Blogger Widgets

Celebrity Story from Different Place

Entertainment story of Bongo land and their work.

Story za wakali wa majuu

Burudani| Video| Tracks na Maisha yao.

Bongo Movie na wasanii wake kwenye maisha yao

News Movie| New Story| New Skendo.

Mafanikio

Story za walio vuka boda na mafanikio yao kama wajasiria-mali.

Elimika na Burudika

Life ya wasio na skendo na wenye skendo| Mafanikio yao na vioo wa jamii.

Saturday, September 29, 2012

ALICHO KIANDIKA DIAMOND KATIKA WEBSITE YAKE KUHUSIANA NA BRITHDAY YA WEMA SEPETU



Mwaka 1990, mwezi na siku kama ya leo Mrs. Abraham Sepetu ama (Mama Sepetu) alipata bahati ya kujifungua mtoto wa kike ambae alimtunuku jina la Wema Abraham Sepetu, Mtoto ambae Nyota yake ilianza kama masihara tu pale aliposhinda taji la Miss Tanzania 2006, kisha baadae kuingia katika Muvie Industry kama utaniutani vile na ghafla kuwa DIVA wa Tasnia hiyo, na licha tu ya udiva pia kuwa ICON wa Tanzania.Siku hii ya leo ya tarehe 28/09/ anazaliwa upya na kutimiza miaka 22.
the HOOD infotainment inakutakia maisha marefu na yenye baraka

Friday, September 28, 2012

STR8MUZIK Free Style 2012 zang’ara Mwanza

Mmoja wa wanakundi cha waburudishaji cha BFB cha mkoani Mwanza akifanya vitu vyake katika mpambano wa kusaka ma-MCs na DJs wa STR8MUZIK Freestyle 2012 mkoani Mwanza uliofanyika katika ukumbi wa Stone mjini humo jana usiku.

RICK ROSS KUPANDA JUKWAA LA SERENGETI FIESTA, OKT 6

  Msanii nyota kutoka nchini Marekani, mzaliwa wa nchini  Marekani, anayetambulika kwa jina la kisanii kama Rick Ross, ambaye kwa jina halisi anajulikana kama William Leonard Roberts II, anatarajia kutua nchini Tanzania hivi karibuni kwa ajili ya kushiriki kikamilifu kushambulia jukwaa la Serengeti Fiesta 2012, litakalofanyika Oktoba 6 ndani ya viwanja vya Lidaz Club,Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Katika kuhakikisha mambo yanakwenda sawa bin sawia kwa kila idara kuhusiana na tamasha hilo, waandaaji ambao ni Prime Time Promotions Ltd wakishirikiana na Clouds Media Group huku mdhamini wao mkubwa ikiwa ni kampuni ya bia ya Serengeti,wameandaa shamara shamra mbalimbali za kuhakikisha tamasha hilo mpaka linafika kileleni,linaamsha na kuacha gumzo la kipekee kabisa miongoni mwa wakazi wa jiji la Dar na vitongoji vyake, ikibidi mpaka Kigoma mwisho wa reli kwa namna moja ama nyingine.

Msanii huyo mwenye umahiri mkubwa wa kufloo awapo jukwaani mpaka sasa anatamba na nyimbo/albamu kadhaa kama vile  Hold Me Back 2012 God Forgives, I Don't, Hustlin' 2006 Port of Miami Diced Pineapples 2012 God Forgives, I Don't So Sophisticated 2012 God Forgives, I Don't 911 2012 God Forgives, I Don't Stay Schemin 2012 Rich Forever Aston Martin Music. 

Nyinginezo ni  2010 Teflon Don DJ Khaled 2008 Trilla Lemme See 2012 So Sophisticated Amsterdam 2012 God Forgives, I Don't Black Magic 2012 Maybach Music Group Presents Self Made, Vol. 2: The Untouchable Empire The Boss 2008 Trilla You the Boss 2011 You the Boss Touch'n You 2012 Touch'N You Bag of Money 2012 Maybach Music Group Presents Self Made, Vol. 2: The Untouchable Empire.

