Blogger Widgets

Celebrity Story from Different Place

Entertainment story of Bongo land and their work.

Story za wakali wa majuu

Burudani| Video| Tracks na Maisha yao.

Bongo Movie na wasanii wake kwenye maisha yao

News Movie| New Story| New Skendo.

Mafanikio

Story za walio vuka boda na mafanikio yao kama wajasiria-mali.

Elimika na Burudika

Life ya wasio na skendo na wenye skendo| Mafanikio yao na vioo wa jamii.

Sunday, March 30, 2014

DIAMOND ATAMANI USHOGA!


NYOTA wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amewashangaza watu kufuatia kuvaa wigi (nywele bandia) la mpenzi wake, Wema Isaac Sepetu, kitendo kilichotafsiriwa kuwa ni dalili ya kutamani mambo ya ushoga.

Diamond alinaswa akiwa amevaa wigi hilo kichwani kisha kupiga nalo picha.

ILIVYOKUWA
Hivi karibuni, Diamond alinaswa akiwa amevaa wigi hilo kichwani kisha kupiga nalo picha huku Wema akilitafuta ili alitinge bila mafanikio.

Habari zilieleza kuwa baada ya Wema kutoka nje akiendelea kulitafuta wigi hilo, alipigwa na butwaa kumkuta Diamond amelivaa, tena akionekana kuwa na amani.
Wema Isaac Sepetu na mpenzi wake Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.

WEMA AMWANIKA
“Jamani nimetafuta wigi langu muda mrefu sijaliona, nashangaa namkuta baby wangu (Diamond) amelivaa, lakini limempendezaje?” aliandika Wema kwenye ukurasa wake wa Instagram uliotembelewa na watu kibao.

WANACHOAMINI WATU KUHUSU USHOGA
Kitendo cha Diamond kuvaa wigi hilo, wengi wamekichukulia kama ni dalili zake za kupenda kuwa kama demu ambapo kwa mwanaume huitwa shoga, kwa vile wenye tabia hizo wengi walianza kwa kujihusisha na mambo ya kikekike, yakiwemo mavazi.

Emmanuel Adebayor (kushoto) na Diamond Platnumz wakiwa Four Point Hotel, jijini Lagos nchini Nigeria.
“Unajua watu wengi wanaojiingiza katika mambo ya ushoga huanza kwa kutamani kuvaa vitu vya kike kama nguo, hereni, viatu, kujipodoa na vingine vingi,” alisema staa mmoja ambaye hakutaka kutajwa gazetini.
WANAOMFAHAMU DIAMOND
Watu ambao wanamfahamu vizuri mwanamuziki huyo, walisema huenda fedha ambazo ameanza kuzipata hivi karibuni zimekuwa zikimpeleka puta kwa kufanya vitu ambavyo si sahihi.

ALIANZA MUDA
Miezi kadhaa iliyopita, Diamond na Wema walipokutana nchini China, jamaa huyo alipiga picha zilizomuonesha akiwa amevaa cheni ya mpenzi wake huyo na kuziweka kwenye mtandao wake wa kijamii wa Instagram.

Jokate Mwegelo.
SURUALI KAMA YA WEMA, JOKATE
Mwaka jana akiwa nchini Nigeria, Diamond aliingizwa kwenye mitandao ya kijamii kufuatia kitendo chake cha kuvaa suruali yenye mistari ya pundamilia ambayo wachunguzi walibaini kuwa, Wema na Jokate Mwegelo pia wanazo.

Jokate (kushoto) na Wema.

TABIA ZA MASTAA WAKIKAMATA FEDHA
Mastaa wengi duniani wamekuwa na tabia ya kufanya vitu ambavyo ni kinyume na maadili mara baada ya kupata ustaa na kushika fedha nyingi.

Mfano mkubwa, aliyekuwa mfalme wa Pop duniani, marehemu Michael Jackson, yeye alianza kufanya vituko kwa kujibadilisha ngozi na pua  mwaka 1984 ili aonekane mweupe. Ni baada ya kuwika kwenya anga la muziki huku kiasi kikubwa cha fedha kikiingia mfukoni mwake.
Hali hiyo ilimsababishia kupata ugonjwa wa Vitiligo hadi akaaga dunia Juni 25, 2009. 

