Blogger Widgets

Celebrity Story from Different Place

Entertainment story of Bongo land and their work.

Story za wakali wa majuu

Burudani| Video| Tracks na Maisha yao.

Bongo Movie na wasanii wake kwenye maisha yao

News Movie| New Story| New Skendo.

Mafanikio

Story za walio vuka boda na mafanikio yao kama wajasiria-mali.

Elimika na Burudika

Life ya wasio na skendo na wenye skendo| Mafanikio yao na vioo wa jamii.

Friday, April 3, 2015

Kumbe Charles Hillary kaondoka BBC na kuamua kurudi nyumbani?

 Chaz 1
Miongoni mwa watu ambao sauti zao zimesikika sana kupitia BBC London, ni Mtangazaji Mtanzania Charles Hillary aliyewahi kusikika sana hata kupitia Radio One pia.

Charles Hillary sasa anarudi nyumbani Tanzania na kujiunga na kituo cha Televisheni cha Azam ambapo mhariri wa BBC Afrika Dar es salaam Solomon Mugera aliwaambia wafanyakazi wake kuhusu kuondoka kwa Hillary.

Naibu Mtendaji mkuu wa Azam Tido Muhando alithibitisha Hillary kutarajiwa kujiunga na Azam Media akiwa na historia nzuri kwenye vyombo vya habari kuanzia alipoanza mwaka 1994 Radio one na kabla ya hapo alitokea radio Deutsch Welle na mwaka 2006 alijiunga na BBC.

kwa hisani ya millard ayo

Sunday, March 29, 2015

MAHAKAMA YA KADHI IMEFIKIA PABAYA: WABUNGE WAVURUGANA, MATUSI NA LUGHA ZA KEJELI ZATAWALA DODOMA

Vurugu ,matusi na lugha za kejeli ni miongoni kati ya mambo yaliyotawala semina ya wabunge kuhusiana muswada wa sheria ya kutambulika hukumu zitakazokuwa zikitolewa na mahakama za kadhi hapa nchini wa mwaka 2014/2015.
 
Ni sehemu ya hali ilivyokuwa wakati wabunge waliposhindwa kuvumuliana na kuheshimiana walipokuwa wakichangia mara baada ya Jaji Robert Makaramba alipowasilisha mada kuhusiana na muswada huo hali iliyolazimu ulinzi kuimarishwa ndani ya ukumbi huo kwa hofu kwamba huenda waheshimiwa wabunge hao wakatwangana makonde na ndipo semina ilipoendelea.

Mbunge wa kuteuliwa, Kassim Issa mbunge baraza la wawakilishi,
Dakika chache baadaye ikafika kipindi cha kila mtu kumtafuta mbaya wake ama suluhu ya anachokiamini huku lugha za kutishana zikitawala.
Wakihitimisha semina hiyo muwasilisha mada Jaji Robert Makaramba pamoja na Waziri mkuu Mh.Mizengo Pinda wamesema ujumbe umefika na mapungufu yaliyoonekana yatafanyiwa kazi.
Chanzo:ITV.

Friday, March 27, 2015

HII HAPA KAMA BADO ULIKUWA HAUJAITAZAMA VIDEO YA DIAMOND ft KHADIJA KOPA.

Monday, August 18, 2014

ANGALIA PICHA WASANII WALIVYOLISHAMBULIA JUKWAA LA KILI MUSIC TOUR 2014 DODOMA

10 (640x427)11 (640x427)19 (640x427)

20 (640x427)17 (640x480)11 (640x427)16 (640x480)14 (640x480)15 (640x336)13 (640x427)9 (640x427)7 (640x427)6 (640x427)2 (640x427)

KITENGE AONDOKA RADIO ONE

Maulid Kitenge.
MTANGAZAJI wa michezo wa Radio One Stereo, Maulid Kitenge kupitia akaunti yake ya Twitter hivi punde ametangaza kuondoka rasmi katika radio hiyo baada ya kuitumikia kwa miaka 14. Kupitia Twitter, Kitenge ameandika hivi:

