Blogger Widgets

Saturday, March 22, 2014

UNAJUA NI KWANINI MSANII TINO ANALIA NA SHERIA YA USHOGA HAPA TANZANIA? ZAIDI SOMA HAPA

clip_image001
MCHEZA sinema za kibongo Hisani Msuya "Tino" ameitaka Tanzania nayo kupiga marufuku suala la jinsia moja 'Ushoga' kama ilivyofanya nchi ya Uganda baada ya hivi karibuni rais wao Yoweri Museveni kusaini sheria hiyo ambayo mtu yeyote atakayepatikana na kosa hilo kuwa anafungwa maisha.

Akizungumza na tovuti hii, Tino alisema kuwa yeye ni miongoni mwa wanaharakati wanaopinga mapenzi ya jinsia moja nchini na ndiyo maana aliamua kutunga filamu yake inayozungumzia suala la kupinga kitendo hicho ambacho ni kinyume na maagizo ya Mungu.


"Naitaka Tanzania nayo kutunga sheria kama ya uganda ili tukomeshe suala hili kwani likiendelea kulelewa miaka ijayo taifa litakuwa na kizazi kilichopotoka na kutuingiza kwenye vita kali na Mungu ambaye aliwahi kuteketeza Sodoma na Gomola kwa makosa kama haya" alisema Tino


credit to swahili

0 comments:

Post a Comment