Blogger Widgets

Celebrity Story from Different Place

Entertainment story of Bongo land and their work.

Story za wakali wa majuu

Burudani| Video| Tracks na Maisha yao.

Bongo Movie na wasanii wake kwenye maisha yao

News Movie| New Story| New Skendo.

Mafanikio

Story za walio vuka boda na mafanikio yao kama wajasiria-mali.

Elimika na Burudika

Life ya wasio na skendo na wenye skendo| Mafanikio yao na vioo wa jamii.

Thursday, April 18, 2013

MSIBA WA BILIONEA BABU SAMBEKE WAZUA GUMZO,,,,VIGOGO WATAWALA MSIBANI .... TUKIO KAMILI LA MAZISHI LIPO HAPA

DSCF8833

Jamal Sambeke mtoto wa marehemu akifunga jeneza la baba yake mara baada ya watu mbalimbali kutoa heshima zao za mwisho nyumbani kwake njiro Themi Mkoani Arusha
DSCF8840
Waombolezaji wakibeba jeneza la Bilionea Babu na kuweka kwenye gari maalumu tayari kwa safari kuelekea Moshi kwa mazishiDSCF8828
Watu wakitoa heshima za mwisho
DSCF8844
Watoto wa marehemu Sia na Getrude waliovalia nguo nyeupe
DSCF8834
Jamal akifunga jeneza la marehemu Babu Sambeke
DSCF8830
Jaji Aisha nyerere msibani pamoja na mkurugenzi wa kibo palace Vicent Laswai
DSCF8832 DSCF8848
Baadhi ya magari ya kifahari yaliyofika katika msiba huo
DSCF8838
Mkurugenzi wa hoteli ya Kibo Palace Vicent Laswai akizungumza msibani mara baada ya watu mbalimbali kutoa heshima zao za mwisho

DSCF8847
Waombolezaji
Mamia ya vigogo pamoja na watu mbalimbali wafurika nyumbabi kwa marehemu Bilionea “Babu Sambeke”Ernest Sambeke eneo la njiro jijini Arusha kuaga mwili wake unaotarajiwa kuzikwa kesho nyumbani kwake eneo la Karanga mjini Moshi huku msiba huo ukiwa tofauti na misiba mingine iliyozoekeaka hapa Nchini
Marehemu,Sambeke alifariki hivi karibuni katika ajali ya ndege aliyokuwa akiiendesha na pia mmiliki wa ndege hiyo ambapo ilianguka katika eneo la Kisongo na kusababisha kifo chake Mkoani Arusha
Shughuli za kuaga mwili wa marehu zilikamilika majira ya saa 8:45 mchana huku mwili huo ukipakiwa katika gari maalumu la kifahari tayari kusafirishwa kuelekea nyumbani kwake Moshi kwaaajili ya mazishi
Taratibu za kuaga mwili wa marehemu zilianza majira ya saa 5 asubuhi huku wafanyabiashara wa madini pamoja wafanyabiashara wengine kutoka hapa Arusha na Moshi walionekana kutawala msiba huo.
Katika zoezi hilo la kuaga mwili wa mareheu Padri Florentine Mallya ambaye ni mdogo wa marehemu aliongoza misa ya kumuombea marehemu na baada ya kumaliza alitoa fursa kwa watu mbalimbali kupita mbele ya jeneza kwaajili ya kuaga mwili Ndani ya jeneza marehemu alivalishwa nguo zake za kirubani huku ,baadhi ya wanajeshi kutoka jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) walionekana jana katika zoezi la kuuaga mwili wa marehemu ambapo baadhi yao walikuwa wamevalia sare za jeshi hilo
Hatahivyo,baadhi ya watu walionekana katika hali ya kawaida huku watoto wakionekana na nyuso za huzuni mda wote
Tofauti na misiba mingine nchini watu mbalimbali walipata fursa ya kupata chakula na vinywaji mbalimbali kwa kujihudumia vikiwemo vinywaji aina ya Bavaria ambapo watu waliohudhuria zoezi hilo walionekana wakijihudumia zaidi vinywaji vya bavaria
Magari ya kifahari yalionekana kutawala msiba huo huku barabara ya njiro ikionekana kuwa na msongamano kubwa iliyosababishwa na zoezi hilo la uwagaji wa mwili
Marehemu aliacha watoto watatu ambao ni Sia,Jamal,Getruda