Friday, May 30, 2014

IMG_4162

Marehemu Geogre Tyson pichani hapa alikuwa yupo kijiji cha Chilonwa Chamwino kwenye utoaji wa madawati katika shule ya msingi Chaula iliyopo Dodoma. Baada ya kumaliza shughuli hii huku akiwa kama producer wa The Mboni Show mauti yalimkuta majira ya saa 12 jioni masaa 4 tu toka tuanze safari ya kurudi Dar es Salaam maeneo fulani hivi kama unataka kukaribia GAIRO mjini.
Katika gari hilo walikuwa watu 8 ila yeye pekee ndio aliyepoteza maisha na wengine kupata majiraha mwilini pamoja na dereva wa gari hilo. Kwa sasa mwili wa marehemu umehifadhiwa Morogoro katika  hospital ya mkoa Morogoro, baadae asubuhi mwili utaanza safari ya kuelekea Dar es Salaam.
IMG_4166IMG_4176 IMG_4213IMG_4214IMG_4215
Kweli ajuae mwisho wetu ni Mungu pekee. Tunaishi kama vile tunajua maisha yetu yataisha lini kumbe tunajidanganya. Haya matukio yote ni kwa ajili yetu kuamka na kujifunza kitu. Tumrudieni Mungu, tuungame dhambi zetu maana hakuna ajuae siku wala saa yake itakuwa lini. R.I.P Tyson na wote mliotutangulia.
Picha zote kutoka DJ Choka Music.

Friday, May 16, 2014

WEMA, AUNT WAMWINGIZA MKENGE JB


IMEKULA kwake! Wauza nyago kwenye sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu na Aunt Ezekiel Grayson wamemuingiza mkenge staa mwenzao, kaka mkubwa Jacob Steven ‘JB’ baada kukubali mwaliko kisha kumkatalia dakika za mwisho.
Staa wa sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu.

Habari za ndani zilidadavua kwamba JB na wasanii hao walitakiwa kusafiri kwenda nchini Uturuki kwa ajili ya kujifunza utamaduni wa huko ambapo walipelekwa na uongozi wa Ukumbi wa Princess Cassino uliopo Posta jijini Dar.
Katika hali ya kushangaza, uongozi huo ukiwa tayari umeshawakatia tiketi za daraja la kwanza (first class) zinazogharimu kama dola elfu moja (zaidi ya Sh. milioni 1.6) kila mmoja na baadhi ya wasanii kama Vincent Kigosi ‘Ray The Greatest’ na Amri Athuman ‘Mzee Majuto’, Wema na Aunt Ezekiel walikataa siku moja kabla ya safari.
Diza kwenye tasnia ya filamu Bongo, Aunt Ezekiel Grayson.

Chanzo chetu makini kilipenyeza habari kuwa, Wema na Aunt walichomoa safari hiyo baada ya kuhisi haikuwa na maslahi kwao na walivyopeleka maombi yao ya kimaslahi kwa JB, aliwaambia ni safari ya kujifurahisha na hakuna fedha yoyote watakayopata.
Baada ya kuzinyaka habari hizo, Risasi Jumamosi lilimtafuta Aunt ambaye alikiri kuchomoa safari hiyo baada ya kushindwana kimaslahi.
“Unajua ile ni kwenda kutangaza biashara ya mtu kwa hiyo sisi tuliwatajia kiasi cha fedha ambacho tulikitaka kulipwa lakini tulishindwana ndiyo maana tukakataa kusafiri maana hatuwezi kufanya kitu ambacho hakina maslahi kwetu na kwenda kuwafaidisha wengine,” alifunguka Aunt.
Naye Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Nyerere’ aliilaani safari hiyo na kusema kwamba JB ni mnafiki kwani aliwachagua wasanii wachache kwa upendeleo ambao baadhi yao wamemwangusha kwa kutokwenda.

JB.

“Ukweli nimegundua JB ni mbinafsi, nilikuwa naambiwa lakini nikawa namtetea, sasa nimeamini kwamba hafai akirudi lazima nitamuita, nitazungumza naye kwa nini aliamua kufanya hivyo wakati kila kitu kinapotokea iwe safari au vitu vingine huwa sisi Bongo Movie Unity tunashirikishana lakini kwa hili ameona afanye mwenyewe,” alisema Steve Nyerere. 

