Blogger Widgets

Celebrity Story from Different Place

Entertainment story of Bongo land and their work.

Story za wakali wa majuu

Burudani| Video| Tracks na Maisha yao.

Bongo Movie na wasanii wake kwenye maisha yao

News Movie| New Story| New Skendo.

Mafanikio

Story za walio vuka boda na mafanikio yao kama wajasiria-mali.

Elimika na Burudika

Life ya wasio na skendo na wenye skendo| Mafanikio yao na vioo wa jamii.

Tuesday, October 30, 2012

TAMKO KUTOKA CHAMA CHA WANANCHI(CUF):SERIKALI INAUKUZA MGOGORO ULIOPO BADALA YA KUUDHIBITI


   Mkurugenzi wa Haki za Binadamu CUF Salim Bimani akifafanua jambo kupitia Katiba katika mkutano wake wa kupinga matumizi mabaya ya Operesheni inayofanywa na Jeshi la Polisi na Vikosi vya SMZ kuwatafuta wavunjifu wa amani.
  Baba wa Marehemu Hamad Ali Kaimu ambaye mwanawe alifariki kutokana na kudaiwa kupigwa vibaya na vikosi vya ulinzi na Usalama akitoa maelezo kuhusu mauaji ya mwanawe
   Waandishi wa vyombo mbali mbali vya habari wakifuatilia kwa makini taarifa ya Chama cha CUF iliyotolewa na Mkurugenzi wa Haki za Binadamu CUF Salim Bimani kuhusu kupinga matumizi mabaya ya Operesheni inayofanywa na Jeshi la Polisi na Vikosi vya SMZ kuwatafuta wavunjifu wa amani.
  Waandishi wa vyombo mbali mbali vya habari wakifuatilia kwa makini taarifa ya Chama cha CUF iliyotolewa na Mkurugenzi wa Haki za Binadamu CUF Salim Bimani kuhusu kupinga matumizi mabaya ya Operesheni inayofanywa na Jeshi la Polisi na Vikosi vya SMZ kuwatafuta wavunjifu wa amani.Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar

Monday, October 29, 2012

MWANAFUNZI AJINYONGA MKOANI MBEYA

 Mwili wa Mwanafunzi wa darasa la tatu, Shule ya Msingi Iwambi, Jijini Mbeya Kervin Patrick (8) jinsia ya kiume ukiwa umefunikwa baada ya kufariki dunia kutokana na kujinyonga kwa kutumia kamba ya viatu katika bomba ya maji nje ya nyumba yao.
 Baadhi ya majirani waliojitokeza kushuhudia mwili Mwili wa Mwanafunzi wa darasa la tatu, Shule ya Msingi Iwambi, Jijini Mbeya Kervin Patrick (8)
 Mama mzazi wa marehemu Kervin Patrick (8)Bi Subira Patrick(38) akiwa katika hali ya majonzi kufuatika kifo cha mwanae aliyejinyonga.
Baadhi ya mashuhuda wakiwa wamekusanyika kushuhudia Mwili wa Mkazi wa Kitongoji cha Gezaulole, Kijiji cha Haporoto Kata ya Ihango Wilaya ya Mbeya Vijijini Mkoani Mbeya Mbwiga Mwandele(50 -55)  amejinyonga kwa kutumia mkanda wa Suruali yake katika Ofisi ya kijiji hicho.
Mke wa marehemu Mbwiga Bi Malita Mbwiga(45) wa pili kutoka kulia akiwa na baadhi ya akina mama waliofika kumfariji kufuatia kifo cha mumewe(Picha na Ezekiel Kamanga,Mbeya)

AZAM WAMFUKUZA KOCHA WAO


Bunjak kulia akiwa na Kali Ongala na Daktari wa timu katika mechi ya juzi dhidi ya Simba
Na Bin Zubeiry Blog 
KOCHA Mserbia wa Azam FC, Boris Bunjak amefukuzwa rasmi leo na sasa aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Muingereza Stewart Hall anarudishwa kazini.

