Blogger Widgets

Celebrity Story from Different Place

Entertainment story of Bongo land and their work.

Story za wakali wa majuu

Burudani| Video| Tracks na Maisha yao.

Bongo Movie na wasanii wake kwenye maisha yao

News Movie| New Story| New Skendo.

Mafanikio

Story za walio vuka boda na mafanikio yao kama wajasiria-mali.

Elimika na Burudika

Life ya wasio na skendo na wenye skendo| Mafanikio yao na vioo wa jamii.

Monday, April 22, 2013

HIVI ULISHAZIONA PICHA NYIIIINGI! ZA SAFARI YA DIAMOND KUTOKA DAR KWENDA ZANZIBAR MSIBANI WA BI KUDUDE? ANGALIA HAPA HOUNE ILIVYOKUWA

Nilipopata taharifa za Msiba Huu.....Nilishitushwa sana..... lakini kadri muda ulipokuwa unazidi kwenda
ndio imani ikazidi kuniingia moyoni kuwa kweli bibi yetu 
kipenzi,Legendari wa muziki wa tanzania
atunae tena dunia....Nilisikitika sana na majonzi tele

 yalitawala moyoni mwangu......
Nilikuwa nipo nyumbani nikijianda na safari yangu ya kwenda

 Mkoani lakini nilihairisha
na kuamua lazima nikamzike bibi,Japo mkoani kulikuwa na 
maswala ya kazi....kama kioo cha
jamii lazima nioneshe mfano......Jana asubuhi ya tarehe 18 mwezi wa 
4 niliamka asubuhi na
mapema kuanza safari yangu kuelekea kisiwani Zanzibar.....
Sikuwa pekee yangu kwenye msafara huo
Niliongozana na dada yangu kipenzi Halima kimwana na Ndugu

 yangu wa karibu na Promota Nguli
barani Afrika Hamisi Tale a.k.a Babu Tale....
kwenda kumzika Bi kidude.......

Zifuatazo ni Picha wakati nikiwa Njiani kuelekea Zanzibar Mpaka kuwasili....!!



















Tukiwa tumewasili salama salimini Zanzibar kwa uwezo wa mwenyezi mungu......



kama msanii nilipowasili nilipokea simu kutoka kituo kimoja cha redio
mjini zanzibar kwenda kuongea dhamira yangu kuwepo zanzibar kwenye msiba huo.....


Baada ya kutoka kwenye mahojiano kwenye studio....Nilifarijika sana kukutana na
Producer Nguli Nchini Tanzania...G Love But I call Him Dad G....LONG TIME
Na yeye ndie aliekuwa Mwneyeji wetu kwa siku hii...

Baby J msanii kutoka zanzibar.....pia alijumuika na sisi kama mwenyeji wetu...

Kutokana na kuwahi safari....tulichelewa kupata kifungua kinywa tukaona isiwe mbaya
kabla ya kwenda kweye mazishi tukipata kifungua kinywa....!!

Video ya ‘Sio Mimi’ ya Madee inachochea usagaji? Tazama picha za utata hapa

Video iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu ya wimbo wa Madee ‘Sio Mimi’ hatimaye imetoka. Ni video kali lakini ina tatizo moja. Ingia ndani kuona ni lipi.
Ndani ya video hiyo kuna sehemu inayoonesha wasichana wakinyonyana ndimi na hivyo kuchochea masuala ya usagaji. Sehemu hiyo inaweza kuchangia video hii kupigwa vita.
madee 2
Picha za wasichana wakinyonyana ndimi kwenye video hiyo
Picha za wasichana wakinyonyana ndimi kwenye video hiyo
 

Thursday, April 18, 2013

MSIBA WA BILIONEA BABU SAMBEKE WAZUA GUMZO,,,,VIGOGO WATAWALA MSIBANI .... TUKIO KAMILI LA MAZISHI LIPO HAPA

DSCF8833

Jamal Sambeke mtoto wa marehemu akifunga jeneza la baba yake mara baada ya watu mbalimbali kutoa heshima zao za mwisho nyumbani kwake njiro Themi Mkoani Arusha
DSCF8840
Waombolezaji wakibeba jeneza la Bilionea Babu na kuweka kwenye gari maalumu tayari kwa safari kuelekea Moshi kwa mazishiDSCF8828
Watu wakitoa heshima za mwisho
DSCF8844
Watoto wa marehemu Sia na Getrude waliovalia nguo nyeupe
DSCF8834
Jamal akifunga jeneza la marehemu Babu Sambeke
DSCF8830
Jaji Aisha nyerere msibani pamoja na mkurugenzi wa kibo palace Vicent Laswai
DSCF8832 DSCF8848
Baadhi ya magari ya kifahari yaliyofika katika msiba huo
DSCF8838
Mkurugenzi wa hoteli ya Kibo Palace Vicent Laswai akizungumza msibani mara baada ya watu mbalimbali kutoa heshima zao za mwisho