Tuesday, May 13, 2014

WEMA AWAGOMBANISHA DIAMOND, PREZZO

Stori: Musa Mateja
RAIS wa Wasafi Bongo, Nasibu Abdul  ‘Diamond’ yuko ndani ya bifu zito na mwanamuziki kiwango cha juu kutoka nchini Kenya, Jackson Ngechu Makini ‘Prezzo’ chanzo kikidaiwa ni Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu.
Diva wa filamu za Kibongo, Wema Sepetu 'Beautiful Onyinye'.
Bifu la wawili hao limekuja kufuatia madai kwamba, Prezzo amemtundika Diamond kwenye mtandao akimkejeli kwa kitendo chake cha kurudiana na Wema na kuweka mambo hadharani.
Ilidaiwa kuwa katika maneno yake, Prezzo alikandia akisema anamshangaa Diamond anatamba kuwa ana mpenzi supastaa ambaye ni Wema wakati yeye mwenyewe alishaanguka naye.
Madai yanazidi kusema kuwa Prezzo akaongeza kwa kuandika kwamba, Bongo hakuna mademu masupastaa kwani hata Jokate (Mwegelo) aliyewahi kutamba naye si lolote kwake.
Msanii huyo anadaiwa alikwenda mbele zaidi kwa kusema kama ni ustaa anao yeye mwenye pesa zake na si Diamond ambaye hamfikii kwa lolote.
MASHABIKI WA DIAMOND WAJA JUU
Baada ya kuanika maneno hayo yaliyoonekana kujaa kejeli, mashabiki wa Diamond walimshukia Prezzo na kuanza kumnanga kwa kila mtu anavyoweza mwenyewe ndipo akaanza kuhaha kutaka suluhu kwa Diamond akimuomba meneja wake awakutanishe.
Mkali wa Bongo Fleva nchini, Nasibu Abdul 'Diamond'.
DIAMOND NAYE AWA MBOGO
Akizungumza kwa hasira na paparazi wetu usiku wa kuamkia Mei 11, mwaka huu ndani ya Ukumbi wa Element uliopo Masaki jijini Dar es Salaam, Diamond alisema kufuatia matusi hayo hatarajii kufika kwenye vikao vya usuluhishi na mtu yeyote yule.
“Nimekasirishwa sana na huyu jamaa (Prezzo) amenitukana kwenye mtandao mimi na demu wangu (Wema) huku akijua sijawahi hata siku moja kujihusisha na yeye kwa jambo lolote lile, daa!” alihamaki Diamond.
HASIRA ZOTE HIZO ZIMETOKA WAPI?
Diamond aliyasema hayo baada ya meneja wa Prezzo aliyejulikana kwa jina moja la Asa kumtaka Mbongo Fleva huyo wakutane yeye akiwa na Prezzo ili wamalize tofauti zao.
“Meneja wake aliniita eti tukakae kikao kuyaongea, mimi sioni sababu ya kukutana na Prezzo, yeye ndiye alianza kunitukana hivyo kama anataka kweli kuelewana na mimi basi arejee tena mtandaoni akaombe radhi, nitamuona muungwana.
“Unajua katika muziki ni wachache sana wenye uwezo wa kutumia ustaarabu katika maamuzi yao, wengi wanaamini kumtusi mtu ndiyo njia pekee ya kupandisha jina au kumfanya abusti ngoma yake kumbe huwa ni njia mojawapo ya kujishushia heshima hasa kwa watu wenye busara walio nyuma yake.”
Mkali wa muziki kutoka Kenya, CMB Prezzo.
ANACHOKIAMINI DIAMOND
Akiendelea kuzungumzia ishu hiyo, Diamond alisema anachoamini yeye, Prezzo alifanya vile ili apate kiki kupitia mgongo wake.
“Najua kama alifanya hayo kwa kufurahisha nafsi yake basi ilisuuzika. Anachotakiwa kukifanya kwa sasa ni kurudi mtandaoni akaandike mazuri yangu.
“Kwanza mimi sina hata chembe moja ya chuki na yeye ingawa amenioneshea uswahili wa hali ya juu,” alisema Diamond.
WAKUTANA, WAFUNGIANA VIOO
Hivi karibuni, wawili hao walikutana katika Ukumbi wa Element, Masaki, Dar ambapo Prezzo alikuwa akifanya shoo lakini walifungiana vioo.
TURUDI NYUMA
Siku za nyuma, iliwahi kuripotiwa na vyombo mbalimbali vya habari vya Tanzania na Kenya (hasa magazeti) kuhusu kuwepo kwa uhusiano wa kimapenzi kati ya Wema na Prezzo ambao ulidumu kwa muda mfupi baada ya Wema kumwagana na Diamond.

