Elizaberth Chijumba ambeye alinyakuwa tuzo ya kuwa Mwigizaji bora wa Kike.
Tasnia ya filamu na muziki imepoteza msanii muhimu wakati filamu na muziki zikielekea katika urasimishaji na kuwa sekta rasmi, pengine inawezekana wasanii wakajikomboa baad

Thursday, June 20, 2013

Picha za watoto wa wasanii 10 wa Tanzania waliozaliwa hivi karibuni na jinsi walivyo sasa

Huenda miongoni mwa wasanii hawa 10 ulikuwa hufahamu kama wana watoto na wanaitwa baba/mama. Watoto hawa waliozaliwa hivi karibuni wameendelea kukua na hizi ni picha zao za hivi karibuni.
Lauren P Msechu – Peter Msechu
Msechu
83fdce6ed41f11e29a6e22000a1fab27_7
0cb063f2d42011e2b83422000a1f9e4c_7
Maleeka Hamis Mwinjuma – Mwana FA
Maleeka - FA
Sameer Herry – Mr Blue
969450_10200766333593992_1227861651_n
Kayla Shettah Bilah – Shettah
Qylala
Abigail – Rama Dee
BMnvajgCYAAQdq3
Ivan – Roma
1011354_400765743374610_1804872592_n
Ella – Grace Matata
Ella
Steve – Barnaba
12520_562953827059493_212743058_n
Rummy – Bob Junior
942016_10151487047249962_450160898_n
Bob Junior
Albert – JCB Makalla
JCB 2
JCB

BAADA YA MSANII SAJNA KU-COPY IDEA YA "muziki gani" MSIKILIZE NEY WA MITEGO ALICHOKISEMA HAPA

 



Hivi karibuni msanii Sajna ametoa wimbo mpya unaokwenda kwa jina la MPIRA GANI ambayo ameshirikiana na msanii mwingine ajulikanae kwa jina la FREGE, kama umepata bahati ya kuusikia wimbo huo hauna tofauti kabisa na ule wa wasanii wakali bongo hapa niki mkusudia Ney wa mitego na Diamond ambao walishirikiana katika ngoma yao ya HUU NI MZIKI GANI, nisikuchoshe hebu tumsikilize mwenyewe Ney wa Mitego analizungumziaje suala hili la dogo kucopy idea yao.
Baada ya tukio hilo je Sajna yeye mwenyewe anasemaje kwanini aliamua kufanya hivi tena bila ya kuwahusisha wenye ngoma yao na mwisho wa siku ngoma ikawa hewani. Hebu tumsikilize naye anasemaje.
Hizo ndizo kauli zao ndugu, nawapongeza sana hasa Ney wa Mitego kwa Uamuzi wake wakujua kuwa Dogo ni mmoja wa Mashabiki wake na Kwa upande mwingine naye ni Msanii ambaye anatafuta namna ya kutoka hivyo jambo zuri ni ushirikiano katika Inderstry hii ya Mziki.. BIG UP SANA MKUBWA NEY WA MITEGO



LAANA:...Huyu ndo Mchungaji aliyewapa mimba wake za watu sita ndani ya mwaka mmoja...

 MCHUNGAJI mmoja  wa kanisa la Church elders of Faith Ministries Nchini Zimbabwe amejikuta akivuliwa wadhifa wake huo mtakatifu mara baada ya kugundulika kuwapa mimba wake za watu sita katika nyakati tofauti tofauti ndani ya mwaka mmoja. "Kitu alichokifanya mchunagaji huyu ni kibaya sana na mtu kama yeye hatakiwi kabisa kuwa sehemu ya kanisa kwa sasa, kwasababu kile alichokifanya ni kinyume kabisa na maadili ya UKRISTO.Kuna baadhi ya watu wenye hasira kali walitaka kumpiga lakini bahati nzuri wazee wa kanisa waliwazuia "..alisema mmoja wa waumini wa kanisa hilo aliyeonekana kuchukizwa na kitendo cha mchungaji huyo Wahubiri katika kanisa hilo walivujisha kuwa katika kanisa hilo kuna kiongozi mkubwa ambaye ana tabia ya kulala na wake za watu na alipokuja kuulizwa kuhusiana na hilo mchungaji huyo alikuwa na haya ya kusema: "Najisikia vibaya sana na ningependa kuomba msamaha kwa hili nililolifanya na kama nikipewa nafasi nyingine naahidi kutorudia tena. Vile vile nakubaliana na maamuzi ya wazee wa kanisa kuamua kunivua wadhifa wangu mtukufu"... alimalizia mchungaji huyo ambaye alionekana kuwa na majonzi ya kutosha.

KUNA VITU VINGINE UKIANGALIA TU UNAANZA KUONA HURUMA, MFANO TAZAMA HIZI PICHA 6

Cheating Husband Funny SignsSweet Brown even made it on Church signs now.The rain will not stop grandma from going to Bingo NightWelcome Home CheaterCurb Parking Car PaintCaught cheating on facebook