ELTON JOHN
Mwanamuziki Elton John wa Uingereza, naye alijikuta akijibadili na kuwa shoga baada ya kuzikamata fedha nyingi.

Mwaka 1984, Elton John alifunga ndoa na mwanamke aliyeitwa Renate Blauel. Mwaka 1988 walitengana, Elton akajiingiza katika mapenzi ya jinsi moja hadi kufikia hatua ya kufunga ndoa na mwanaume mwenzake, David Furnish mwaka 2005.
WHITNEY HOUSTON
Mwanamuziki mwingine ambaye alijizolea umaarufu mkubwa kutokana  na sauti yake nzuri ni Whitney Elizabeth Houston ambaye baadaye alijiingiza kwenye masuala ya usagaji na matumizi ya madawa ya kulevya ambayo aliyatumia kwa muda mrefu na kumsababishia kifo.

Whitney alifariki dunia mwaka 2013 katika bafu la Hoteli ya Baverly Hills nchini Marekani. Vyombo vya habari vilimwelezea marehemu huyo kuwa, alitumbukia kwenye matumizi ya ‘unga’ kwa sababu ya kumiliki mkwanja mnono akiwa na mumewe, Bobby Brown.
UZOEFU
Uzoefu kwamba mashoga wengi huanza kwa kupenda vitu vya mademu upo kwa baadhi ya vijana Bongo ambao nao ni ‘chakra’. Wengi waliowahi kuzungumza na vyombo vya habari wamekuwa wakisema kuwa walikuwa wakipenda kuongozana, kukaa, kuvaa au kulala kwenye vyumba vya dada zao.

chanzo GPL

BINTI KUTOKA KENYA ALIYE WAAMBUKIZA UKIMWI WANAUME KIBAO NCHINI KENYA SASA ANATOKA NA KIBABU CHA KIZUNGU, TAZAMA NA SOMA HAPA


 
Mwanadada Vanessa Cheruto Chettle amabaye alithibitisha kuwa anaishi na HIV na ameshatembea na wanaume wengi bila kutumia kinga wakiwemo watu wenyemajina makubwa nchiniKenya...kama
Shaffie Weru na Nick Mutuma ambao ni watangazaji maarufu nchini humo.



Kwamujibu wa chanzo cha habari hizi (chengwon.com) Vanessa na huyo babu wakizungu mwenye asili ya kiyaudi walikutana kwenye mtandao wakijamii  baada ya babu kupitia akaunti yake kuandika anataka kusaidia msichana mwenye HIV.



Monday, March 24, 2014

Picha 25 za show ya Young Dee,Young Killer na Country Boy Maisha Club.



Image00025
Image00011
Miongoni wasanii waliokuwepo na kuperfoam usiku huo ni pamoja na Dogo Janja,God zilla,Mwana Fa,Young Dee,Young Killer na Country Boy,show hii ilipata sapraiz ya mwanadada kutoka kiwanda cha filamu Bongo Jacquline Wolper ambaye aliimba wimbo wa Fununu pamoja na Young Dee.
Hizi ni baadhi ya picha.
Image00024
Image00023
Image00022
Image00021
Image00020
Image00019
Image00018
Image00017
Image00016
Image00015
Image00014
Image00010

Image00011

Image00012

Image00013

Image00009

Image00008

Image00007

Image00006

Image00002

Image00003

Image00004

Image00005

Image00001

Kwa hisani ya Millard Ayo.  special THANKS kwake.