Friday, May 2, 2014

FADHILA ZA WEMA SEPETU ZAMTOKEA PUANI. KAJALA: SIMLIPI WEMA MIL.13 NG'O!

JAMBO limezua jambo! Zile shilingi milioni 13 alizolipa staa mkubwa wa kike Bongo, Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ mahakamani ili kumnusuru Kajala Masanja kwenda gerezani, zinaendelea kusababisha fukuto na sasa Kajala amejibu mapigo, akisema hatamlipa Wema fedha hizo.
Malkia wa filamu za Kibongo, Kajala Masanja.
Wema na Kajala wapo kwenye gogoro zito kwa muda mrefu huku mashabiki wa mastaa hao waliojipa majina ya Team Wema (wanaomuunga mkono Wema) na Team Kajala (walio upande wa Kajala) wakiukuza ugomvi huo kwa kushambuliana kwa maneno makali kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii.
WEMA KUFUNGUKA
Katika gazeti hili, toleo namba 877 la Aprili 25-Mei Mosi, 2014 la wiki iliyopita, liliandika habari ya Wema iliyokuwa na kichwa; Kwa mara ya kwanza Wema afunguka, asema: NAJUTA KUMLIPIA KAJALA MIL. 13!
Hiyo ilikuwa mara ya kwanza kwa Wema kufunguka baada ya bifu la kimyakimya la muda mrefu ambapo alifafanua chanzo cha bifu lao na namna anavyojuta kumlipia Kajala fedha hizo.
“Kusema kweli najuta kumlipia (Kajala) ile faini ya Sh. milioni 13. Bora angeenda jela miaka saba kuliko kunisababishia matatizo na maumivu kiasi hiki. Mimi sijawahi kumsema vibaya K kisa eti nilimlipia fedha hizo,” alisema Wema katika gazeti hilo.
Alipoambiwa kama Kajala yupo tayari kurudisha fedha hizo alisema:
“Kama anataka kunilipa, anilipe kisha aende jela maana mimi sikumkopesha, nilitoa kwa moyo.”
Diva wa filamu Bongo, Wema Isaac Sepetu a.k.a ‘Beautiful Onyinye’.
HABARI ZA MOTO
Baada ya gazeti hilo kuruka mitaani na Kajala kulipata ndipo akaeleza mambo mazito.
Akizungumza na mwanahabari wetu, Kajala alisema katika vitu ambavyo Wema anatakiwa kuvisahau ni pamoja na kumlipia mahakamani hizo milioni 13.
“Siwezi kumlipa ng’o. Namlipa nini sasa na kivipi? Kwani tulikopeshana? Hakuna anachonidai Wema, hata kama akisema nimlipe, siwezi kufanya hivyo,” alisema Kajala.
Huku akimwaga machozi, Kajala aliendelea: “Unajua haya mambo yanachukuliwa kirahisi tu na wadandiaji wa mambo, ni vile watu hawajui ni kwa kiwango gani hili suala linaniumiza.
“Wema alinisaidia, alinilipia fedha mahakamani wakati ambao nilikuwa na uhitaji na sikuwa na zile fedha. Kama asingejitokeza kunilipia nilikuwa nakwenda jela.
“Lile ni jambo kubwa. Thamani yake haifananishiki na fedha. Ule ulikuwa ni utu tu, sasa leo iweje ligeuzwe kuwa kama deni? Siwezi kufanya hivyo.”
YUPO TAYARI KWA SULUHU
Kwa mara nyingine tena, Kajala alisema kuhusu kupatana na Wema yupo tayari muda wowote, maana haoni sababu ya kuendelea kwa ugomvi huo.
Hii ni mara ya tatu Kajala kuzungumzia suluhu akisisitiza: “Nakosa amani kabisa na huu mzigo. Natamani kuutua. Nipo tayari kukutanishwa naye hata leo tuyamalize.” HABARI YA MJINI