JAMII BLOG

Wednesday, April 17, 2013

DIVA LOVENESS LOVE amtumia ujumbe huu mfupi wa maneno WEMA SEPETU. UJUMBE WENYEWE HUU HAPA

Kupitia account yake ya Instagram mwanadada Diva Loveness Love anayetangaza Clouds FM kwenye kipindi cha usiku Ala za Roho, inasemekana kuna mtu amefungua account ya facebook kwa jina hilo la diva na kuanza kumporomoshea mvua ya matusi mwanadada Wema Sepetu.

Angalia Picha mbalimbali za Maandalizi ya Mazishi ya Marehemu Bi Kidude.


Gari lililokuwa limeubeba mwili wa msanii mkongwe wa muziki wa tarab, marehemu Fatuma Binti Baraka 'Bi. Kidude', likiusafirisha kutoka katika Kijiji cha Kihinani na kuupeleka nyumbani kwake Rahaleo kwa matayarisho ya mazishi yatayofanyika kesho mchana katika Kijiji cha Kitumba, Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja. (Picha zote kwa hisani ya Othman Maulid wa ZanZinews)
Mwili wa marehemu ukishushwa katika gari wakat ukiwasili nyumbani kwake, Rahaleo kwa taratibu za mazishi yatakayofanyika kesho mchana na Kijiji cha Kitumba, Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja.
Ndugu, Jamaa na marafiki, wakiubeba mwili wa marehemu Bi. Kidude wakati ulipowasili nyumbani kwake, Rahaleo kwa ajili ya matayarisho ya mazishi yatakayofanyika kesho Kijiji cha Kitumba, Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja.
Mrajisi wa Baraza la Sanaa la Zanzibar, Khadija Batashi, akizungumza na waandishi wa habari jinsi alivyoupokea msiba wa msanii mkongwe wa muziki wa taraba nchini, Bi Kidude.
Matayarishi ya mazishi ya msanii wa muziki wa tarab, Bi. Kidude yakiendelea nyumbani kwake Rahaleo, mjini Zanzibar.
Mjukuu wa Bi. Kidude Omar Ameir, akiwasiliana na jamaa kwa ajili ya kuwajulisha msiba wa marehemu Bi. Kidude, baada ya mwili wa marehemu huyo, kuwasili nyumba kwake kwa ajilimatayarisho ya mazishi yatakayofanyika kesho mchana baada ya Swala ya Adhuhuri, ambapo atazikwa Kitumba.
Bi. Maryam Hamdani akilakiwa na Bi. Sihaba wakati akiwasili nyumbani kwa marehemu Bi. Kidude Rahaleo, mjini Zanzibar akiwa na majonzi.  
Waandishi wa habari wakizungumza na Mfadhili Mkubwa wa Bi. Kidude, Maryam Hamdan, kuhusiana na marehemu ambaye yeye alikuwa ni mtayarishaji na mratibu wa safari za Bi. Kidude nje ya nchi na katika matamasha mbalimbali aliyokuwa akihudhuria nje ya nchi wakati wa uhai wake.

HII NDO SABABU YA KIFO CHA BI KIDUDE, SOMA NA SIKILIZA ALICHOKISEMA MJUKUU WAKE

Mjukuu wake aitwaye Omar ameiambia Bongo5 kwa simu muda mfupi uliopita kuwa Bi. Kidude alikuwa amelazwa kwa muda mrefu kutokana na kusumbuliwa na maradhi ya sukari na uvimbe kwenye kongosho. “Kwa ufupi alilazwa kipindi kirefu na baadaye akatolewa, lakini baadaye akaja kuendelea kuumwa tena tukampeleka hospitali tukawa tunampeleka kwenda na kurudi hapa juzi akaanza kuzidiwa tena tukampeleka hospitali moja inaitwa Keeni (???) Kwaajili ya matibabu zaidi na drip na vitu vingine lakini baadaye baada ya siku ya tatu mwenyezi Mungu akachukua roho yake,” amesema Omar.

HIVI NDIVYO MAUTI YALIVYOMKUTA BI. KIDUDE


Taarifa zilizotufikia muda huu zinasema msanii mkongwe na mahiri katika fani ya muziki wa mwambao Fatuma binti Baraka almaarufu kama Bi Kidude amefariki dunia muda mfupi uliopita.

