Blogger Widgets

Friday, December 13, 2013

LOWASSA ANUSURIKA KIFO AJALI YA NDEGE

 
Waziri Mkuu mstaafu na mbunge wa Monduli, Mhe. Edward Lowassa.
ABIRIA kadhaa akiwemo Waziri Mkuu mstaafu na mbunge wa Monduli, Mhe. Edward Lowassa wamenusurika kifo, baada ya ndege waliyokuwa wakisafiria kupasuka matairi yote manne ya nyuma wakati ilipokuwa ikitua katika uwanja wa ndege wa Arusha mchana mchana huu.
Ndege hiyo ya shirika la ndege la Precision aina ya ATR ilipata ajali hiyo wakati ikitua. Matairi yote manne ya nyuma yamepasuka na kusababisha taharuki kubwa kwa abiria.
"Yaani Mungu ni mkubwa kwa kweli, ametunusuru maisha yetu na kiongozi kipenzi chetu Lowassa...Mungu atamlinda jamani...siamini" alisikika akisema mama mmoja miongoni mwa abiria hao…
Waziri Mkuu mstaafu na mbunge wa Monduli, Mhe. Edward Lowassa.
ABIRIA kadhaa akiwemo Waziri Mkuu mstaafu na mbunge wa Monduli, Mhe. Edward Lowassa wamenusurika kifo, baada ya ndege waliyokuwa wakisafiria kupasuka matairi yote manne ya nyuma wakati ilipokuwa ikitua katika uwanja wa ndege wa Arusha mchana mchana huu.
Ndege hiyo ya shirika la ndege la Precision aina ya ATR ilipata ajali hiyo wakati ikitua. Matairi yote manne ya nyuma yamepasuka na kusababisha taharuki kubwa kwa abiria.
"Yaani Mungu ni mkubwa kwa kweli, ametunusuru maisha yetu na kiongozi kipenzi chetu Lowassa...Mungu atamlinda jamani...siamini" alisikika akisema mama mmoja miongoni mwa abiria hao wakati akishuka.
Lowassa ni miongoni mwa wana CCM wanaotajwa kuwania urais 2015 na amekuwa na nguvu kubwa katika harakati hizo.

0 comments:

Post a Comment