Sunday, March 23, 2014

KAULI YA MADEE NA BABU TALE VIONGOZI WA TIP TOPBAADA YA DOGO JANJA KUOMBA MSAMAHA ILI ARUDI TIP TOP

Baada ya Dogo Janja kuuomba msamaha kupitia vyombo vya habari uongozi wa Tip Top Connection na Madee aliyemtoa Arusha, Boss wa Tip Top Connection Babu Tale ameiambia tovuti ya Times Fm kuwa anataka rapper huyo aseme ukweli wa yote aliyoyasema awali baada ya kutoka Tip Top.  “Babu Tale ameweka wazi vipengele ambavyo anataka Dogo Janja aviweke sawa.  “Dogo anatakiwa aseme kama kweli aliibiwa, kama kweli alidhurumiwa na kama kweli hajawahi kuishi nyumbani kwa Madee. Anatakiwa aongee dhahiri asifiche, aongee tu ukweli.” Babu Tale ameeleza.  Amegusia pia tukio ambalo lilimsikitisha zaidi wakati Dogo Janja anafanya kazi akiwa chini ya menejimenti ya Mtanashati Entertainment.  “Siku zote kwenye ukweli uongo hujitenga, wakati yuko South Africa alipost picha ‘ningekuwa Tip Top nisingefika huku’. Nilishangaa heeh huyu kutoka huko kijijini kwao alifanyaje hadi kufika hapa  “Wazazi wake nao wakawa wamekubali uongo wa mtoto wao wakaanza kutuongelea na sisi maneno ambayo ni uongo. Ulikuwa uongo wa watoto halafu bado wao wanakandamiza uongo zaidi ya uongo. Kwa kuwa ni mtoto kuna wazazi ambao walisimama nyuma yake ambao nao walikuwa wanasapoti. Aongee ukweli mimi ntamsaidia.” Babu Tale ameeleza.  Babu Tale ameeleza kuwa Dogo Janja ameshamtafuta kwa njia ya simu lakini amemwambia ujumbe ule ule kuwa awaambie ukweli watanzania.  Kwa upande wa dogo janja, ameongea na Tovuti ya Times Fm na hakutaka kuizungumzia kwa undani kauli ya Babu Tale, zaidi alieleza kuwa alichokifanya kuomba msamaha alimaanisha kuwa alikuwa amekosea na hakuna aliyemsukuma kufanya hivyo.  Ameeleza kuwa endapo atakaribishwa tena Tip Top Connection atajiunga na kundi hilo japo ameeleza kuwa kuomba kwake msamaha hakuwa na maana kuwa alikuwa na lengo la kurudi Tip Top.  “Mimi nimeomba msamaha kwa kuwa nataka kuweka mambo sawa na kumaliza tofauti na uongozi wangu wa zamani. Hivyo tu. Wakinikaribisha Tip Top itakuwa poa tu pia…fresh.”  Times Fm ilimtafuta Madee ambaye alisema kuwa bado hajawa tayari kuongelea suala hilo na kwamba mtu anaeweza kuzungumzia suala hilo kwa sasa ni Babu Tale.

Saturday, March 22, 2014

UNAJUA NI KWANINI MSANII TINO ANALIA NA SHERIA YA USHOGA HAPA TANZANIA? ZAIDI SOMA HAPA

clip_image001
MCHEZA sinema za kibongo Hisani Msuya "Tino" ameitaka Tanzania nayo kupiga marufuku suala la jinsia moja 'Ushoga' kama ilivyofanya nchi ya Uganda baada ya hivi karibuni rais wao Yoweri Museveni kusaini sheria hiyo ambayo mtu yeyote atakayepatikana na kosa hilo kuwa anafungwa maisha.

Akizungumza na tovuti hii, Tino alisema kuwa yeye ni miongoni mwa wanaharakati wanaopinga mapenzi ya jinsia moja nchini na ndiyo maana aliamua kutunga filamu yake inayozungumzia suala la kupinga kitendo hicho ambacho ni kinyume na maagizo ya Mungu.


"Naitaka Tanzania nayo kutunga sheria kama ya uganda ili tukomeshe suala hili kwani likiendelea kulelewa miaka ijayo taifa litakuwa na kizazi kilichopotoka na kutuingiza kwenye vita kali na Mungu ambaye aliwahi kuteketeza Sodoma na Gomola kwa makosa kama haya" alisema Tino


credit to swahili

BAADA YA DOGO JANJA KUOMBA MSAMAHA NA KUTAKA KURUDI TIP TOP HII NDIYO KAULI YA BABA YAKE MZAZI JUU YA SWALA HILO..!!