Habari ambazo zimeenea mjini lakini bado hazijathibitishwa zinadai kuwa, Kajala anajiamini kwa sababu anajua fedha alizolipiwa na Wema si zake, zililipwa na aliyekuwa mwanaume (boyfriend) wa Wema, yule kigogo wa Ikulu anayetajwa kwa jina la CK.
“Lile lilikuwa agizo, Wema hakuwa na fedha zote zile kwa ajili ya kumlipia Kajala. Alipewa na CK na kuambiwa amlipie ili asiende jela,” alisema mmoja wa watu wa karibu na mastaa hao kwa sharti la kutotajwa gazetini.
ETI ULIKUWA MPANGO!
Chanzo kinaendelea: “Alivyoingia mitaani, CK akajiweka karibu na Kajala na kumweleza mchongo mzima, kuwa yeye ndiye aliyetoa  hizo fedha kwa hiyo asiwe na wasiwasi.
“Ndiyo maana hata Wema na CK walivyoachana ikawa rahisi kwa CK kujimilikisha Kajala moja kwa moja kwa sababu anaujua ukweli.”
Haya ni madai ya chanzo chetu ambayo hayajathibitishwa na wahusika.
SAFARI ZA CHINA VIPI?
Habari nyingine ambazo bado zinafuatiliwa ili zithibitishwe, zinasema kuwa, safari nyingi za Kajala kwenda China kwa mapumziko huwa anamfuata au kuongozana na CK.
“Hata sasa hivi (juzi Jumatano) wapo safarini China wanakula bata. Yaani haya mambo yamejifunga sana. Yanahitaji hekima sana kuyamaliza,” aliendelea kudai.
BIFU HADI LINI?
Wadau wa tasnia ya filamu Bongo, kwa nyakati tofauti wamekuwa wakipiga simu na kutuma ujumbe mfupi katika chumba cha habari cha magazeti pendwa Tanzania, Global Publishers na kueleza jinsi ambavyo mtaani kunazidi kuchafuka kuhusu sakata hilo huku wengi wakiwataka wayamalize.
“Haya mambo yanakuzwa na watu. Hawa ni wasanii wazuri, wana majina makubwa na wanaendana, nashauri wazungumze, wayamalize. Bifu lao halijengi badala yake linabomoa,” Maimuna Sadallah wa Majani Mapana, Tanga alieleza katika ujumbe wake.
Msomaji mwingine aliyejitambulisha kwa jina la mama Mwaija mkazi wa Mbagala - Maji  Matitu, Dar alikuwa na haya ya kusema: “Haya mambo ya wanangu Wema na Kajala yananichoma sana. Napenda sana filamu zao, nafurahia namna wanavyoshirikiana na kusaidiana. Hebu wamlaani shetani.”
WAZAZI WAOMBWA KUINGILIA KATI
James Sukae wa Kimara-Baruti, Dar alisema: “Hili jambo na umri wao naona ni kubwa sana kwao kulimaliza. Tukisema tusubiri wayamalize wenyewe, haitawezekana ila litazidi kuwa kubwa.
“Kajala ana wazazi wake, Wema naye kadhalika.
Tena hapa nisisitize, wazazi wanaopaswa zaidi kushughulikia hili ni mama zao. Mama Kajala na mama Wema wanatakiwa kukutana na watoto wao ili wawakalishe na kuzungumza.
“Kwangu mimi, mbele ya wazazi ni jambo dogo sana. Hekima zao ni kubwa na bila shaka watalimaliza kuliko kuacha likielea kama ilivyo sasa. Wakipuuzia hili suala litasababisha janga kubwa.”
DAWATI LA IJUMAA
Bado tunaendelea kusisitiza kuwa, Wema na Kajala ni mabinti ambao wanapaswa kushikamana. Alichokifanya Wema kwa kumtolea Kajala milioni 13 ulikuwa ni wema, kugombana kwa sababu nyepesi si jambo zuri. Bado wanayo nafasi ya kuzungumza na kuendeleza urafiki wao. – MHARIRI.