Wednesday, September 26, 2012

VITUKO VYA BEYONCE WA TANZANIA......

 Huyu ndio beyonce wa tanzania kwajina halisi anajulikana kama mwanaisha idd,ana watoto wawili mapacha wa kizungu .

Anaishi msasani,hana simu na wala hajawahi kumiliki simu hapendi kwasababu kila mara anajikuta akipoteza akiwa na simu, pia hajawahi kwenda club yoyote zaidi ya NEW MAISHA CLUB,

"Maisha ndio home hata nikiumwa nakuja kulala hapahapa au kunywa dawa hapahapa sijawahi kukosa new maisha club napaona kama nyumbani,hata baba watoto wangu nilikutana nae new maisha club."

 Miss triity live na beyonce wa tanzania kwenye stage

 Mashabiki wakicheza na miss trinity na beyonce kwenye stage

 Miss trinity akimshangaa beyonce wa tanzania

Hapa akitoa style zake zakujikunja kama kinyonga

Sunday, September 23, 2012

‘ROSE NDAUKA’ AKAMILISHA FILAMU MBILI ‘UPOFU’ NA ‘SPECIAL COVER’…. KUZIACHIA OCTOBA…!!

 
MSANII mahiri anayefanya vizuri kwenye tasnia ya filamu bongo Rose Ndauka, asema kuwa baada ya kuwa kambini kwa muda mrefu akitengeneza kazi ambazo awali alizitaja sasa zimekamilika na Octoba zinaenda sokoni ambazo ni ‘Upofu’ na ‘Special Cover’ huku zote zikiwa zimefanyika chini ya kampuni yake inayojulikana kama Ndauka Entertainment.

Awali msanii huyo alizungumza na DarTalk ambapo alisema kuwa filamu hizo zipo kwenye mchakato wa kupigwa picha lakini sasa ameamua kuweka wazi kuwa kila kitu kimekamilika na mwezi ujao zitakuwa sokoni kwa ajili ya kuwapa uhondo mashabiki.

Ndauka alisema kuwa ameamua kutoa filamu mbili kwa mpingo kwani mashabiki wake wana hamu ya kuona kazi nyingi zaidi na nzuri kutoka kwenye kampuni yake pia malengo yake ni kujitangaza zaidi kimataifa.

“Nakumbuka niliwahi kusema Octoba nitakuja na filamu mbili kutoka kwenye kampuni yangu kazi zipo tayari hivyo kinachosuburiwa ni ratiba ifike ili mashabiki wangu waweze kuona utamu wa kazi zangu, ujio huo utakuwa ni mzuri kwani utaifanya kampuni yangu iweze kujulikana zaidi kimataifa,” alisema. 

Maisha Plus 2012 usaili wa Dar

 Audition ya Maisha Plus hapa Dar ni Jumatatu kwenye attachment kuna full information.Kwa mliopo Dar, Team Maisha Plus inawaalika mfike Millenium Tower hiyo Jumatatu kuna mengi mazuri ya kushare nanyi kama familia yetu.



Makamu wa kwanza wa Rais Zanzibar na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amelaani kitendo cha vyombo vya dola kuwapiga na kuwakamata wafuasi wa Cuf

  Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Maalim Seif Shaif Hamad akizungumza na wahanga wa vurugu za uchaguzi mdogo wa Bububu huko ofisi kuu ya Chama hicho Mtendeni.
  Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Maalim Seif Shaif Hamad akizungumza na wahanga wa vurugu za uchaguzi mdogo wa Bububu (hawapo pichani) huko ofisi kuu ya Chama hicho Mtendeni.
Mbunge wa Jimbo la Mtoni (CUF) Mhe. Faki Haji Makame akizungumza kwa niaba ya waganga wa vurugu za uchaguzi mdogo wa Bububu, mbele ya Katibu Mkuu wa Chama hicho Maalim Seif Sharif Hamad (kushoto). Picha na Salmin Said-Ofisi ya Makamu wa kwanza wa Rais Zanzibar.