Alhamisi ya March 20 2014 lilitoka tamko ambalo lina maamuzi ya msanii wa bongofleva Dogo Janja kuhusu kuomba msamaha na kuhitaji kurudi kwenye kundi lake za zamani la Tiptop connection na kuyasahau yaliyopita kati yake na aliyekuwa meneja wake pia ambae ni Madee.Stori hii ina pande nyingi sana ambazo zitazungumza kupitia hapahapa kwenye tovuti hii lakini kwa kuanzia, baba mzazi wa Dogo Janja amepata nafasi kuzungumza kwa mara ya kwanza baada ya mtoto wake kuomba msamaha.
Anasema >>’Dogo Janja alishakua mtu mzima na tayari nilishawahi kumwambia achague mahali atakapoona kuna manufaa kwake, akishafanya maamuzi yake huwa ananishirikisha kwenye kujadiliana, tayari alishawahi kuniambia kuwa atafanya maamuzi baada ya kuona Mtanashati hakuna muelekeo wowote na hakuna anachopata ndipo akaniambia baba mimi mtu yoyote au kundi lolote nitakalokubaliana nalo basi nitafanya nao kazi’.
Hayo ni maelezo ya Baba mzazi wa Dogo Janja ambae ametoa baraka zote kwa Janja kurudi kujiunga na Tiptop Connection hivyo kazi imebaki kusikia kutoka upande wa Tiptop kufahamu kama wameukubali msamaha wa Dogo Janja.

source: millard

Wakati Wenger akitimiza mechi 1,000 leo – hizi ndio rekodi zake mbalimbali ndani ya Arsenal

381108_heroa
Kocha Arsene Wenger leo katika mchezo dhidi ya Chelsea atatimiza mechi 1,000 tangu alipoanza kuifundisha klabu hiyo ya London ya Kaskazini.

Akiwa anatimiza michezo hiyo – mtandao wa Opta unaodili na masuala ya takwimu za kimichezo umetoa ripoti ya rekodi mbali mbali za Wenger ndani ya michezo hiyo 1,000.
Takwimu zinaonyesha katika mechi 1,000 ameshinda mara 572, sare mara 235, na amepoteza mechi 192.
Ameshinda makombe matatu ya Premier League, manne ya FA Cup, na manne ya Ngao ya Hisani.
381174Thierry Henry ndio mchezaji aliyemfungia Wenger mabao mengi zaidi, akifunga mabao 228, wakati Patrick Vieira ndio mchezaji aliyecheza mechi nyingi chini ya Wenger, jumla ya mechi 402.

 

Monday, March 17, 2014

WEMA, DIAMOND WACHAPANA

 
Stori: WAANDISHI WETU

Tayari kimenuka! Habari ya mjini wikiendi iliyopita ni madai ya njiwa wapendanao Bongo, Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kuchapana makofi laivu, Ijumaa Wikienda lina kisa na mkasa.
Diamond.
TIMBWILI STUDIO

Kwa mujibu wa shuhuda wetu aliyekuwa eneo la tukio, timbwili hilo la haja lilijiri usiku mnene kwenye studio ya kurekodia nyimbo za Bongo Fleva za Tanzania House of Talent (THT) ambapo Diamond alikuwa akirekodi wimbo wa kolabo…
Stori: WAANDISHI WETU
Tayari kimenuka! Habari ya mjini wikiendi iliyopita ni madai ya njiwa wapendanao Bongo, Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kuchapana makofi laivu, Ijumaa Wikienda lina kisa na mkasa.
Diamond.
TIMBWILI STUDIO
Kwa mujibu wa shuhuda wetu aliyekuwa eneo la tukio, timbwili hilo la haja lilijiri usiku mnene kwenye studio ya kurekodia nyimbo za Bongo Fleva za Tanzania House of Talent (THT) ambapo Diamond alikuwa akirekodi wimbo wa kolabo na msanii wa Kenya, Victoria Kimani ‘Vicky’ na Omary Faraji ‘Ommy Dimpoz.
Stori ni kwamba wakati wasanii hao watatu wakifanya yao studio, Ommy alichukua kipande cha video kilichowaonesha wakiwa pamoja huku Diamond akiwa ‘veri klozi’ na Vicky kisha akakitumbukiza kwenye ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram.
Wema.
MUVI YAANZA
Hapo ndipo muvi lilipoanzia kwani ilisemekana kuwa Wema ‘Mama la Mama’ alikiona kipande hicho cha video ndipo akaunganisha na ule uvumi wa Diamond ‘kuminya kimalavu’ na Vicky walipokuwa nchini Afrika Kusini ‘Sauz’.
Ilidaiwa kuwa Wema alimtafuta shostito wake kwa sasa, Aunt Ezekiel ambaye alimuomba ‘amdraivu’ hadi katika studio hizo lakini yeye (Aunt) hakushuka kwenye gari aina ya Toyota Lexus Harrier la rangi ya pinki.
Mastaa hao wawili ambao wameurudisha uhusiano wao hivi karibuni baada ya awali kuvunjika, walijikuta kwenye ugomvi mkubwa mara tu Wema alipozama studio na kukutana na wasanii hao.
Diamond na Victoria.
UHUSIANO GANI?
Ilidaiwa kuwa Wema alipofika alimhoji Diamond ana uhusiano gani na Vicky huku akimkumbusha kuwa siku chache zilizopita kulikuwa na tuhuma za wao kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi.
Ilisemekana kuwa mzozo huo ulianza taratibu lakini baadaye ulikuwa mkubwa hadi kufikia hatua ya kuchapana makofi huku Ommy na prodyuza Tuddy Thomas wakifanya kazi kubwa ya kuwaamulia bila mafanikio.

