Blogger Widgets

Thursday, September 5, 2013

HIZI HAPA PICHA JINSI KIDONDA CHA AUNT KILIVYOARIBIKA KWAKUOZA, HATARINI KUKATWA MKONO

 Na Imelda Mtema

INASIKITISHA! Staa wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel Grayson ‘Gwantwa’ yupo hatarini kukatwa mkono kutokana na jeraha la chupa alilolipata hivi karibuni.
Aunt Ezekiel akisafishwa kidonda.
Tukio la Aunt kupigwa chupa na mwanamke aliyetajwa kwa jina moja la Yvonne nje ya Club Bilicanas, Posta jijini Dar, lilitokea Agosti 26, mwaka huu wakati staa huyo alipokwenda kujiachia na mshosti zake.
Baada ya kupigwa chupa siku hiyo, Aunt alikimbizwa katika Hospitali ya Aga Khan lakini bahati mbaya alikosa daktari wa kumtibu hivyo akalazimika kwenda kutibiwa katika Hospitali ya Dk. Mvungi, Kinondoni ambapo alishonwa nyuzi sita pamoja na dawa za kukausha kidonda.

Kidonda cha Aunt kilichoanza kuoza.
ALIKATISHA DOZI
Kwa mujibu wa chanzo makini, Aunt ni muoga wa dawa na wakati kidonda kikiwa bado hakijapona vizuri aliacha kumeza dawa alizopewa.
Chanzo hicho kilisema tatizo la staa huyo kukatisha dozi lilisababisha kidonda kishindwe kupona na badala yake kikaanza kutengeneza usaha na taratibu mkono ukaanza kuoza.
“Mkono ulifikia hatua ukaanza kuoza kwani licha ya kushonwa lakini kilibadilika rangi ndipo alirudi hospitali.

...Akisubiri kupatiwa matibabu.
ASAFISHWA UPYA
Imeelezwa kuwa mapema wiki hii, Aunt alirudi tena katika Hospitali ya Dk. Mvungi na kusafishwa upya kidonda baada ya madaktari kugundua tatizo lilizidi kuongezeka.

MKONO ULIANZA KUOZA
Kwa mujibu wa nesi wa hospitali hiyo aliyeomba hifadhi ya jina lake, hali ya Aunt ilimshtua daktari, akamwambia aombe Mungu kwani kidonda kilichimbika sana na tatizo kama hilo huweza kusababisha mtu kukatwa mkono.
 “Iligundulika mkono ulikuwa unaoza, daktari alimwambia amuombe Mungu kwani hatua iliyokuwa imefikia ni mbaya hivyo asipokuwa makini tatizo hilo litamfanya akatwe mkono,” alisema nesi huyo.

Mkono wa kushoto wa Aunt Ezekiel Grayson ‘Gwantwa’ baada ya kupasuliwa na Yvonne kwa chupa.
CHANZO CHA UGOMVI NI NINI?
Licha ya kuhusishwa na ugomvi wa kimapenzi baina yake na mpenzi wa Yvonne anayejulikana kwa jina la Joff, Aunt alisema ugomvi wao uliisha zamani na kila mmoja ana maisha yake.
“Yale mambo yalipita, yeye ana maisha yake na mimi nina yangu,” alisema Aunt.

Huyu ndiye Yvonne aliyempasua Aunt.
Wakati huohuo, taarifa ambazo Amani limezipata kuhusu mtuhumiwa wa Aunt, Yvonne ambaye alifikishwa katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay jijini Dar siku ya tukio, anahaha kukwepa kifungo kwani uchunguzi ukikamilika atapelekwa mahakamani kisha gerezani.

0 comments:

Post a Comment