DSCF8847
Waombolezaji
Mamia ya vigogo pamoja na watu mbalimbali wafurika nyumbabi kwa marehemu Bilionea “Babu Sambeke”Ernest Sambeke eneo la njiro jijini Arusha kuaga mwili wake unaotarajiwa kuzikwa kesho nyumbani kwake eneo la Karanga mjini Moshi huku msiba huo ukiwa tofauti na misiba mingine iliyozoekeaka hapa Nchini
Marehemu,Sambeke alifariki hivi karibuni katika ajali ya ndege aliyokuwa akiiendesha na pia mmiliki wa ndege hiyo ambapo ilianguka katika eneo la Kisongo na kusababisha kifo chake Mkoani Arusha
Shughuli za kuaga mwili wa marehu zilikamilika majira ya saa 8:45 mchana huku mwili huo ukipakiwa katika gari maalumu la kifahari tayari kusafirishwa kuelekea nyumbani kwake Moshi kwaaajili ya mazishi
Taratibu za kuaga mwili wa marehemu zilianza majira ya saa 5 asubuhi huku wafanyabiashara wa madini pamoja wafanyabiashara wengine kutoka hapa Arusha na Moshi walionekana kutawala msiba huo.
Katika zoezi hilo la kuaga mwili wa mareheu Padri Florentine Mallya ambaye ni mdogo wa marehemu aliongoza misa ya kumuombea marehemu na baada ya kumaliza alitoa fursa kwa watu mbalimbali kupita mbele ya jeneza kwaajili ya kuaga mwili Ndani ya jeneza marehemu alivalishwa nguo zake za kirubani huku ,baadhi ya wanajeshi kutoka jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) walionekana jana katika zoezi la kuuaga mwili wa marehemu ambapo baadhi yao walikuwa wamevalia sare za jeshi hilo
Hatahivyo,baadhi ya watu walionekana katika hali ya kawaida huku watoto wakionekana na nyuso za huzuni mda wote
Tofauti na misiba mingine nchini watu mbalimbali walipata fursa ya kupata chakula na vinywaji mbalimbali kwa kujihudumia vikiwemo vinywaji aina ya Bavaria ambapo watu waliohudhuria zoezi hilo walionekana wakijihudumia zaidi vinywaji vya bavaria
Magari ya kifahari yalionekana kutawala msiba huo huku barabara ya njiro ikionekana kuwa na msongamano kubwa iliyosababishwa na zoezi hilo la uwagaji wa mwili
Marehemu aliacha watoto watatu ambao ni Sia,Jamal,Getruda

JAMII BLOG

Wednesday, April 17, 2013

DIVA LOVENESS LOVE amtumia ujumbe huu mfupi wa maneno WEMA SEPETU. UJUMBE WENYEWE HUU HAPA

Kupitia account yake ya Instagram mwanadada Diva Loveness Love anayetangaza Clouds FM kwenye kipindi cha usiku Ala za Roho, inasemekana kuna mtu amefungua account ya facebook kwa jina hilo la diva na kuanza kumporomoshea mvua ya matusi mwanadada Wema Sepetu.

Angalia Picha mbalimbali za Maandalizi ya Mazishi ya Marehemu Bi Kidude.


Gari lililokuwa limeubeba mwili wa msanii mkongwe wa muziki wa tarab, marehemu Fatuma Binti Baraka 'Bi. Kidude', likiusafirisha kutoka katika Kijiji cha Kihinani na kuupeleka nyumbani kwake Rahaleo kwa matayarisho ya mazishi yatayofanyika kesho mchana katika Kijiji cha Kitumba, Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja. (Picha zote kwa hisani ya Othman Maulid wa ZanZinews)
Mwili wa marehemu ukishushwa katika gari wakat ukiwasili nyumbani kwake, Rahaleo kwa taratibu za mazishi yatakayofanyika kesho mchana na Kijiji cha Kitumba, Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja.
Ndugu, Jamaa na marafiki, wakiubeba mwili wa marehemu Bi. Kidude wakati ulipowasili nyumbani kwake, Rahaleo kwa ajili ya matayarisho ya mazishi yatakayofanyika kesho Kijiji cha Kitumba, Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja.
Mrajisi wa Baraza la Sanaa la Zanzibar, Khadija Batashi, akizungumza na waandishi wa habari jinsi alivyoupokea msiba wa msanii mkongwe wa muziki wa taraba nchini, Bi Kidude.
Matayarishi ya mazishi ya msanii wa muziki wa tarab, Bi. Kidude yakiendelea nyumbani kwake Rahaleo, mjini Zanzibar.
Mjukuu wa Bi. Kidude Omar Ameir, akiwasiliana na jamaa kwa ajili ya kuwajulisha msiba wa marehemu Bi. Kidude, baada ya mwili wa marehemu huyo, kuwasili nyumba kwake kwa ajilimatayarisho ya mazishi yatakayofanyika kesho mchana baada ya Swala ya Adhuhuri, ambapo atazikwa Kitumba.
Bi. Maryam Hamdani akilakiwa na Bi. Sihaba wakati akiwasili nyumbani kwa marehemu Bi. Kidude Rahaleo, mjini Zanzibar akiwa na majonzi.  
Waandishi wa habari wakizungumza na Mfadhili Mkubwa wa Bi. Kidude, Maryam Hamdan, kuhusiana na marehemu ambaye yeye alikuwa ni mtayarishaji na mratibu wa safari za Bi. Kidude nje ya nchi na katika matamasha mbalimbali aliyokuwa akihudhuria nje ya nchi wakati wa uhai wake.