Blogger Widgets

Celebrity Story from Different Place

Entertainment story of Bongo land and their work.

Story za wakali wa majuu

Burudani| Video| Tracks na Maisha yao.

Bongo Movie na wasanii wake kwenye maisha yao

News Movie| New Story| New Skendo.

Mafanikio

Story za walio vuka boda na mafanikio yao kama wajasiria-mali.

Elimika na Burudika

Life ya wasio na skendo na wenye skendo| Mafanikio yao na vioo wa jamii.

Friday, April 3, 2015

Kumbe Charles Hillary kaondoka BBC na kuamua kurudi nyumbani?

 Chaz 1
Miongoni mwa watu ambao sauti zao zimesikika sana kupitia BBC London, ni Mtangazaji Mtanzania Charles Hillary aliyewahi kusikika sana hata kupitia Radio One pia.

Charles Hillary sasa anarudi nyumbani Tanzania na kujiunga na kituo cha Televisheni cha Azam ambapo mhariri wa BBC Afrika Dar es salaam Solomon Mugera aliwaambia wafanyakazi wake kuhusu kuondoka kwa Hillary.

Naibu Mtendaji mkuu wa Azam Tido Muhando alithibitisha Hillary kutarajiwa kujiunga na Azam Media akiwa na historia nzuri kwenye vyombo vya habari kuanzia alipoanza mwaka 1994 Radio one na kabla ya hapo alitokea radio Deutsch Welle na mwaka 2006 alijiunga na BBC.

kwa hisani ya millard ayo

Sunday, March 29, 2015

MAHAKAMA YA KADHI IMEFIKIA PABAYA: WABUNGE WAVURUGANA, MATUSI NA LUGHA ZA KEJELI ZATAWALA DODOMA

Vurugu ,matusi na lugha za kejeli ni miongoni kati ya mambo yaliyotawala semina ya wabunge kuhusiana muswada wa sheria ya kutambulika hukumu zitakazokuwa zikitolewa na mahakama za kadhi hapa nchini wa mwaka 2014/2015.
 
Ni sehemu ya hali ilivyokuwa wakati wabunge waliposhindwa kuvumuliana na kuheshimiana walipokuwa wakichangia mara baada ya Jaji Robert Makaramba alipowasilisha mada kuhusiana na muswada huo hali iliyolazimu ulinzi kuimarishwa ndani ya ukumbi huo kwa hofu kwamba huenda waheshimiwa wabunge hao wakatwangana makonde na ndipo semina ilipoendelea.

Mbunge wa kuteuliwa, Kassim Issa mbunge baraza la wawakilishi,
Dakika chache baadaye ikafika kipindi cha kila mtu kumtafuta mbaya wake ama suluhu ya anachokiamini huku lugha za kutishana zikitawala.
Wakihitimisha semina hiyo muwasilisha mada Jaji Robert Makaramba pamoja na Waziri mkuu Mh.Mizengo Pinda wamesema ujumbe umefika na mapungufu yaliyoonekana yatafanyiwa kazi.
Chanzo:ITV.

Friday, March 27, 2015

HII HAPA KAMA BADO ULIKUWA HAUJAITAZAMA VIDEO YA DIAMOND ft KHADIJA KOPA.