Blogger Widgets

Celebrity Story from Different Place

Entertainment story of Bongo land and their work.

Story za wakali wa majuu

Burudani| Video| Tracks na Maisha yao.

Bongo Movie na wasanii wake kwenye maisha yao

News Movie| New Story| New Skendo.

Mafanikio

Story za walio vuka boda na mafanikio yao kama wajasiria-mali.

Elimika na Burudika

Life ya wasio na skendo na wenye skendo| Mafanikio yao na vioo wa jamii.

Wednesday, January 22, 2014

MUONEKANO MPYA WA MREMBO WEMA SEPETU

Pichani juu ni taswira za Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu alizotupia katika ukurasa wake wa Instagram ambapo mojawapo aliandika hivi "For my baby... yes you...". Mrembo huyu kwa sasa yupo na aliyekuwa mpenzi wake wa zamani Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz'.

Thursday, January 16, 2014

Walichoandika Adam Mchomvu na Diva Loveness kwenye instagram.

Jana kitu kilichokua headline kubwa kwenye mtandao ni kuhusu Adam Mchomvu, Diva na B12.
Leo asubuhi hizi ndio status walizoandika Adam Mchomvu na Diva kwenye kurasa zao za instagram.
http://millardayo.com/wp-content/uploads/2014/01/diva.jpghttp://millardayo.com/wp-content/uploads/2014/01/diva2.jpghttp://millardayo.com/wp-content/uploads/2014/01/babajonii.jpg
adam

http://millardayo.com/wp-content/uploads/2014/01/babajonii2.jpg

ANGALIA PICHA ZA WAKE ZA WATU, MAKAHABA WANGONOKA NA MADEREVA KWENYE MALORI....HALI INATISHA SANA....!

KILE kikosi maarufu kilichojizolea sifa kwa utenda kazi wake cha Operesheni Fichua Maovu (OFM) kilicho ndani ya jumba la Magazeti Pendwa Tanzania, Global Publishers jijini Dar kinazidi kufichua uovu, twende pamoja ili kujua.Mwishoni  mwa wiki iliyopita, OFM ilitua ‘Mji Kasoro Bahari’ (Morogoro) ambapo kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Morogoro, kazi kubwa ilifanyika.

KAZI YENYEWE
Kazi ilikuwa kuyafumua madanguro na maeneo ya kujiuzia makahaba ambapo kwa mujibu wa watoa habari, baadhi ya maeneo mjini humo (hatuyataji kwa sasa) yamekubuhu kwa biashara ya wanawake kuuza miili yao.SOMA ZAIDI

MAENEO YALIYOFIKIWA NA OFM
OFM na jeshi la polisi walijipanga sawa kwa ushirikiano huku wakitumia  mbinu za hali ya juu ili kuwanasa machangu hao.

Itigi Msamvu ni kambi maarufu ya machangudoa hao ambapo wateja wao wakubwa ni baadhi ya madereva wa magari makubwa ‘malori’ wanaoegesha magari yao eneo hilo lililopo kandokando ya Barabara Kuu ya Morogoro -Dar es Salaam.
ILIKUWAJE?
Awali, wakazi wa eneo hilo walilalamikia uchafuzi wa mazingira na hatari kwa watoto wao kupata magonjwa ya ajabu kutokana na utupwaji hovyo wa kondom zilizotumika unaofanywa na machangu hao ambapo watoto hao huziokota na kuzigeuza maputo.

Wakazi hao walisema kuwa wamesharipoti hali hiyo kwa jeshi la polisi lakini kulionekana kusuasua.
Mbali na athari za mwanzo, wakazi hao waliwaambia OFM kuwa, kumekuwa na tabia ya ukabaji na unyang’anyi kwa watu ambao wanakatisha katika vichochoro vya eneo hilo.

MSIKIE HUYU
“Jamani OFM tunaomba msaada wenu kwani hapa Msamvu ni jehanam, maasi yote yanafanyika hapa, ngono mpaka kwenye uvungu wa magari makubwa ambayo yamepaki, watu wanakabwa, kondom zilizotumika zimezagaa hovyo,” alisema mkazi mmoja aliyesema anaitwa Mkude.

OFM NA JESHI LA POLISI
Baada ya kupokea malalamiko hayo, OFM waliwasiliana na jeshi la polisi mkoani hapo ambapo  walisema wapo katika kujipanga kuingiza operesheni ya kufungua mwaka 2014.

”Ni kweli kabisa wakazi wa hapo wanapalalamikia sana pale mahali lakini tumeshajipanga, hata RPC nadhani alishawaambia nyie (OFM) mje mshuhudie kazi. Tena kama mnaweza, leo si Alhamisi (Januari 9, 2014) kesho Ijumaa njooni tuingie kazini, sisi hatuna siasa,” alisema afisa mmoja wa polisi.

