Friday, August 31, 2012
'Campus Divas For Rich Men’ kundi la Facebook wanapouzwa wanachuo wa Kenya
7:58 AM
No comments
![]() |
Jane 18 has just finished high school and will be
joining UoN she wants a rich dude who is willing to pay her half % school fees
|
“Sisi madiva tuna gharama, NYWELE, zinataka dawa!
MASIKIO yanataka,hereni!! MACHO yanataka wanja na shadow! PUA inatka kipini!
MDOMO, unatka lipstic! USO unataka poda na foundation! SHINGO inataka cheni! MATITI
yanataka sidiria! MIKONO inataka Bangali! VIDOLE vinataka, Pete! KIUNO kinataka
shanga. MA***KO yanataka chupi MIGUU inataka hina rangi na viatu. KAMA HUNA
MKWANJA POLEEEEEEE,” ni baadhi ya status zinazosomeka kwenye ukurasa uitwao 'Campus Divas For Rich Men’.
Ni ukurasa maarufu sana kwenye Facebook sasa hivi nchini Kenya, ukiwa
na likes 34,339.
Ukurasa huu huonesha picha za wasichana ‘wanaodaiwa kuwa ni
wanachuo’ wakijiuza na kutafuta wanaume wenye fedha ili wawatimizie haja zao.
Hata hivyo kwa uchunguzi uliofanywa na gazeti la Daily Post,
umegundua mtu aliyeufungua ukurasa huo ambao kiukweli picha na majina
anayoyaweka sio vya kweli.
![]() |
Huyu ndiye aliyeanzisha ukurasa huo |
Mtu huyo ni mvulana ambaye inasemekana kuwa alikuwa akimpenda
msichana aitwaye Samira Osman lakini alipokataliwa, aliamua kufungua ukurasa
huo kwa hasira.
![]() |
Mkononi amejichora jina la Samira, msichana aliyemkataa |
Hivi ndivyo anavyoweka picha za wasichana zikiwa na maelezo kuwa wanataka wanaume matajiri huku maelezo akiyaandika mwenyewe.
![]() |
Candy 20 Kenyatta university wants a rich man who can
cater for her needs
|
MWANAUME NA MWANAMKE WAFUPI DUNIANI WAKUTANA
7:41 AM
No comments
Kwa mara ya kwanza katika historia,
Mwanaume mfupi na mwanamke mfupi duniani wamekutana, Mwanaume mfupi
anayeitwa Chandra Bahadur Dangi mwenye miaka 72 anatokea Nepal anaurefu
wa inchi 21.5 na Mwanamke mwenye miaka 18 Jyoti Amge anatokea Nagpur
India anaurefu wa ichi 25.
Ilikuwa ni katika kupiga picha kwa ajili ya promo ya maandalizi ya kitabu cha Guiness World Records kitakachotoka Septemba 2013.
Ilikuwa ni katika kupiga picha kwa ajili ya promo ya maandalizi ya kitabu cha Guiness World Records kitakachotoka Septemba 2013.
Tuesday, August 28, 2012
HIVI UMESIKIA ALICHOSEMA T.I.D KUHUSU TAARIFA ZA KUTAKA KUMUUA ALLY KIBA? HII NDIO STORI YENYEWE.
11:05 PM
No comments
Posted: 29th August 2012 by yusha
Kwenye U heard ya XXL Clouds Fm
august 28 2012 Gossip Cop Soudy Brown ameripoti kwamba kuna mwanamke
aliekamatwa na Polisi na kuhojiwa kwa saa nane wakati akiwa kwenye
mipango ya kumuua msanii wa bongo fleva Ally kiba.
Baada ya kuhojiwa na polisi kwa saa nane, mwanamke huyo alikiri kwamba alitumwa na T.I.D kwenda kumuua Ally Kiba.
Alipohojiwa na Soudy Brown,
T.I.D amesema “kwa nini nimuue Ally Kiba bwana, si mtu wangu nampenda
kabisa bwana, kweli sasa hivi niko polisi kwa ajili ya kuhojiwa, nilikua
safari, nimerudi sasa sijui mwanamke gani anaweza kufanya hivyo, siwezi
kufanya hivyo, kwa sababu gani? toka nimezaliwa sijawahi kugombana na
Ally Kiba, ukibisha muulize mwenyewe kama ameshawahi kukorofishana na
mimi,nia ya hao watu ni kuniangusha mimi nionekane ni mtu mbaya nisiuze
mziki wangu nisipendwe”
Soudy alipomtafuta meneja wa
Ally Kiba alijibiwa “hakuna taarifa zozote ambazo ziko tayari kutolewa
kwenye vyombo vya habari sasa hivi lakini ikiwa tayari utakua wa kwanza
kujua”
Monday, August 27, 2012
JINSI MASHEHE WALIVYOKWEPA KUHESABIWA KWENYE SENSA.
10:53 PM
No comments
Posted: 28th August 2012 by yusha
Zoezi la sensa ya watu na
makazi kwenye mkoa wa Kigoma lilipata ugumu kutokana na waumini wa dini
ya kiislamu wanaopinga kuhesabiwa kukimbilia misikitini hivyo kutofikiwa
na makarani waandikishaji.
Mkuu wa wilaya Kigoma Ramadhani
Maneno amesema kwenye pitapita yao kufanya tathmini wamekutana na ugumu
huo na tayari wameanza kuufanyia kazi, maeneo ambayo wamegundua tatizo
hilo ni pamoja na Mwandiga na Katonga ambapo licha ya kutaka kuongea na
viongozi wa misikiti hiyo, wameshindwa kupata ushirikiano wowote hivyo
amesema kamati ya ulinzi na usalama inatarajia kukaa kujadili ili kuona
hatua za kuchukua.
Amekaririwa akisema “kuna
baadhi ya viongozi wa kiislam wameshawishi waislam wenzao kwenda kulala
misikitini ili kusiwe na nafasi tena kwa makarani wa sensa kuingia
misikitini, nilipojaribu kwenda kwenye msikiti wa Mwandiga kujaribu
kushawishi niongee na viongozi wao, sikufanikiwa”
Mwandishi Fadhili Abdallah
anasema Mkuu huyo wa wilaya amethibitisha jumla ya kaya 40 kati ya 64
kwenye kijiji cha Bubango kata ya Bitale Kigoma Vijijini, zimekataa
kuandikishwa kufuatia maelekezo ya viongozi wa kaya hizo.
HIVI NDIVYO SERENGETI FIESTA 2012 TANGA ILIVYOKUA.
10:15 PM
No comments
Posted: 28th August 2012 by yusha
Recho nae alifanya poa sana.. kuna video yake hapo chini jinsi alivyovionyesha viuno pamoja na dancers wake.
MSIMAMO MPYA WA SAMUEL ETOO KUHUSU TIMU YAKE YA TAIFA.
9:46 PM
No comments
Posted: 28th August 2012 by yusha
Mwandishi Shaffih Dauda wa
shaffihdaud.com ameripoti kwamba mchezaji Samuel Eto’o amekataa
kuichezea Cameroon katika kutekeleza mgomo wake dhidi ya kile
alichokiita mpangilio mbovu na mazingira yasioeleweka katika kikosi cha
timu ya taifa.
Etoo alikuwa kwenye kikosi cha
Cameroon kwa ajili ya kupambana na Carpe Verde katika michuano ya kufuzu
kombe la mataifa ya Afrika September baada ya kumaliza adhabu yake
kufungiwa miezi nane.
Lakini Eto’o alisema kwenye
barua yake aliyoiandika kwa shirikisho la soka la Cameroon kwamba
hatoweza kurejea kwenye timu ya taifa kwa sababu matatizo yote
yaliyomfanya akafungiwa bado hajatafutiwa ufumbuzi.
Eto’o ambaye ameshaichezea nchi
yake mechi 109 na kufunga magoli 54, alifungiwa kutokana na kuongoza
mgomo wa wachezaji baada ya kutolipwa posho zao, shirikisho
la soka la Cameroon liliamuarifu Eto’o na mwanasheria wake pamoja na
timu yake ya Anzhi Makhachkala kwamba kifungo chake kimeisha mapema wiki
hii ambapo baada ya hapo kocha
Denis Lavagne akamchagua Eto’o katika kikosi chake cha wachezaji 23
kwa ajili ya kucheza dhidi ya Cape Verde tarehe 8 mwezi ujao kwenye
mchezo wa raundi ya kwanza ya kufuzu kushiriki AFCON 2013.
Lakini nahodha wa Cameroon bado
amekosa furaha dhidi ya masuala ya uongozi mbovu kwenye timu ya taifa
na suala lao la kuwapandisha wachezaji ndege daraja la pili tena kwenye
safari ndefu – na kutokana na sababu hizo mshambuliaji huyo wa zamani wa
Barca amejiondoa kwenye timu ya taifa.
Amekaririwa akisema “timu yetu
ya taifa inaendelea kupotea kutokana na mazingira mabovu na mpangilio
usioleweka, vitu ambavyo haviendi sawa na michezo ya kisasa, nina mashaka mashabiki wa timu ya taifa wataelewa hatua yangu hii ambayo mlengo wake mkuu ni kubadilisha mambo yote ya ovyo, timu ni taasisi yenye heshima ambayo imechangia sana mafanikio ya nchi”
Nape Aikomalia Chadema, Akataa Kuomba Radhi
3:42 AM
No comments
Akataa kuomba radhi, asema tuhuma
atazithibitisha mahakamani, Amtaka Dk. Slaa kuandaa bilioni 3 na
shilingi moja. Ni kwa kudai CCM inaingiza silaha nchini.
KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye amewataka Chadema kwenda mahakamani haraka badala ya kusubiri kuombwa radhi kama walivyotaka ili kusafishwa dhidi ya madai ya chama chao kupewa mabilioni ya fedha na mataifa tajiri.
Aidha amemtaka Katibu Mkuu wa chama hicho Dk. Wilbrod Slaa kuiomba radhi CCM la sivyo itamburuza mahakamani kudai fidia ya sh. bilioni 3 na shilingi moja, kwa kuituhumu uongo kwamba imeingiza silaha kutoka nje ya nchi tena bila kulipia ushuru.
Nape alisema hayo leo Agosti 27, 2012, kwenye mkutano wake na waandishi wa habari, uliofanyika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, mtaa wa Lumumba mjini Dar es Salaam.
"Bila shaka mmesikia jana Chadema wakinitaka niombe radhi au wananipeleka mahakamani kudai fidia ya sh. bilioni 3, kwa madai eti nimesema Chama hicho kinapata mabilioni ya fedha kutoka kwa mataifa tajiri. Mkubwa hatishiwi nyau, nawataka waende haraka mahakamani wala wasisubiri hizo siku saba", alisema Nape.
Alisema, CCM inao ushahidi wa kutosha kuhusu madai aliyotoa Nape dhidi ya Chadema na kwamba huyo tayari kutoa uthibitisho huo mahakamani badala ya kuomba radhi.
"Nadhani wakienda mahakani itapendeza zaidi maana huko ndiko pazuri kutoa uthibitisho kuhusu tuliyosema, na ninawahakikishieni tukishathibitisha na Msajili wa Vyama akaupata uthibitisho huo chama chao kinafutwa", alisema.
Kuhusu CCM kumburuza Dk. Slaa mahakamani, Nape alisema, ameshawaagiza wanasheria wa Chama, kuandaa barua ya kusudio la mashitaka hayo, na Dk. Slaa atapelekewa ili aamue kama ataomba radhi au atakuwa tayari kwenda mahakamani.
"Wakati wanakwenda mahakamani, Chadema wamwambie babu yao ajiandae kuomba radhi au kuburuzwa mahakamani kuilipa CCM fidia ya sh. bilioni 3 na shilingi moja kwa kuizushia CCM uongo kwamba inaingiza silaha nchini tena", alisema Nape.
Bashir Nkoromo
Blogger & Senior Photojournalist
Uhuru Publications Ltd,
Publishers of Uhuru, Mzalendo and Burudani tabloids
Cell; +255 712 498008, +255 789 498008, +255 773 600007 +255 756 646131
E-mail: nkoromo@gmail.com, bnkoromo@yahoo.com.
P O Box 9221, Dar es Salaam.Tanzania, East Africa
KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye amewataka Chadema kwenda mahakamani haraka badala ya kusubiri kuombwa radhi kama walivyotaka ili kusafishwa dhidi ya madai ya chama chao kupewa mabilioni ya fedha na mataifa tajiri.
Aidha amemtaka Katibu Mkuu wa chama hicho Dk. Wilbrod Slaa kuiomba radhi CCM la sivyo itamburuza mahakamani kudai fidia ya sh. bilioni 3 na shilingi moja, kwa kuituhumu uongo kwamba imeingiza silaha kutoka nje ya nchi tena bila kulipia ushuru.
Nape alisema hayo leo Agosti 27, 2012, kwenye mkutano wake na waandishi wa habari, uliofanyika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, mtaa wa Lumumba mjini Dar es Salaam.
"Bila shaka mmesikia jana Chadema wakinitaka niombe radhi au wananipeleka mahakamani kudai fidia ya sh. bilioni 3, kwa madai eti nimesema Chama hicho kinapata mabilioni ya fedha kutoka kwa mataifa tajiri. Mkubwa hatishiwi nyau, nawataka waende haraka mahakamani wala wasisubiri hizo siku saba", alisema Nape.
Alisema, CCM inao ushahidi wa kutosha kuhusu madai aliyotoa Nape dhidi ya Chadema na kwamba huyo tayari kutoa uthibitisho huo mahakamani badala ya kuomba radhi.
"Nadhani wakienda mahakani itapendeza zaidi maana huko ndiko pazuri kutoa uthibitisho kuhusu tuliyosema, na ninawahakikishieni tukishathibitisha na Msajili wa Vyama akaupata uthibitisho huo chama chao kinafutwa", alisema.
Kuhusu CCM kumburuza Dk. Slaa mahakamani, Nape alisema, ameshawaagiza wanasheria wa Chama, kuandaa barua ya kusudio la mashitaka hayo, na Dk. Slaa atapelekewa ili aamue kama ataomba radhi au atakuwa tayari kwenda mahakamani.
"Wakati wanakwenda mahakamani, Chadema wamwambie babu yao ajiandae kuomba radhi au kuburuzwa mahakamani kuilipa CCM fidia ya sh. bilioni 3 na shilingi moja kwa kuizushia CCM uongo kwamba inaingiza silaha nchini tena", alisema Nape.
Bashir Nkoromo
Blogger & Senior Photojournalist
Uhuru Publications Ltd,
Publishers of Uhuru, Mzalendo and Burudani tabloids
Cell; +255 712 498008, +255 789 498008, +255 773 600007 +255 756 646131
E-mail: nkoromo@gmail.com, bnkoromo@yahoo.com.
P O Box 9221, Dar es Salaam.Tanzania, East Africa
Sunday, August 26, 2012
Saturday, August 25, 2012
SHERIA MPYA YA VYOO VYA UMMA CHINA: NZI WASIZIDI WAWILI
11:29 AM
No comments
Sheria
hiyo inakataza choo kuwa na zaidi ya nzi wawili kwa wakati mmoja.Sheria
hiyo iliyowekwa na halmashauri ya mannispaa ya jiji la Beijing inalenga
kuhakikisha hali ya usafi katika vyoo vinavyotumiwa na jamii.
Hata hivyo haijawekwa wazi ni hatua gani zitachukuliwa iwapo nzi wa watu atakutwa chooni.
Sheria
nyingine ni kuhakikisha vyoo vinasafishwa kila mara na matumizi ya
vifaa vyakisasa na mafunzo ya kutosha kwa watu wanaovitazama vyoo hivyo.
Mwandishi
wa BBC mjini Beijing amesema sheria hizi mpya ni mahsusi kusaidia watu
wengi mjini humo ambao hawana vyoo majumbani mwao na wanategemea vyoo
vya umma. Bila shaka watakuwa wakitazama huko na huko kutafuta nzi wa
tatu yuko wapi..
Subscribe to:
Posts (Atom)