Friday, September 21, 2012

MCHUNGAJI MSIGWA AENDELEZA VUGUVUGU LA MABADILIKO MKOANI IRINGA.

 Mbunge Peter Msigwa akiwa na viongozi wenzake wakati akiwahutubia wananchi Iringa eneo la soko kuu.

Umati wa wananchi uliofurika kumsikiliza

MBUNGE wa Iringa Mjini kupitia chama cha demokrasia na maendeleo(CHADEMA) Peter Msigwa jana ameongea na wananchi wake katika eneo la soko kuu la Iringa.

Thursday, September 20, 2012

HUYU NDIO MWANAMKE ALIOLEWA NA BABA MZAZI NA KUPATA WATOTO BILA KUGUNDUA.

Add caption
Taarifa ambayo imewashtua watu wengi inamuhusu mwanamama Valerie Spruill ambae ameishi na baba yake mzazi kama mke na mume kwa miaka 40 bila kugundua.
kwa mujibu wa Daily Post Nigeria, Spruill aligundua hii siri mwaka 2004 na amewavutia wengi kwa ujasiri wake wa kuiweka wazi kuhusu mumewe ambae kwa sasa ni marehemu.
Chanzo cha yeye kufahamu ni kutokana na kukusanya taarifa mbalimbali ambazo mwanzoni alianza kuzipata kama tetesi za umbea kutoka kwa watu mbalimbali.
Mpaka sasa mama huyu mwenye umri wa miaka 60 ana watoto watatu na wajukuu nane na alifahamu ukweli wa hii ishu kupitia kwa Uncle wake siku chache baada ya kifo cha mume wake.
Umeshawahi kusikia kisa cha aina hii? unemfahamu yeyote? mawazo yako ni yapi ili kuepuka vitu kama hivi? share na mimi kwa kucomment mtu wangu wa nguvu.

Wednesday, September 19, 2012

AJALI MBAYA MKOANI MBEYA: KAMBA YA KUFUNGIA NG'OMBE PAMOJA NA GOGO LA MTI VYATUMIKA KUFUNGIA USUKANI WA BASI LA ABIRIA.



 Sehemu ya chini ya usukani ukiwa umefungwa kwa kamba (ambayo hutumika kufungia ng'ombe) na mti kama uonavyo pichani,katika basi la abiria linalomilikiwa na Kampuni la Mwasha ambalo husafirisha

Tuesday, September 18, 2012

KAMA UMEZALIWA HI LEO UTAKUA UMEZALIWA NA STAR HUU.

MSANII ANAEKIMBIZA KWA STYLE YAKE YA RAGA A. TOWN YUNG OMEGA AMEZALIWA TAREHE 18/09/1992, HII LEO AMETIMIZA MIAKA 20 AMEONGEA NA BLOG HII the HOOD infotainment  ANAFURAHI SANA KUTIMIZA MIAKA HII NA ANAMSHUKURU MUNGU PAMOJA NA MAMA YAKE MZAZI KWA KUMLINDA KWA KIPINDI CHOTE TANGU AMEKUJA DUNIANI HADI HIVI SASA. VILEVILE ANAWAOMBA MASHABIKI WAKE WAENDELEE KUMPA SUPPORT YAKUTOSHA NA WAMUOMBEE KWA MUNGU AENDELEE KUFANYA VIZURI KWENYE HII GAME.

the HOOD infotainment INAKUTAKIA MAISHA MAREFU NA MUNGU AKUJALIE HERI NA MAFANIKIO KATIKA MAISHA YAKO YA MUZUKI NA MAISHA YA KILA SIKU.
 

Monday, September 17, 2012

Usaili video ya Diamond Nyumbani Lounge

diamond
USAILI wa wanamitindo na wachezaji watakaonekana kwenye video mpya ya msanii wa Kimataifa wa Tanzania, Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’ unatarajiwa kufanyika katika ukumbi wa Nyumbani Lounge, Kinondoni, Dar es Salaam.