Wednesday, October 24, 2012

HII NDIO NDEGE ILIYOSABABISHA KIFO CHA KEPTEIN MAGUSHI BAADA YA KUPATA AJALI WAKATI AKILITUMIKIA TAIFA

jwtz ndege ya jeshi iliyopata ajali Picha za ndege ya JWTZ iliyopata ajali
ndege ya jeshi iliyopata ajali jwtz Picha za ndege ya JWTZ iliyopata ajali
Pichani ni muonekano wa ndege ya Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ), iliyopata ajali juzi. Ndege hiyo ndogo ya kijeshi ya mazoezi, (Military training aircraft) namba JW 9129 ilipata ajali na kusababisha askai mmoja kufariki na mwingine kujeruhiwa katika ajali hiyo wakati marubani wanafunzi wa jeshi wakitumia ndege hiyo kufanya mazoezi.
 
Mmoja wa wanajeshi hao, Kepten Deogratiusi Magushi, alifariki dunia na mwingine kepteni Feruzi Kwidika, alijeruhiwa katika ajali hiyo iliyotokea katika uwanja wa ndege wa Julius Nyerere eneo la airwing Ukonga jijini Dar es Salaam. Picha na JWTZ

HILI NDIO GARI JINGINE AMBALO KUNDI LA KINA LORD EYES LINATUHUMIWA KUIBA.

.
Siku moja baada ya Polisi kutangaza kwamba inamshikilia msanii Lord Eyes na mwenzake mmoja kwa tuhuma za wizi wa vifaa vya gari la Ommy Dimpoz huku wakikabiliwa na mashtaka mengine zaidi ya 30, walioibiwa wanaanza kujitokeza.

Serikali kuivunja Bodi ya Mikopo




Serikali imesema inafikiria kuifumua na kuivunja Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) kwa kuwa imeshindwa kukidhi matarajio ya serikali pamoja na Watanzania wengi kama ilivyotarajiwa wakati inaanzishwa.

Tuesday, October 23, 2012

MAKAHABA WATATUMALIZA JAMANI......HII NI SEHEMU YA RIPOTI YA WIZARA YA AFYA

Utafiti wa hivi karibuni wa wizara ya afya na ustawi wa jamii unaonesha kwamba MAKAHABA waishio dar hufanya ngono zembe na wanaume 15000 kwa siku tena kwa gharama ya juu........
 Biashara hiyo ambayo huwahusisha makahaba 5000 mpaka 10000  huwaingizia  sh. 50000 mpaka 200000 kwa mwezi kutegemea na uzuri wa kahaba husika.........
Utafiti wa shirika la HIV Behavioural and Biological Surveillance ambao umetolewa weekend hii unadai kuwa makahaba hao humudu kufanya mapenzi  na wanaume angalau 5 kwa siku tena bila Kondomu.
KINACHOTIA HUZUNI ni kuwa makahaba 3 kati ya 10 wameathirika na HIV na makahaba 10 kati ya 100 wana magonjwa ya zinaa.
 Ukosefu wa elimu na Umasikini vimetajwa kuwa ni miongoni mwa  vitu vinavyosababisha wanawake hao kujihusisha na biashara hiyo ambayo ni haramu.

WANAFUNZI WA CHUO CHA UANDISHI WA HABARI NA UTANGAZAJI ARUSHA (AJTC) WALIVYOTEMBELEA CHUO CHA WALEMAVU USA-RIVER ARUSHA.


