Blogger Widgets

Friday, November 30, 2012

WASANII WA BONGO FLAVA NA HIP HOP, WALALAMIKIWA KUTOHUDHURIA MAZISHI YA SHARO MILIONEA. December 1, 2012



Kupitia  kituo cha luninga cha EATV ndani ya kipindi cha Frieday Night Live jana, kuna malalamishi kibao yaliyojitokeza kwa baadhi ya wasanii wa kike waliokuwa wakihojiwa katika kipindi hicho.

Wasanii hao wakike wawili walionekana kukelwa na kushangazwa na kitendo cha wasanii wa miondoko ya bongo Flava hapa nchini kutojitokeza kabisaa katika mazishi ya msanii mwenzao
Hussein Sharo milionea aliyepata ajali tarehe 26 majira ya saa mblili za usiku mkoani Tanga na kupoteza maisha hapo hapo.

Wadada hao walili wakionekana
EAST AFRICA TV wakiongea kwa kuchungu, walidai kuwa wasanii wa hip hop nao waliohudhuria msiba wa Sharo Milionea walikuwa  wa kuhesabu kama Mwana FA, Roma, Ney wa Mitego Shetta na wengine.

Walidai kuhuzunishwa sana kwani wasanii wakubwa ambao pia walitajwa kutohudhuria msiba huo ni pamoja na
AY, Lady Jay Dee, Bob Junior, Timbulo, PNC, Dogo Janja, DJ Choka, Weusi na wasanii kibao. Mtangazaji wa kipindi hicho pia Sam Misago alishangazwa na kitendo cha wasanii wa hip hop kuto hata zungumzia msiba wa msanii Sharo milionea bali walionekana kufanya yao na kutoona umuhimu wa kuhudhulia msiba huo.

Wadada hao walidai kuwa kila msanii wa Bongo anamfahamu meneja wa Sharo Milionea maarufu kwa jina la
HK, meneja ambaye amekuwa akifanya kazi na wasanii kibao.Ni kwanini wakati amefikwa na msiba wa Sharo Milionea hakuna hata msanii mmoja aliyempigia simu kumpatia pole! hata kama walishindwa kuhudhulia msiba huo?

Katika upande wa
Comedy walidai wasanii wote hawakuhudhulia msiba wa Sharo milionea, kitu ambacho kimewakera sana na kuwaasa kujitokeza katika matatizo ya yanapokuwa yamejitokeza kwani na wao wakipata matatizo hayo watahudhuriwa na nani?

Yapo mengi zaidi yaliyozungumziwa katika kipindi hicho cha
Frieday Night Live ya East Africa TV

0 comments:

Post a Comment