Blogger Widgets

Wednesday, August 14, 2013

ANGALIA PICHA ZA NYUMBA ZILIZO JENGWA KATIKATI YA MAKABURI MKOANI IRINGA ZIKIVUNJWA LEO

Mgambo  wa  Halmashauri ya Manispaa ya  Iringa na  viongozi mbali mbali wakielekea  kuvunja nyumba zilizojengwa makaburi ya Mtwivila  leo
Mgambo  wa Manispaa ya  Iringa na mwanasheria  katikati Bw Innocent Kihaga  wakielekea  kuvunja nyumba  zilizojengwa makaburini Mtwivila
Mgambo  wa Halmashauri ya Manispaa ya  Iringa  wakivunja  nyumba  iliyojengwa katikati ya makaburi ya Mtwivila
Kaburi  hili la Rashid M. Lukuvi likiwa  jirani kabisa na ukuta  wa nyumba  hiyo iliyovunjwa

Hii  ndio  nyumba ambayo ipo  jirani na kaburi la marehemu Idd Chonanga aliyekuwa  diwani wa kata ya Nduli kaburi  lenye mashada kushoto ,na hapo  waliposimama mgambo ndipo alipokaa waziri mkuu Mizengo Pinda  wakati wa mazishi na viongozi mbali mbali  wa mkoa wa Iringa
Uvunjaji wa  nyumba wa nyumba ukiendelea huku mmiliki wake amepewa  siku 30  kuanzia  leo  kuivunja
Wananchi ambao  wamezika  ndugu  zao katika makaburi hayo  wakishuhudia  zoezi hilo
HATIMAYE Halmashauri ya  Manispaa ya  Iringa imeivunja nyumba  iliyokuwa ikijengwa katikati ya makaburi  ya Mtwivila   ambayo  iliripotiwa na mtandao huu  na  vyombo mbali mbali  vya  habari likiwemo gazeti la Jamboleo , radio Ebony Fm na  radio Cloud FM  pamoja na   nyumba nyingine mbili ambazo pia zilikuwa  zikianzwa  kujengwa eneo hilo .

Pamoja na  kuendesha  zoezi la  kuzivunjwa  nyumba  hizo ambazo  zilikuwa katika  hatua ya mwanzo  kabisa  pia Halmashauri hiyo  imetoa  muda wa  siku  30  kuanzia  leo  kwa mmiliki  wa  nyumba nyingine iliyokutwa  imekamilika ambayo pia  imejengwa karibu na makaburi ya Mtwivila eneo ambalo waziri Mkuu Mizengo Pinda alikaa wakati  wa mazishi  ya  aliyekuwa diwani wa kata ya Nduli marehemu Iddi Chonanga

Hatua ya  kuvunjwa kwa makaburi hayo  imekuja  ikiwa ni  siku  mbili zimepita  baada ya mtandao huu  wa matukio daima  kuibua suala  hilo  kuibua ujenzi huo holela  na  ni  siku  moja  baada ya mkurugenzi mtendaji  wa halmashauri ya  Manispaa Bi  Terresia  Mahongo  kutoa agizo kwa  maofisa mipango  miji , afisa ardhi na mwanasheria  wa Manispaa ya  Iringa  kufika  eneo hilo  ili  kuchukua hatua sitahiki.

Zoezi la  kuvunja nyumba  hizo  leo  majira ya  saa 3 asubuhi limeongozwa na maofisa mbali mbali  wa Manispaa ya  Iringa akiwemo mwanasheria  wa Halmashauri  hiyo Bw Innocent Kihaga pamoja na mgambo  zaidi ya  watano wa Halmashauri  hiyo.

Kuvunjwa  kwa  nyumba  hizo  kumeshuhudiwa na umati  mkubwa wa  wananchi  wa  maeneo mbali mbali ya mji  wa Iringa ambao  walifika  kushuhudia  utekelezaji  wa agizo la mkurugenzi baada ya  baadhi  yao  kudai  wamiliki wa nyumba  hizo  wamejenga katika makaburi ya ndugu  zao  hivyo  walikuwa  wakishindwa  kuchukua hatua  kutokana na kutojua  wahusika  wa  ujenzi huo wa nyumba makaburini.

na fransicgodwinblogspot

0 comments:

Post a Comment