Saturday, September 15, 2012

WADANGANYA NA KUJIPATIA FEDHA KWA JINA LA ASHA ROSE MIGIRO

Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Wakala wa kupakia na kupakua mizigo bandarini ya Mokha Agency Co. Ltd, Mohamed Lema akionesha Taarifa ya Polisi (RB) kwa waandishi wa habari Dar es Salaam leo waliyofungua katika Kituo cha Polisi cha Msimbazi baada ya watu waliofahamika kwa majina ya Yusuf Kalala na mke wake Sharifa Kalala kuitapeli kampuni hiyo kiasi cha fedha shilingi milioni 11.1 kwa kujipatia huduma kwa njia ya udanganyifu wakutumia jina la aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dk. Asha-Rose Migiro. Katikati ni Msemaji wa kampuni hiyo, Salim Dawa na mmoja wa wanafamilia hiyo, Amin Kulateni.

TAHADHARI DHIDI YA MVUA ZA OKTOBA 2012–DISEMBA, 2012


 Kufuatia Utabiri wa Hali ya Hewa uliofanywa kwa pamoja na Mamlaka za Hali ya Hewa kwa nchi za Pembe ya Afrika na Afrika Mashariki, Mamlaka ya Hali ya Hewa – Tanzania imetoa taarifa kuhusu uwezekano wa nchi kupata mvua nyingi iliyo juu ya wastani. Hali hii ya kuwa na mvua nyingi inatabiriwa kuikumba nchi kwa kipindi cha Oktoba, 2012 hadi Disemba, 2012 na huenda ikaendelea zaidi.

Hii ndio maana ya neno BADO NGWARE "G-NAKO"

Pichani: G-Nako & Nikki wa Pili
 
Msanii kutoka kundi la Weusi G-Nako ametiririka na Bongo Star Link na kusema maana ya neno BADO NGWARE ambapo jina hili amelitumia katika track zake mbili ile ya kwanza aliyomshirikisha Peter Msechu na hii rmx ambayo kamshirikisha Nikki wa Pili. 
G-Nako anasema maana ya neno hilo ni BADO MAPEMA na kama unataka kujua maneno yaliyosemwa humo ndani isikilize track hii ambayo ni remix

Friday, September 14, 2012

USAILI WA MAISHA PLUS 2012 UNAENDELEA MIKOANI

                          Hii ndiyo team nzima ya maisha plus inayofanya usaili mikoani kote Tanzania.

KILICHOIKUTA KAMATI ILIYOUNDWA KUCHUNGUZA KIFO CHA MWANDISHI IRINGA.

 
  
 
Ikiwa ni siku moja tu baada ya kufikishwa Mahakamani kwa askari polisi anaetuhumiwa kwa mauaji ya mwandishi wa habari Iringa Daudi Mwangosi,

DMX AMEMCHANA DRAKE TENA, HII NDIO STORI YENYEWE.

.
DMX kapanda on air tena na kumchana rapper Drake ambae siku kadhaa zilizopita alirekodi kolabo na sauti ya marehemu Aaliyah.

Thursday, September 13, 2012

Kiasi Kilichopatikana Hada Sasa Harambee Ya Mjane Wa Daud Mwangosi;

 

1. Chris Cremence                                     100,000
2. Anonymous                                             500,000
3. Maggid Mjengwa                                     100,000
4. Raymond Kasoyaga                                   20,000
5.Edward Mgogo                                            10,000
6.Joachim Kiula                                                5,000
7.Libory Muhanga     

Monday, September 10, 2012

KALAPINA AJA NA FILAMU YA TUKIO LA DR ULIMBOKA


Rapper aliyepotea kwenye ramani ya muziki wa Tanzania, Kalapina, yupo kwenye hatua za mwisho za kuanza kushoot filamu

USIKU WA MUONEKANO WA DHAHABU SERENGETI FIESTA MKOANI SINGIDA

           Cyril ni moja kati wasanii ambao walitoa burudani ya kutosha kabisa katika serengeti fiesta mkoani singida.

Sunday, September 9, 2012

TAARIFA KAMILI KUHUSU P SQUARE KUSHITAKIWA.