UGOMVI SAA MBILI
Kwa mujibu wa ‘kronometa’ yetu, ugomvi huo ulidumu kwa zaidi ya saa mbili huku Diamond akidaiwa kuichukua simu ya Wema na kuipasua chini.
Ilidaiwa kwamba wakati wawili hao wakipeana ‘nakozi’, kila mmoja alikuwa akimtupia mwenzake lugha ‘mbofumbofu’ kama ‘wewe umetembea na fulani’ huku mwingine akimwambia ‘na wewe mbona umetembea na fulani na fulani na fulani na fulani na fulani na…’.
Ilielezwa kwamba kauli hizo zilimfanya Diamond aishie kumwambia Wema kuwa yeye ndiye anamuweka mjini kwa sasa hivyo afunge mdomo wake.
Ilidaiwa kuwa Wema alipoendelea na maneno ndipo Diamond akapandwa na hasira hadi akamchania mwanadada huyo dela sehemu ya mgongoni.
“Asikwambie mtu, palichimbika kweli,” kilisema chanzo hicho.

WAACHANISHWA
Baada ya Ommy na Tuddy kufanikiwa kuwaachanisha, Wema alitoka kwa hasira kisha akatimua. Uzuri ni kwamba hakumgusa Vicky.
Baada ya kuzinyaka habari hizo, gazeti hili lilimsaka Ommy ambaye alikiri kutokea kwa ishu hiyo huku akidai ni masuala ya kawaida katika mapenzi.
Kwa upande wake Diamond simu yake iliita bila kupokelewa na hata alipotumiwa ujumbe mfupi (SMS) hakujibu.

WEMA ATOA LA MOYONI
Alipotafutwa Wema, alieleza ya moyoni juu ya sakata hilo ambapo alisema hayo ni mapenzi na ndiyo raha ya mapenzi.
“Kwenye uhusiano kugombana ndiyo raha yenyewe, mapenzi huwa hayaingiliwi nampenda na nitampenda maisha yote.
“Kama ni mjinga, taahira ndiyo tayari amekwishakuwa wangu, kumbuka kuna usemi kuwa chukua jembe ukalime,” alisema staa huyo anayeaminika kuwa maarufu zaidi kwa sasa Bongo.

DIAMOND NA VICKY
Uvumi wa kuwepo kwa uhusiano wa kimapenzi kati ya Diamond na Vicky ulivuma baada ya wawili hao kuonekana kwenye picha ya pamoja wakiwa katika One Project Campaign nchini Afrika Kusini.
Hata hivyo, wote walikana kwa nyakati tofauti.

SI MARA YA KWANZA
Kuhusu Wema na Diamond kupigana siyo mara ya kwanza kwani jamaa huyo anayeuza zaidi muziki wa Bongo Fleva aliwahi kumtoa nundu mrembo huyo enzi za uhusiano wao wa awali.
Imeandaliwa na Imelda Mtema, Musa Mateja na Shakoor Jongo. GBL

Friday, March 7, 2014

HIKI NDICHO ALICHOFUNGUKA DIAMOND KUHUSIANA NA YEYE KUWA

Exclusive Interview! Staa anayeuza zaidi kwa sasa kwenye muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul Jumaa ‘Diamond Platnumz’ amefungukia skendo ambazo zimekuwa zikimtafuna kila kukicha huku akieleza kuwa, sasa anajuta kuwa staa, Ijumaa lina mzigo kamili.