SIKU YA TUKIO
Siku ya tukio ambayo ilikuwa usiku wa saa tano, Ijumaa iliyopita, Kaimu Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya ya Morogoro, Jamal Ibrahim na  msaidizi wake wa karibu, Tausi Mbalamwezi huku OFM wakiwa kwa ukaribu nao, walipafungia kazi mahali hapo.

Oparesheni ilifanyika na kufichua maovu mengi, madada poa kibao walidakwa wakiwa na watu waliojitambulisha kuwa ni madereva wa malori.

Katika sakata hilo, baadhi ya madereva ambao ndiyo wateja waliingia mitini, wengine kujifungia kwenye magari yao na kuwaacha machangudoa hao wakiwa hawana pa kukimbilia na hivyo kunaswa kama ndege kwenye mtego wa mti wenye ulimbo.
Baadhi ya makahaba walikiri kuliwa uroda na madereva, wakasema ni wateja wao wa siku nyingi na ndipo wanapoponea wao.

“Jamani tunatubu lakini hao madereva ndiyo wateja wetu wakubwa. Wakija kama hivi kutoka Dar wanakuwaga na hela sana,” alisema changudoa mmoja bila kujitaja jina.
HA! HATA WAKE ZA WATU!
Katika hali ambayo haikutarajiwa, makahaba wawili walidai wao wameolewa lakini waume zao wapo nje ya mji kikazi ndiyo maana waliamua kujiuza ili kupata ‘chochote’.

UTETEZI WA MADEREVA
Baadhi ya madereva waliozungumza na paparazi wetu walikiri kuwa kuna madereva wenye tabia hiyo ya kuwanunua machangudoa lakini si wote.

“Jamani kwanza tuwekane sawa, si madereva wote wana tabia ya kununua machangu, sisi wengine tunajiheshimu sana, hatuwezi,” alisema dereva mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Mafongo baada ya kukutwa pembeni ya lori.

OFM IKAINGIA GESTI
Baada ya polisi kuwasomba makahaba hao wa kwenye malori, OFM na polisi wakaenda kuvamia gesti moja inayojulikana kwa jina la Itigi ambapo, katika hali ya kushangaza, wanawake wawili, mmoja bonge,  walinaswa ndani ya chumba kimoja, kitanda kimoja.

Hawakuwa na la kujitetea lakini pembeni ya kitanda hicho palikuwa na kondom kibao. Watoa habari walisema kuwa, wanawake hao wamekuwa wakilala humo kwa ajili ya kusaka wateja ambao huwaingiza ndani ya chumba hicho ‘kuwahudumia’.



Wanawake hao waliunganishwa na wenzao kwenye gari na kupelekwa kituo kikuu cha polisi cha mjini Morogoro

Monday, January 13, 2014

ETI HUU NDIO MWISHO WA DUNIA WATAJWA

Stori: Mwandishi Wetu na Mitandao
WAKATI binadamu wakiendelea na mipango yao ya kuifanya dunia kuwa sehemu salama ya kuishi kimazingira, kiulinzi na usalama, utabiri mpya wa kutisha unaonesha kuwa mwaka 2032 ndiyo mwisho wa sayari hii ya tatu katika mfumo wa jua.
Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali katika mitandao ya internet, sayari iitwayo Nibiru, ambayo kisayansi inafahamika kama Planet X ipo njiani kuigonga dunia na hivyo kusababisha majanga mbalimbali kutokea.

ITAONEKANA ANGANI KAMA MWEZI
Kwa mujibu wa mitandao hiyo ya kisayansi, sayari hiyo ambayo inaisogelea dunia kwa kasi kubwa, itaonekana kubwa na angavu wakati wa usiku angani na kuwa katika umbo la mwezi na hivyo kufanya miezi ionekane miwili.

DALILI KWAMBA IPO JIRANI
Taarifa zaidi za kisayansi zinasema kuwa, kadiri sayari hiyo inavyozidi kusogea, dunia itaanza kutikisika na kusababisha matetemeko ya ardhi kuongezeka sehemu mbalimbali.
Mbali na dunia kutikisika na matetemeko, milipuko ya volcano nayo itatokea huku idadi kubwa ya milipuko hiyo mipya ikiongezeka, vimbunga vikubwa kama Tsunami vitaibuka na mwishowe dunia itapigwa na bomu la miamba midogo na vimondo kutokea angani.

DUNIA ITAKUMBWA NA GIZA NENE
Wakati volcano zote duniani zitakapoanza kulipuka na zingine mpya kujitokeza, dunia itafunikwa na giza nene  na matope kwa wakati wote wa usiku na mchana huku watu wakitakiwa kusoma katika Biblia Joel 2: 1-2 na Zephaniah 1:14-17.

NI TUKIO LA AINA YAKE KARNE YA 21
Nibiru inatajwa kama kitu kinachoisogelea dunia kinachoaminiwa kusababisha madhara makubwa ambapo kama hakitaigonga dunia, kitasababisha mtikisiko usio wa kawaida kitakapopishana nayo. Baadhi ya wanasayansi wanaamini kuwa kitendo hicho kitatokea mapema katika karne ya 21 (tuliyonayo sasa).