Thursday, May 1, 2014

WEMA, DIAMOND MAHABA BARABARANI

MASUPASTAA ambao ni wachumba (wanasema wenyewe), Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu na Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, walijikuta wakionesha upendo wao mbele za watu kwa kudendeka  barabarani, Amani lilishuhudia.
Nasibu Abdul ‘Diamond’, na Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu wakiwa kwenye pozi la mahaba
Ishu hiyo ambayo wapendanao wengi huifanya kwa faragha, ilijiri hivi karibuni maeneo ya Bamaga- Mwenge jijini Dar es Salaam ambapo ni hatua chache kutoka kwenye Ofisi za Global Publishers ambao ni wachapishaji wa Magazeti Pendwa ya Amani, Risasi, Uwazi, Ijumaa, Championi na Ijumaa Wikienda.
ILIVYOKUWA
Kwa mujibu wa watu walioshuhudia tukio hilo, Wema alikuwa kwenye shughuli zake za kila siku maeneo hayo ambapo alikuwa ameegesha pembeni gari lake la rangi ya pinki aina ya Toyota Lexus Harrier bila kujulikana alikokuwa ameelekea.

Wakionyeshana upendo hadhalani
DIAMOND AIBUKA PEKE YAKE
Ikadaiwa kuwa, mara Diamond naye alitokea bila kujulikana alikotokea akiwa anaendesha gari lake aina ya Toyota Prado na kuegesha gari lake jirani na alipoegesha Wema.

SIMU YAPIGWA CHUMBA CHA HABARI GLOBAL
Mapaparazi wa Global wakiwa katika kazi za kila siku ndani ya ofisi, simu ilipigwa kwa mmoja wao na kutonywa kuhusu wawili hao kuwepo eneo hilo kimahabamahaba.

“Jamani Global hapa jirani na ofisi zenu Diamond amekuja sasa hivi, lakini inaonekana amemfuata Wema maana Wema alishakuwepo muda mrefu uliopita, njooni mchukue picha si ndiyo zenu au bado mna bifu na Wema tangu siku ile alipokuja kuwafanyia fujo?”
PAPARAZI AWAFIKIA
Haraka sana paparazi mmoja alibeba kamera yenye uwezo wa kupiga picha kwa umbali wa mita hata 250 bila mhusika kushtukia na kutoka nayo.

Kweli, lilikuwa tukio lilionesha kushangaza kwani paparazi alikuta wapita njia wakiwa wanapunguza mwendo ili kuwashuhudia wawili hao walichokuwa wakikusudia kukifanya bila kuogopa watu.
WEMA NJE, DIAMOND NDANI
Kamera ya paparazi wetu iliweza kuwanasa wawili hao, Wema yeye alisimama nje ya gari la Diamond upande wa dirisha la dereva na kuongea na mwandani wake huyo jambo ambalo hakuna mpita njia aliyeonekana kushangaa.
Hata hivyo, mshangao ulianza pale Diamond alipotoa mkono nje na kumshika kiuno Wema huku wakiendelea kuongea ndipo baadhi ya wapita njia nao walipokoleza macho kodo, wengine wakihoji kama aliyesimama nje ya gari ni Wema, nani alikuwa ndani ya gari hilo!

Haikuwa rahisi kupata majibu kwani wengi walikuwa wanashindwa kumwona Diamond. Wengine waliamini kwamba, Wema alikuwa ameshikwa kiuno na mwanaume mwingine ambaye huena akampindua Diamond kama na yeye alivyompindua yule kigogo wa ikulu ‘CK’.
“Sasa mbona Wema anakubali kushikwa kiuno hivihivi tu, haoni watu?” alihoji mpita njia mmoja ambaye alijitambulisha kwa jina la Salome, mwanafunzi wa Chuo cha Ustawi wa Jamii, Kijitonyama jijini Dar.
DENDA NJE NJE
Katika hali isiyotarajiwa, baada ya kushikwa kiuno, Wema alikwenda mbali zaidi pale alipomwinamia ‘baby’ wake huyo na kula naye denda ambapo naye mwanaume hakufanya ajizi hata kidogo.

