Blogger Widgets

Wednesday, April 3, 2013

HII NI HATARII:::KANGA MOJA TAZAMA WALIVYOFANYA LAANA KATIKA SHOW YA MSANII DIAMOND HUKO BUKOBA.



Mambo yanayofanywa na hawa wakina dada wanaojiita kanga moja kusema ukweli yanatutia aibu sana japo nao wapo katika kutafuta maisha ila kwa hali hii kusema kweli taifa tunalizika zima zima bila kuliuwa.
Mimi binafsi nimeshahudhuria shoo nyingi za hawa akina dada kwa lengo la kusaka habari huko nimeona mengi ambao mengine si rahisi kuyaanika hapa kutokana na maadili yetu lakini kifupi kinadada hawa wanachofanya mungu atunusuru
Kina dada hawa ambao uchezaji wao hauna tofauti sana na wale wachezaji wa casino maana huvaa kanga moja huku ndani wakiwa wamevaa bikini mfano wa kamba nyembamba kama uzi kisha huimwagia maji au bia  na ikishalowa kabisa huyaanika maungo yao wazi kabisa huku mwenzie akimuingizia chupa nyuma na kisha kuiachia ikisha ingia na mchezaji hucheza nayo na mara nyingine huikalia kwa staili ya kimahaba kana kwamba kakalia mwanume,  Na mara nyingine katika uchezaji wao watu hujikuta wanaona nyuchi zao ila wao hawajali hulewa na sifa za makelele na kujikuta wakiendelea na shoo.
Utafiti wa mtandao huu umebaini kuwa kina dada hawa licha ya kazi ngumu waifanyayo hulipwa ujira mdogo sana ambao haufiki hata laki moja ila kutokana na ugumu wa maisha wamejikuta wakilazimika kufanya kazi hiyo bila kujali

Akizungumza na mtandao huu juzi baada ya shoo waliyofanya na diamond huko bukoba mmoja wa akina dada hilo ambaye hakupenda kutajwa hapa kutokana na kuogopa ataonekana kuwasaliti wenzie alilonga na blog hii pendwa na kusema,Unajua kaka sisi si kama tunapenda kufanya hii kazi ila ugumu wa maisha ndio umetufikisha hapa maana ukituambia tuache hii kazi inamaana unatuambia tukajipange kinondoni makaburini mwananyamala au buguruni kujiuza kitu ambacho sisi tumeshindwa ndio maana tunajitafutia riziki zetu za halali alisema mwadada huyo mapepe kupindukia,mwandishi wetu alipomuhoji wao wanaifundisha nini jamii kwakucheza vile alisema kuwa wao wapo kazini sasa haamini kama mzazi anaweza kwenda sehemu kama ile na mtoto wakati ameshaambiwa kanga moja watakuwepo au wewe kama hupendi shoo shoo hizi sidhani kama utakuja.
Baada ya maswali kadhaa mtandao huu ulitaka kujua wanalipwa kiasi gani kwa shoo ambapo dada huyo alisema Unadhani hata tunalipwa pesa nyingi sana basi pesa yetu ni kama elfu hamsini kwa kila mtu mmoja kwa shoo ila tukisafiri mikowani ndio tunarudi na pesa alisema mwanadada huyo bila kufafanua wanarudi na pesa kivipi
Hii ndio moja ya kazi za dada zetu siku hizi iliyochukuwa umaarufu sana nchini kwa kuteka watu wengi katika shoo zao na kufanya makundi ya namna hiyo kuibuka kila kukicha kwani ni kama wadau au wawekezaji wa sehemu za starehe wamegundua biashara hiyo inawalipa bila kujali madhara kwa taifa hili maana  uchezaji wao wakuwekeana chupa ni sawa nakudhihirisha kuunga mkona vitendo vya ulawiti au ushoga.
Makundi mengine ya dizaini hiyo ni kama Kitu Tigo,Wela Wela,kundi la msanii wa filamu na muziki Shilole Classic, na lile la Sunura Mush ambaye pia ni msanii wa filamu alimfuata shilole katika muziki huo.



















































 

1 comment: