Blogger Widgets

Friday, September 13, 2013

HII SASA NI ZAIDI YA LAANA. ANGALIA WANAUME WAWILI BOSI NA MFANYAKAZI WAKE WAKUTWA CHOONI PAMOJA


 
Stori: Richard Bukos na Issa Mnally
MDOSI au Kanjibai aliyefahamika kwa jina moja la Milah ambaye ni bosi wa kampuni moja ya ujenzi yenye makao yake Mwenge jijini Dar alinaswa chooni akiwa na mfanyakazi wake, John Carlos ‘Shabani’ (watu walimpachika jina la Shabani kutokana na Kanjibai wa kwenye Komedi) ikidaiwa walikuwa katika mazingira ya ulawiti, Ijumaa ‘Kubwa’ lina sinema yote.
 
...Choo walipokuwa wamejifungia Milah 'Kanjibai' na John Carlos ‘Shabani’.

Ishu hiyo nzito ilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo wawili hao walikuwa chooni humo kwa zaidi ya nusu saa na kuwasababishia usumbufu watu waliokuwa wakitaka kutumia choo hicho.

KISA KILIPOANZA
Siku hiyo ya tukio, mtu mwenye sauti ya kiume alipiga simu kwenye chumba cha habari cha Global Publishers, Mwenge jijini Dar na kupasha juu ya tukio hilo. Alisema:
“Jamani hebu njooni haraka hapa kwenye hii kampuni ya ujenzi ya… (jina lipo) iko hapa Mwenge. Kuna bosi wetu mmoja amejifungia chooni na mfanyakazi mwenzetu kwa zaidi ya robo saa sasa, sijajua nini kinaendelea humo ndani. Sisi wengine hapa matumbo ya kuendesha yametushika sijui tufanyaje?!”
Mtoa habari huyo alikwenda mbele zaidi kwa kuwaambiwa mapaparazi wetu waliompokelea simu wachukue Bajaj au Bodaboda ili kuwahi.
Sosi huyo kabla ya kukata simu aliweka wazi ramani ya kufika kwenye choo hicho na kusisitiza kwamba muhimu kuwahi kwa sababu huenda wanagombana.

MAPAPARAZI WAWASHA PIKIPIKI
Kufuatia msisitizo huo, mapaparazi wetu makini  waliwasha pikipiki zao, kila mmoja na yake na kushika njia kuelekea eneo la tukio.
Hata hivyo, kwa kuamini wanaweza kukutana na lolote, waliona ni vyema kwanza kwenda kutoa taarifa kwenye Kituo Kidogo cha Polisi cha Mwenge ambapo walipewa askari wawili kuelekea eneo la tukio.
 
...Ndani ya choo walimokutwa.


ENEO LA TUKIO SASA
Timu hiyo iliwasili kwenye eneo la tukio. Mlango wa choo hicho ulikuwa umefungwa lakini kwa mara moja tu haikuwa rahisi kugundua kama ulifungwa kwa funguo au kawaida tu.
 Afande mmoja alijitolea kugonga mlango wa choo hicho ili kupima ushirikiano utakaotolewa na wawili hao au mmoja wao.
Sauti iliyoonekana ni ya Kanjibai kutokana na kushindwa unyoofu wa lugha ya Kiswahili ilisikika ikiuliza:
“Nani wewee… taka nini huku?”
 
...Wakiwa chini ya ulinzi.

Afande: Sisi ni askari polisi, fungua haraka tunajua mko wawili humo ndani, fungua.
Kanjibai: Subiri kidogo.
Baada ya dakika kadhaa ambazo mapaparazi wetu hawakuzifuatilia, mdosi huyo alifungua mlango na kukutwa akiwa na ‘Shabani’.

WALICHOKUWA WAKIKIFANYA CHOONI
Katika maswali ya harakaharaka nje ya choo hicho kila mmoja alisema la kwake ambalo aliliamini linaweza kumchomoa kwenye skendo hiyo mbaya.
‘Shabani’ alisema yeye aliingia kwenye choo hicho baada ya kuitwa na bosi wake huyo ambapo alishindwa kumkatalia kwa kuogopa kupoteza ajira yake na kama inavyojulikana maisha ya Dar bila kazi ni ngumu kuyamudu.

 
...Mafuta aliyokutwa nayo Kanjibai ambayo mtaani hujulikana sana kwa jina la ‘mlainisho’.

Alipoulizwa walichokuwa wakikifanya ndani ya choo hicho, Shabani alibaki akiwatumbulia macho maafande, wakati mwingine mapaparazi wetu.
Kwa upande wake Kanjibai alipotakiwa kujieleza kisa cha kuingia chooni na mfanyakazi wake, alisema alimuomba wazame humo ili akamnyoe. Yaani Kanjibai alitaka kunyolewa.

IKAFIKA ZAMU YA KUPELEKWA KITUONI
Afande mmoja aliamuru wawili hao wapelekwe kituo cha polisi, lakini kabla ya kuanza safari, mdosi huyo aliingiza mkono kwenye mfuko wa suruali na kutoa vitu vyake kadhaa na kuwakabidhi wadosi wenzake waliofika ‘kumsaidia’ muda mfupi baada ya kunaswa.
Halafu aliingiza mkono kwenye mfuko mwingine na kutoa mafuta aina ya KY (pichani) ambayo mtaani hujulikana sana kwa jina la ‘mlainisho’ lakini askari alimwambia mafuta hayo yanatakiwa kituoni kwa ajili ya ushahidi hivyo asiwape nduguze.
Breki ya kwanza ilikuwa kwenye Kituo Kidogo cha Polisi Mwenge ambapo baada ya mahojiano mafupi walihamishiwa Kituo cha Polisi cha Kijitonyama ‘Mabatini’ ambapo walihojiwa zaidi kuhusiana na tukio hilo


CHANZO KWA HISANI YA: www.globalpublishers.info

0 comments:

Post a Comment