Akizungumza na paparazzi wetu katika mahojiano maalum wiki hii, Diamond alisema kuwa amekuwa akivumilia mengi ambayo yanaelekezwa kwake lakini sasa imefika wakati yanamuumiza kwani naye ni binadamu, ana moyo wa nyama na siyo chuma. 


Ni kweli unatumia ndumba kutafuta mafanikio?
Diamond: “Baadhi ya watu wanakuwa na imani hizo kuwa mimi natumia mambo ya kishirikina kutafuta mafanikio lakini kwa wasiojua ni kwamba kila nifanyalo namtegemea Mungu na muongozo wa mama yangu mzazi (Sanura Kassim a.k.a Sandra).
“Hao ukijumlisha na jitihada zangu mwenyewe na kujituma sana ndiyo wanaonifanya niwe hapa nilipo leo.
“Si kwa sababu ya mambo ya kishirikina. Kwanza siamini katika ushirikina.” 


Hili la mama Wema Sepetu kudai umemloga Wema likoje?
“Sijawahi kumsikia mama Wema akisema nimemloga Wema na hata kwenye magazeti sijaona ila siku nikimsikia ndiyo naweza kusema chochote juu ya hilo.”
Unazungumziaje madai ya wizi wa nyimbo za wasanii wenzako?
Diamond: “Kwa hatua niliyofikia mimi si mtu wa kuiba wimbo wa mtu, bali wapo baadhi ya watu wanaopenda kunisukumia skendo kwa sababu wanazozijua wenyewe.
“Wakati mwingine wanaotuponza ni maprodyuza ambao huenda siku za nyuma walitengeneza biti kali kwa ajili ya msanii fulani, msanii huyo akaingia mitini. 


“Siku unakwenda studio kwake anakusikilizisha biti hiyo na ukiiona kali anakuambia uilipie utengeneze ngoma.
“Baadaye ndiyo unasikia msanii mwingine anaibuka na kusema kaibiwa biti au wimbo. Sasa hapo kosa ni la nani?
Kwa nini una msururu wa mademu?
Diamond: “Mimi ni Sukari ya Warembo na ni kweli baadhi nilikuwa nao kwenye uhusiano lakini wengine ni maneno ya watu tu, sijawahi kutoka nao.
“Kuna ambao wanajitafutia umaarufu kupitia kwangu kwa kusema nimetembea nao lakini siyo kweli. Si unajua ukizungukwa na uaridi na wewe unanukia uaridi? Ndivyo hivyo, wapo baadhi wanajitangazia tu ili wapate umaarufu.”
Baadhi ya warembo ambao tayari ameshaelezwa kutoka nao kimapenzi ni pamoja na Rehema Fabian, Pendo Maisha Plus, Jacqueline Wolper, Natasha, Najma Shaa, Jokate Mwegelo, Penniel Mungilwa ‘Penny’ na Wema Sepetu.
Unazungumziaje U-freemason wako?
Diamond: “Mimi siamini juu ya imani hiyo kabisa na sijui kama ipo. Huenda mavazi wakati mwingine yanafanya watu wanahisi hivyo. Kama ni mafanikio niliyonayo, yanatokana na kazi zangu za muziki ambazo kila mmoja anaona.
“Naweza kusema napata shoo nyingi ambazo nalipwa pesa nyingi na mimi situmii pesa yangu kwa anasa. Nawekeza ili baadaye mali zinisaidie nitakaposhuka kimuziki. Huwezi kuwa juu muda wote hivyo ni lazima niwe na tahadhari.”

Ni kweli unawapa mademu mimba kisha kuwatosa hivyo wanachoropoa?
Diamond: “Mabinti wanaoibuka na kusema nimewapa mimba ni walewale wanaotafuta umaarufu ‘kick’ kupitia mimi. Ndiyo maana kuna yule aliyeibuka na kuandikwa na magazeti lakini baadaye alikanusha mwenyewe.
“Najiheshimu na namjua Mola, najua kufanya hivyo ni sawa na kuua.”
Kwa mujibu wa Diamond, kumekuwa na baadhi ya wasanii wenzake ambao wamekuwa wakimchonganisha na mastaa wenzake, mfano ukiwa ni hivi karibuni ambapo alizushiwa kumkandia Ali Kiba ili waingie kwenye bifu.
          CREDIT : GPL