“He! Jamani! Naona wenzetu leo wameamua, hata barabarani? Huu ustaa nahisi unawafanya watu wawe vichaa mbele za watu. Mimi siwezi kabisa kudendeka mbele za watu,” alisema mrembo mmoja ambaye hakutaka kutaja jina lake lakini naye ni denti wa Chuo cha Ustawi wa Jamii ambacho kipo jirani kabisa na eneo la tukio.
DIAMOND ACHOMOKA KWA KASI
Baada ya denda hilo lililodumu kwa dakika moja, Diamond alimuaga Wema na kukanyaga mafuta kuondoka katika eneo hilo huku wananachi wakimfuatilia kwa macho yaliyojaa mshangao.

Monday, April 28, 2014

ANGALIA PICHA ZA MAUAJI YA KUTISHA YALIYOTOKEA SUDAN YA KUSINI,TUITUNZE AMANI YETU.

http://www.ufukunyuku.blogspot.com/ 
Umoja wa Mataifa unasema kuwa vikosi vinavyoipinga serikali nchini Sudan Kusini viliwaua mamia ya watu kwa sababu ya kabila lao wakati vilipouteka mji wa Bentiu wiki jana.Kwa mujibu wa taarifa ya shirika hilo, watu hao walilengwa wakiwa katika maeneo salama walikokuwa wanahifadhiwa kama vile msikitini, makanisani na hospitalini.Umoja huo umesema kuwa watangazji katika baadhi ya vituo vya redio walitumia lugha ya chuki na uchochezi na kuwataka watu wa kabila fulani kuondoka mjini humo huku wakiwashauri wanaume kuwabaka wanawake.



UNGA WAZIDI KUMTESA RAY C

Rehema Chalamila ‘Ray C’ katika pozi.
NA MAKONGORO OGING'
MSANII mkongwe wa muziki wa kizazi kipya Bongo, Rehema Chalamila ‘Ray C’ ambaye aliwahi kuathirika na utumiaji wa ‘unga’, hivi karibuni alitinga ofisi ya kitengo cha kupambana na kudhibiti madawa ya kulevya na kuomba kupatiwa majina, idadi na sehemu walipo watumiaji wa mihadarati hiyo ili aweze kuwasaidia kwa kuwapa somo, kitu kinachotafsiriwa kama bado unamtesa.
Ray C katika harakati zake akifanya mahojiano na msanii wa Hip hop, ambaye yupo mbioni kuachana na madawa ya kulevya, Ibra the Hustler.
Ray C anadaiwa kufika katika ofisi hizo, Aprili Mosi, mwaka huu, saa nne asubuhi hali iliyozua gumzo kwa askari waliomuona ambao walijiuliza kitu alichokifuata.
Akizungumza na Uwazi, kamanda wa kitengo hicho cha madawa ya kulevya, Godfrey Nzowa alikiri kufika kwa msanii huyo ofisini kwake na kutoa madai hayo lakini alimwelekeza kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili kwani huko kuna kitengo kinachoshughulika na watu wenye matatizo ya akili wakiwemo watumiaji wa madawa ya kulevya.
Ray C.
Kamanda huyo alionesha kufurahishwa na kitendo cha msanii huyo ambaye pia anamiliki taasisi yake yenye lengo la kuwasaidia waathirika wa matumizi ya madawa hayo kwa kuwapa elimu, akisema atatoa msaada mkubwa kwa wenzake.
Aliwataka watumiaji wa madawa hayo ambao wameshindwa kuacha, wamfuate msanii huyo ili awape elimu na amewaonya wote wanaotumia na kusafirisha madawa hayo.
“Wote wanaotumia na kuuza madawa hayo waache mara moja kwani kikosi kazi kinachopambana na biashara hiyo kimejipanga kila kona ili kukomesha biashara hiyo haramu,” alisema Kamanda Nzowa.

chanzo: GPL