Blogger Widgets

Friday, July 12, 2013

Picha 7 za huyu Mtanzania ambae yuko safarini akitembea kwa mguu kutoka Mbeya mpaka Dar

.
.
Anakwambia safari yake ya kutembea kwa mguu kutoka 87.8 Mbeya mpaka Dar es salaam anaiita Uzalendo Tour kuisupport Taifa Stars na anategemea baada ya kuimaliza, watu wengi wataiunga mkono timu ya taifa Taifa Stars.
Anavyotembea kwa sasa anakutana na watu wengi sana na watu wengi wamekua wakimpigia simu baada ya namba yake kutajwa hewani Clouds FM, wengine amekutana nao njiani na wamekua wakimpa vitu mbalimbali vikiwemo viatu na nguo mpya.
Katoka Mbeya saa kumi alfajiri akafika Makambako saa moja na dakika 19 akiwa tayari katembea kilometa 186, akachukua gari mpaka 92.9 Iringa mjini kwa sababu ilikua imeshakua usiku tayari… akachukuliwa na gari la Wambura mdau wa Power Breakfast ya Clouds FM na kumuacha Iringa mjini alikolala mpaka asubuhi na kuianza safari tena.
Anakwambia saa nane kamili alikua anauanza mlima Kitonga na akaumaliza kwenye saa tisa na dakika kadhaa, baada ya hapo alitembea mpaka kitongoji cha mwisho kabla ya kuianza Ruaha kisha akachukua gari mpaka Morogoro mjini kwa sababu ilikua usiku tayari,  ameamkia 88.5 Morogoro mjini na sasa anakuja 88.5 Dar es salaam.
.
.
Anasema hii ni idea aliyokua nayo kwa muda mrefu sana lakini akashindwa kuifanya kutokana na kukosa mda ila anamshukuru sana Gerald Hando wa Power Breakfast @Cloudsfm ambae amemsaidia sana kufanikisha hii safari.
.
.
.
Ripota wa nguvu Addo November akiwa na wenzake kwenye picha ya pamoja.
.
.
.
.
.
.

0 comments:

Post a Comment