 Posted: 9th September 2012 by Yusha Shabani
P Suare na Akon.
Unakumbuka ile kolabo ya P Square na Akon inaitwa Chop my money ambayo ilimfanya May D kuwa staa zaidi baada ya kuongezwa kuwa mtu wa nne kusikika kwenye hiyo single?
kama hufahamu May D ni msanii wa Nigeria ambae alisainiwa kuwa chini ya lebo inayomilikiwa na P Square (Square Records) ambapo ni siku kadhaa zimepita toka lebo hiyo itangaze kwamba haimuhitaji tena na wala hayuko tena chini yao.
Leo mtandao wa Naijag umeripoti kwamba May D ambae alitimuliwa na lebo hiyo wiki kadhaa zilizopita yuko kwenye hatua za mwisho za mazungumzo na wanasheria wake ili awashitaki P Square kwa kuvunja mkataba kiholela.
May D anasema taarifa za kutimuliwa kwake alizipata kwenye blogs na magazeti kama walivyopata watu wengine na kwamba hakupewa taarifa zozote za kiofisi kama inavyopaswa, hiyo ndio sababu inayomfanya awashitaki P Square akiwemo kaka yao mkubwa Jude Okoye ambae ndio alitangaza kuuvunja mkataba wa May D.
.

Saturday, September 8, 2012

Harambee Ya Mjane Wa Daud Mwangosi; Waliochangia, Namna Ya Kuchangia Na Kiasi Kilichopatikana Hadi Sasa...


1. Chris Cremence                                     100,000
2. Anonymous                                             500,000
3. Maggid Mjengwa                                     100,000
4. Raymond Kasoyaga                                   20,000

FUNIKA BOVU LA FSERENGETI FIESTA JANA.

Mmoja wa wasanii mahiri katika miondoko ya hip hop hapa nchini,Mwana FA akiwaimbisha wakazi wa mji wa Tabora wimbo wake wa Yalaiti,usiku wa kuamkia

MAAMUZI YALIYOFIKIWA NA SERIKALI BAADA YA WAISLAM KUANDAMANA.

Posted: 8th September 2012 by yusha shabani
                  Maandamano yenyewe (picha kutoka hakingowi.com)

Zaidi ya waumini mia tatu wa dini ya kiislam jana september 7 waliandamana mpaka Wizara ya mambo ya ndani wakishinikiza jeshi la polisi kuwaachia baadhi ya viongozi wa kiislam waliokamatwa kwa kupinga zoezi la sensa.

Thursday, September 6, 2012

Video| Samale-Mzungu wa nne.(Official Video)

Video| RICO SINGLE-MADEMU WAZURI OFFICIAL VIDEO from ZANZIBAR TANZANIA

Saturday, September 1, 2012

MCHOMVU APATA SHAVU LA KUWA JUDGE KATIKA FANALI ZA NOKIA

Adam mchomvu
Among of hottest show in town double XXL kutoka The people station clouds fm namzungumzia Baba john au Adamu mchomvu amepata shavu la kuwa the judge katika mashindano ya nokia don’t break the beat ambayo

FUNIKA BOVU MUSOMA SERENGETI FIESTA 2012

Msanii wa muziki wa Hip Hop Bongo, Roma Mkatoriki, akiwajibika mbele ya mashabiki wake, kwenye jukwaa la Serengeti Fiesta 2012, ndani ya Viwanja vya Karume mjini Musoma usiku wa kuamkia leo.

ALICHOKISEMA MARLAW KUHUSU HIKI KILICHOANDIKWA NA GAZETI KWAMBA AMESHINDWA KUZAA.

Posted: 1st September 2012 by Yusha.

AY ndani ya Categories 3 kwenye tuzo za CHANNEL O (CHOMVA12)

AY msanii kutoka TANZANIA ameingia kwenye tuzo za Channel O Music Video Award 2012 akiwa kwenye sehemu 3, sehemu hizo ni pamoja na
Most Gifted Video of the Year

Most Gifted East African video of the Year

Most gifted male video of the year