Blogger Widgets

Wednesday, May 15, 2013

Mwisho wa kusubiri ni kesho-MwanaFA

Mwanamuziki anayesifika kwa tungo zenye uwezo wa kusambaza misemo mitaani, Hamees mwin'jumah, au MwanaFA kama wengi walivyozoea kumuita, sasa ametangaza kuiachia mtaani ngoma yake ya Kama Zamani ambayo mwanzoni ilikuwa iingie mtaani Februari 25 mwaka huu(..kama inavyoonekana kwenye Poster)
"Kulikuwa na sababu za kibiashara, ikabidi ingoje lakini sasa, the wait is over, na kuanzia kesho itakuwa ikiuzwa kwenye mitandao na pia itakuwa ikisikika redioni.
Katika wimbo huo MwanaFA amewashirikisha wanamuziki kutona The Kilimanjaro Band pamoja na Man'dojo na Domokaya

0 comments:

Post a Comment