Taarifa zilizothibitishwa na mwandishi wa habari wa ITV Farouk Karim zinasema kuwa Bi Kidude amefariki nyumbani kwake Bubu Zanzibar.
Bi Kidude aliwahi kusema hafahamu tarehe halisi aliyozaliwa, isipokuwa anachojua ni kwamba alizaliwa wakati rupia ikitumika kama fedha, na vilevile ana hakika ni kabla ya Vita Kuu ya Kwanza ya Ulaya, ila inaaminika alikuwa na zaidi ya miaka 90.

Mungu ailaze mahala pema roho ya marehemu Bi Kidude, Amen

Tuesday, April 16, 2013

Style za Kanga moja laki si pesa ni kama filamu za wakubwa..ni ‘HATARI’ usiende na mtoto au mtu unaeheshimiana nae, maana duh!




Moja kati ya makundi yanayovuma sana kwa kuwapagawisha mashabiki wakiwa jukwaani ni kundi la ‘kanga moja laki si pesa’. Kundi hilo limejipatia umaarufu mkubwa sana na hivyo kupiga matamasha wakizunguka Tanzania na kila walikopita wameacha historia ya aina yake.

Lakini Kile wanachokifanya wakiwa jukwaani hakihitaji mwalimu wa nidhamu kuwa karibu nao ama jopo la kuhifadhi maadili ya taifa kushuhudia kwa sababu endapo wakishuhudia inaweza kuzua ‘msalaaa’ si kidogo. Na tukisema ingekuwa enzi za mwalimu, dah, sijui ingekuwaje.....!
 
Style wanazocheza wakiwa jukwaani naweza kuthubutu kusema ni kama movie za wakubwa kwa asilimia kadhaa, na kwa ushauri wa haraka na muhimu ni kwamba watoto ama watu wanaoheshimiana na kuoneana aibu hawashauriwi kabisaa kushuhudia pamoja shangwe hizo za Kanga Moko laki si pesa, ikiwa hivyo mnaweza kupoteana ukumbini kukwepa aibu wakati watu ndo wanazidi kushangilia.

Ipo mitindo mingi ya kushtua wanayoicheza, lakini kati ya hiyo huu wa kumwagiwa kilevi sehemu za faragha kisha kuchezesha maungo yaliyolowana na kuonekana mithili ya karatasi iliyomwagiwa mafuta ya taa na kilaza ili aitumie kuchora kwa urahisi ramani iliyowekwa chini ya karatasi hiyo kwa kufuatisha tu, imetisha!! Hapa naweka kalamu chini nisigusie sana sentensi  hii‘Maadili ya Kitanzania yako wapi?’

Jionee mwenyewe baadhi ya picha za ‘kanga moko’ zilizochukuliwa huko Bukoba wakiwa wanamsindikiza Diamond Platinumz kuwapa shangwe wakazi wa Bukoba, show iliyoweka historia ya aina yake mjini humo.








Wataalam wa mambo wanakwambia 'DON'T TRY THIS AT HOME'.

Kumbe Wimbo mpya wa Diamond ‘Mapenzi basi’ umevuja! Awalaumu AM Records kwa kuvujisha nyimbo zake makusudi, anaweza asifanye nao kazi tena.

                           
Diamond platinumz kila akitoa wimbo hushika attention ya watu wengi na kuwa hit, lakini kumekuwa na mfululizo wa kesi za nyimbo zake kuvuja ikiwa ni pamoja na wimbo wake wa ‘Ukimwona’ na video ya wimbo wake ‘Kesho’.

theHOODinfotainmentimemtafuta Diamond Platinumz ambae alifunguka kuwa wimbo huo ulivuja. Aliwalaumu sana AM Records na kwa kile alichodai kuwa wanajua ni kwanini wao wameamua kuvuja wimbo huo japo wanakwepakwepa.

“AM record wenyewe sijui wanachonitafuta ni nini nikirekodi nyimbo kwao wanakuwa wanazivujisha yani makusudi. ” Alifunguka Diamond. Alisisitiza kuwa anajua AM Records ndio wako responsible kwa zoezi la kuvujisha nyimbo zake, “yani ni wao mi najua kabisa ni wao, wanaongea ila wanakuwa kama wanakwepakwepa ila mi najua kabisa ni wao.”

