Blogger Widgets

Friday, September 14, 2012

DMX AMEMCHANA DRAKE TENA, HII NDIO STORI YENYEWE.

.
DMX kapanda on air tena na kumchana rapper Drake ambae siku kadhaa zilizopita alirekodi kolabo na sauti ya marehemu Aaliyah.

Kwenye interview na Power 105, Dmx amesema msimamo wake bado uko palepale kwamba sio shabiki wa Drake, alipoulizwa kuhusu album mpya ya Aaliyah ambayo Drake ni producer mkuu, DMX ameshtuka na kusema hiyo ni kumkosea Aliyah heshima, kama wamemdharau na hakubaliana na hiyo ishu.
Imempa hasira DMX na kusema anatamani wakati huu ungekua miaka 7 iiyopita, unakutana na mtu kwenye lift unampiga alafu unasepa, Drake hawezi kuendelea kuachiwa kufanya mambo ya kipuuzi kama hayo.
Baada ya hiyo kauli, mtangazaji alimwambia Dmx kwamba ni ngumu kumkuta Drake anatembea bila walinzi hivyo hatoweza kupata nafasi ya kumpiga, Dmx akajibu “hata mimi natembea na washkaji zangu pia”

0 comments:

Post a Comment