Wakufunzi na Wanafunzi wa chuo cha Uandishi wa Habari Arusha (AJTC ) Mr. Ngobole (mwenye shati jeusi kushoto) na Madam Neem Ezekiel (Mwenye Red na poch nyeusi) wakijadiliana kabla ya kutembelea sehemu mbali mbali za kituo hicho cha walemavu Usar-River Arusha.
Mkurugenzi wa kituo hicho Mr. Diakon Claus Heim(Kulia) na Chaplin wa kituo hicho Mr. Elibariki Kaaya wakitoa maelekzo kwa ufupi.
Wanachuo wakisikiliza kwa umakini
Haya Twendeni kwenye eneo la washonaji wa Viatu ...
Green colourz ilitawala na usomaji mzuri wa bronchure
Viatu mabali mbali wanavyotengeneza walemavu wa kituo hicho.
Viatu vya wazi wanavyotengeneza walemavu wa kituo hicho.
Mafundi mashuhuri wakiwa katika karakana ya kutengenezea viatu tofauti tofauti....wakiwezeshwa wanaweza....!!
Hili ni eneo la ushonaji wa nguo mbali mbali ,maelezo yakitolewa na mkufunzi wa chuo hicho Bw. Rams Mosha.
Maelezo kidogo yakitolewa na mkufunzi wa eneo la ushonaji Bw. Rams Mosha.
Mavazi mbali mbali wanayotengeneza walemavu hao,maelezo yanatolewa na mkufunzi wa eneo la ushonaji Bw. Rams Mosha.
Madam Neema na wanafunzi wake wakifurahia Mavazi...Jamani kimini hichoooo!!!
Kimini hichooooo.....
Mavazi mbalimbali
Huu ni upande wa karakana ya Viungo Bandia (Orthopaedic Workshop) ,hapa maelezo yakitolewa na mtaalam wa eneo hilo Bw. Nanyaro
Hii ni mashine inayotengeneza Viungo Bandia (Orthopaedic Workshop) ,hapa maelezo yakitolewa na mtaalam wa eneo hilo Bw. Nanyaro

Hii ni mashine ya kukatia vitu vinavyotengeneza Viungo Bandia (Orthopaedic Workshop) ,hapa maelezo yakitolewa na mtaalam wa eneo hilo Bw. Nanyaro
Hii ni mashine ya kunyooshea vitu vinavyotengeneza Viungo Bandia (Orthopaedic Workshop) ,maelezo yakitolewa na mtaalam wa eneo hilo Bw. Nanyaro
Hili ni duka la nguo zinazo shonwa na walemavu wa kituo hicho,Madam Neema(mkufunzi wa chuo cha uandishi wa habari Arusha) akifurahia vazi hilo.


Mtangazaji wa kituo cha radio cha MJ FM ARUSHA .Bw Charles akipata picha ndani ya duka la vitu mbalimbali wanazotengeneza walemavu katika chuo hicho.


Zawadi zikiwasilishwa na kiongozi wa wanachuo cha habari cha Arusha(AJTC) YUSUF SHABANI
Mkufunzi wa chuo cha uandishi wa habari Arusha (AJTC) Bw, Ngobole Andrea akitoa zawadi zilizoletwa na wanachuo hao.
Mkufunzi wa chuo cha uandishi wa habari Arusha (AJTC) B, Neema Ezekiel akitoa zawadi zilizoletwa na wanachuo hao.
Picha ya pamoja na baadhi ya wanachuo wawili wa chuo cha walemavu Usar-River Arusha pamoja na wanachuo cha uandishi wa habari Arusha (AJTC).
Kamera man wa kipindi cha STREET CONER(kushoto mwenye orange t-shirt) akipiga picha ya pamoja na baadhi ya wanachuo wawili wa chuo cha walemavu Usar-River Arusha, pamoja na wanachuo cha uandishi wa habari Arusha (AJTC).
Madam Neema Ezekiel akipiga picha na wanachuo cha ulemavu cha Usar-River Arusha
Kiongozi mkuu wa wana-AJTC (mmiliki wa the HOOD infotainment  blog) YUSUF SHABANI (YUSHA) akipiga picha na wanachuo cha ulemavu cha Usar-River Arusha
Presenter wa kipindi cha television STREET CONER, wa AJTC TV akipata machache toka kwa wanachuo cha ulemavu cha Usar-River Arusha.  
KARIBU ARUSHA JOURNALISM KWA MAFUNZO BORA YA UANDISHI WA HABARI NA UTANGAZAJI WA TV NA REDIO, Kwa maelezo zaidi tembelea www.ajtc.ac.tz