WANASAYANSI WAPINGANA
Baadhi ya wanasayansi wanapinga kwa maelezo kwamba hakuna ushahidi wowote wa kitafiti unaoonesha wazi kwa mabingwa wa anga za juu waliobobea wa masuala ya nyota.

MWANAMKE ALIWAHI KUOTA NDOTO
Kwa mara ya kwanza jambo hilo lilitokea mwaka 1995, wakati mwanamama Nancy Lieder muasisi wa mtandao wa ZetaTalk, aliwahi kudai kuoteshwa ndoto kwamba, Mei 2003 kuna kitu kitaingilia mfumo wa jua (solar system) na kusababisha dunia kutoboka tundu litakalosambaratisha sehemu kubwa ya kizazi cha binadamu.
Lieder aliifafanua kuwa, kitu hicho kitakuwa na ukubwa wa mara nne ya dunia.

BAADA YA NDOTO
Baada ya mwanamama Lieder, mtu wa kwanza kuizungumzia Nibiru alikuwa Mark Hazlewood, mwanachama wa zamani wa mtandao wa ZetaTalk ambaye mwaka 2001 alichapisha kitabu kilichoitwa Blindsided na kusema kuwa mwisho wa dunia ungekuwa mwaka 2003 baada ya kuwasili kwa sayari ya kumi (Nibiru).
Katika mfumo wa sasa, baadhi ya wanasayansi wanasema sayari ziko 12, wakizitaja kwa namba 1. Jua 2. Mercury 3. Venus 4. Dunia 5. Luna (mwezi) 6. Mars 7. Jupiter 8. Saturn 9. Uranus 10. Neptune 11. Pluto 12. Nibiru.

IMANI NYINGINE YASEMA MWISHO WA DUNIA NI FEBRUARI 22, 2014
Hata hivyo, utabiri mpya uliotolewa na watu wa jamii ya Vikings jijini New York, Marekani umesema mwisho wa dunia ni Februari 22, mwaka huu.
Mitandao mbalimbali pamoja na gazeti maarufu la Daily Mail la Uingereza lilielezea utabiri huo uliofanywa na jamii hiyo ukidai kuwa mwisho wa dunia utatokana na Mungu Odin kupigana na kuuawa na shetani Wolf Fenrir, hivyo kuiachia dunia anayoishikilia.
Wamesema baada ya kuiachia dunia itafurika maji ambayo yatakuwa na sumu, hivyo viumbe wote watateketea.

WATUMISHI WA MUNGU TANZANIA
Baadhi ya watumishi wa Mungu nchini wamekuwa wakisimamia andiko la kwenye Biblia linalosema kuwa, hakuna mwanadamu anayeijua siku wala tarehe ya mwisho wa dunia na ni siri ya Muumba.
Makanisa mengi nchini Tanzania yana sera tofauti lakini yanaongozwa na Biblia moja. Makanisa hayo ni Romani Katoliki, Lutheran (KKKT), Anglikana na makanisa ya kiroho kama Full Gospel& Bible Fellowship la Zakaria Kakobe.

FREEMASON WABARIKI
Jamii ya Freemason tayari imebariki mwisho wa dunia kwamba umefika na dunia inatarajie tukio kubwa la pamoja.
Mitandao ya jamii hiyo inataja kama hizi ni nyakati za mavuno kwa maana kwamba, upande wa Mungu na shetani kushindania watu huku waendao upotevuni  wakiwa wengi.

MFUMO WA DUNIA TANGU KUUMBWA
Kwa mujibu wa kitabu kinachoitwa Panorama ya Biblia, ulimwengu tangu kuumbwa kwake umekuwa na matukio makubwa kila baada ya miaka 2000 (inaweza isitimie au ikapita kidogo).
Tangu kuumbwa kwa Adamu na Eva mpaka gharika inadaiwa ni miaka 2000. Gharika hadi dunia kubadili mfumo wa mawasiliano (Mnara wa Babeli) ni miaka 2000. Kuzaliwa kwa Yesu hadi saa ni miaka 2000 ambapo katika karne hii, dunia huenda ikaingia katika tukio kubwa sana ambalo halijawahi kutokea.

Wednesday, January 8, 2014

HIZI HAPA NDIO GHARAMA ZA VIDEO YA- My Number One Rimix YA DIAMOND PLATNUMZ


Naseeb Abdul “Diamond” ameweka kuhusu gharama za video yake ya Number One Remix aliyofanya na director Clarence Peters wa Nigieria.

Diamond anasema gharama hii hazijumuishi usafiri wala accommodation walivyokua huko Nigeria.

Diamond amelipa dola 25,000 sawa na Tsh millioni 40 za kitanzania kufanya production ya hii video ambapo ilijumuisha gharama za kila kitu hadi models na dancers.