Blogger Widgets

Wednesday, July 31, 2013

List ya mastaa wa bongo ambao wamefanya/walifanya kazi kama mabalozi wa kampuni kubwa.

Unaambiwa vyanzo vikubwa vya pesa kwa wasanii wakubwa huko Ulaya na Marekani ni udhamini wa kutoka kwenye makampuni mbalimbali ambayo huwapa mastaa hao kazi ya kutangaza bidhaa fulani za kampuni yao au kuwa balozi kamili wa kampuni nzima. Moja ya mafanikio makubwa ni pale unapomuangalia P.Diddy ambaye anaingiza pato kubwa sana akiwa anafanya kazi na Vodka ya Ciroc ambayo ni mali ya kampuni kubwa ya vinywaji duniani Diageo.
diddy-ciroc-vodka1
Tukirudi hapa nyumbani Tanzania kuna makampuni ambayo yamesha amini nguvu na nafasi ya wasanii kwenye kuzitangaza bidhaa zao japokuwa bado wasanii wanaendelea kupeleka kilio chao mbele kama alivyofanya Ommy Dimpoz kwenye Kili Music award wakati anapokea tuzo yake.
Hii hapa ni list ya watu maarufu wa hapa nchini Tanzania ambao waliweza kupewa na wengine wanaendelea hadi sasa hivi kufanya kazi na brand ili kufikia malengo ya kibiashara na kijamii ya brand hizo.

MWANA F.A NA SAMSUNG

1

Sio muda mrefu sana umepita tangu Samsung Tanzania kumtangaza Mwana F.A kama balozi wa bidhaa za Samsung hasa simu. Hii ilikuja mara baada ya kampuni hii ya vifaa vya electronic kuzindua simu ya Samsung Galaxy S4. Mwana F.A ni msanii ambaye amejijengea personality nzuri na uwezo wake mkubwa kwenye sanaa kwa miaka mingi, vinaweza kuwa ni baadhi ya vitu vilivyowavutia Samsung kumpa hili dili bwana Hamisi Mwinjuma.

B12 NA REDBULL
b12
Hamisi mwingine huyu baada ya Hamisi Mwinjuma, kati ya watu maarufu wa kwanza sana kipindi hicho kupewa kazi ya kuwa balozi wa kinywaji cha Redbull. B12 kutokana na kuwa ndiyo mtangazaji mkuu wa kipindi cha XXL ambacho ni moja ya vipindi vinavyosilizwa sana na vijana. Hivyo kumfanya moja kati ya vijana wanaosikilizwa sana na vijana wenzao hasa kwenye upande wa burudani. B12 au Hamisi Mandi alikuwa balozi wa RedBull kwa muda kadhaa ambapo ilifika wakati hadi alipata a.k.a nyingine ya B-Balozi. Kama ulikuwa hujui, B12 weekend hii ametajwa kwenye list ya moja ya watu maarufu kwenye kazi ya radio ndani ya Africa ambapo alishika namba tisa. Hii ni sababu nyingine ya kupata ubalozi wa brand tena.

MAREHEMU KANUMBA NA STARTIMES
3
R.I.P The great pioneer kama alivyokuwa anajiita, lakini jina lake lingine alilokuwaga nalo ni balozi wa Star Times. Kampuni hii ya ving’amuzi wakati inaingia kwenye soko la Tanzania ilitumia pia mbinu ya kimasoko kwa kumtumia mmoja kati ya watu maarufu kwenye TV. Baada ya kufanya tamthilia kwa muda mrefu na baadae kuhamia kwenye movie na kufanya vizuri zaidi, Kanumba alijipatia hili dili na kulifanyia kazi vizuri.Steven Kanumba alizunguka mikoa mbalimbali kwenye ziara za kuhamasisha bidhaa ya Startimes. Kazi hii haikuishia hapo, Kanumba alipiga picha za kutosha kutengeneza mabango ya matangazo kwa ajili ya promotion ya Startimes.
MZEE MAJUTO NA SHARO – AZAM
20

Marehemu Hussein Mkietti maarufu kama Sharo millionea akiwa pamoja na Mzee Majuto walipata dili tofauti tofauti kutoka kwenye makampuni makubwa. Moja wapo ni kufanya tu matangazo ya Airtel lakini pia walipata nafasi ya kuwa mabalozi wa Azam. Kwa wale waliowahi kwenda sabasaba mwaka 2012 kwenye banda la Azam, basi waliwaona Mzee Majuto na Sharo millionea wakiwa nje ya banda hilo katika kazi ya Azam. Kutoka kwenye moja ya vyanzo vya uhakika Mzee Majuto alisema ,”Mkataba wetu na Azam ni mzuri na tunamshukuru mungu kwa hili. Mkataba wetu unasema kwamba tutahusika kwenye kutengeneza matangazo ya bidhaa za Azam,promotion za wazi pamoja na kupewa udhamini kama tukifanya shughuli yetu ya pamoja na mwanangu Sharo”. Hii ilikuwa kabla ya Sharomillionea kufariki, lakini hivi sasa Mzee Majuto anaendelea na dili hili kama kawaida.

AMBWENE YESAYA (A.Y) NA AIRTEL
SONY DSC
Boss wa Unity Entertainment, mkali toka kipindi cha ngoma yake kali “Raha tu” hadi “Bed and breakfast” hadi siku hizi na “Party Zone” ali-sign mkataba kufanya kazi na Airtel Tanzania. Kama Mzee Majuto na Sharo walivyofanya matangazo ya Airtel na baadaye kupata dili lingine na Azam. A.Y aliwahi kufanya tangazo la T.V, Radio na printing aki-promote moja bidhaa za Vodacom Tanzania. Lakini baadaye baadaye sana akapata dili la kufanya kazi na Airtel.
ADAM MCHOMVU NA COCACOLA
adam_mchomvu
Mtangazaji wa XXL na Bongoflava vyote vya Clouds FM, aliwahi kuwa balozi wa Cocacola kwa muda kadhaa. Adam Mchomvu alihusika katika vitu kadhaa vya Cocacola kama kuwapa watu mbalimbali zawadi kutoka Coca Cola.

DIAMOND PLATINUMZ NA COCACOLA
nn

Huyu jamaa anajiita Coca Boy, kama unataka kujionea hilo nenda kwenye account ya Instagram ya huyu jamaa ndiyo utaona jinsi gani anautendea haki ubalozi wake. Diamond akiwa kwenye interview na XXL alisema kwamba, “Mimi nilipata nafasi ya kufanya tangazo la mashindano ya Cocacola, lakini nilikuwa na malengo na nikaamua kuwapa zaidi. Nilijifanya kama balozi wakati kabla sijawa balozi kamili. Kwa hiyo jamaa wakaona duh huyu jamaa hatujampa hii kazi anafanya hivi. Je tukimpa kazi itakuwaje?. Hapo ndiyo nikapata hii kazi”.
Diamond ni msanii ambaye anatajwa kupata mafanikio sana hapa Tanzania, kwa upande huu wa kuwa balozi wa Cocacola anafanya vizuri sana kitu ambacho kinaweza kuyavutia hata makampuni mengine.

st
Tangazo la Startimes ambalo Kanumba alitokea
PICT6_8246
A.Y akiwa kwenye shughuli zake za kibalozi
PICT1_8079
mwana11
Mwana F.A akikabidhiwa Samsung4
mw2
G8 maxresdefault

 

0 comments:

Post a Comment