Huu sio wimbo wa kwanza kwa Diamond platinumz kuwa na matatizo kutoka AM Records, ‘Ukimwona’ pia ni wimbo ambao ulivuja na ulipikwa na AM Records, lakini Nataka kulewa iliyozua gumzo pia ilifanyika katika studio hiyo hiyo chini ya producer Maneck.

‘Kesho hit maker’ amesema baada ya wimbo wake ‘Ukimwona’ kupigwa sana japo hakuitoa officially na imeshahit basi ameamua kuacha ipigwe tu wakati anaangalia ngoma yake nyingine ya kuachia.
 
  theHOODinfotainment inaendelea kufanya jitihada za kumtafuta Manecky wa AM Records ili kujua kwa upande wake nini kinatokea hadi nyimbo za Diamond zinavuja kutoka katika studio hiyo.
 
chanzo: kwa msaada wa leotainment

Jokate na Penny wazungumzia tetesi za uhusiano kati ya Diamond na Irene Uwoya

Katika muda ambao kila mmoja alikuwa amejaribu kuamini kuwa Diamond Platnumz ameamua kutulia na mpenzi mmoja, mtangazaji wa DTV, Penniel Mungilwa, hivi karibuni kumezuka tetesi kuwa staa huyo wa ‘Ukimuona’, ameanzisha uhusiano wa kimapenzi na muigizaji wa filamu Irene Uwoya.
page
Baadhi ya magazeti ya udaku nchini yameandika habari hiyo ikiwa na picha inazowaoenesha mastaa hao wakichukua chumba kwenye hoteli ambako yalidai walienda kufanya yao.
DIAMOND3
Kufuatia tetesi hizo, Bongo5 imezungumza na mpenzi wa sasa wa Diamond, Penny ambaye amesema kwa ufupi kuwa wameshayazungumza na Diamond na wako vizuri kwa sasa lakini akasisitiza kuwa asingependa kuliongelea zaidi suala hilo.
Katia hatua nyingine, Jokate Mwegelo aliyewahi kuwa na uhusiano na Diamond amekanusha kupitia Bongo5 taarifa iliyoandikwa na gazeti moja la udaku kuwa amemcheka Irene kwa kunaswa kwenye himaya ya Diamond.
JOKATE
“Mimi hivyo vitu havinihusu na wanapenda kupata quotes zangu pasipo hitajika. I don’t know why? I don’t why wanatafuta story. That’s their life kiukweli with whatever they choose to do, more power to them,” amesema Jokate.

chanzo:  bongo5

Wajanja wajaribu kumtapeli Bob Junior

Imebainika kuwa kuna mtu aliyetengeneza line mpya kwa kutumia namba ya Bob Junior aliye barani Ulaya kwa sasa na kutaka kuwatapeli watu wake wa karibu kuwa hitmaker huyo wa Nichum yupo hoi na anahitaji msaada haraka.
72910_10151418615904962_719201817_n
Taarifa hiyo imetolewa na baba yake mdogo, Guru Ramadhan ambaye ni mmiliki wa G Records. Kupitia Facebook, Guru aka G Lover ameandika:
“Hii sijaipenda kabisa ni too much sasa..eti mtu yupo Europe na simu yake inaita bongo ukipiga duh kumbe mtu katengeneza line mpya na kutumia namba ya Bob Junior na pia jamaa anayetumia hiyo line ya simu eti anaomba msaada kwa watu kuwa Bob Junior anaumwa sana Ulaya anahitaji msaada wako ili arudi Bongo.
Hivi nini maana ya kusajili namba?…makampuni ya simu ya Bongo mjipange sanaaa…hili limemkuta msanii Bob Junior siku chache hizi, mpaka imeripotiwa polisi eti ndio wamejidai kui block number…t.g. mmeniboaje?..so guyz mnaosafiri muwe makini sana mkisafiri maana mnaweza kukuta madeni kibao mkafa na presha bure…wizi mtupu…I hate dat.”

Monday, April 15, 2013

MAGAZETI YA LEO APRIL 16 2013 KURASA ZA MWANZO NA MWISHO ZENYE STORI NZITO

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.