Blogger Widgets

Celebrity Story from Different Place

Entertainment story of Bongo land and their work.

Story za wakali wa majuu

Burudani| Video| Tracks na Maisha yao.

Bongo Movie na wasanii wake kwenye maisha yao

News Movie| New Story| New Skendo.

Mafanikio

Story za walio vuka boda na mafanikio yao kama wajasiria-mali.

Elimika na Burudika

Life ya wasio na skendo na wenye skendo| Mafanikio yao na vioo wa jamii.

Thursday, May 30, 2013

MUONE MBUNGE WA NYAMAGANA ALIVYOCHAFUA HALI YA HEWA BUNGENI, NAIBU SPIKA JOB NDUGAI AHAIRISHA KIKAO

 


Mbunge wa Nyamagana, Ezekiel Wenje, leo amechafua hali ya hewa bungeni baada ya kusoma hotuba yaake iliyowakasirisha wapinzani wenzao wa Chama cha CUF, jambo lililomfanya Naibu Spika Job Ndugai, kuahirisha Kikao cha Bunge mapema asubuhi.
Wabunge wa CUF wakisimama na kucharuka huku kila mmoja akifoka kivyake
.....
Wabunge wa Chama cha CUF wamezua tafrani hiyo Bungeni mjini Dodoma leo wakati Mbunge huyo wa Nyamagana, akisoma hotuba ya Kambi ya Upinzani ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Wenje akiendelea kusoma hotuba hiyo ndipo Mbunge wa Mtambile (CUF), Masoud Abdalla Salim, aliomba muongozao kwa Naibu Spika, Job Ndugai, akipinga maneno yaliyokuwa yameandikwa katika ukurasa wa nane wa hotuba hiyo yaliyosomeka Hivi:-

Mheshimiwa Spika wa Upande wa CUF, kutokana na itikadi zake za mrengo wa kiliberali ambazo miongoni mwa misingi yake mikuu ni pamoja na kupigania haki za ndoa ya Jinsia moja, usagaji na ushoga hii ni kwa mujibu wa tangazo lao la kwenye mtandao wa umoja wa maliberali ulimwenguni, ikiungwa mkono na Waziri wa Haki na usawa wa Uingereza, Lynn Featherstone kutoka Chama cha Libera Democratis.

Baada ya hapo wabunge wa Cuf walisimama na kusema wakitaka maneno hayo yafutwe ingawa msomaji wa hotuba hiyo alikuwa hajafika katika ukurasa huo wa hotuba wakati huo msomaji alikuwa amefika kwenye ukurasa wa nne.

Baada ya kuona mabishano na kutoelewana ukumbini humo, Naibu Spika , Job Ndugai, alitumia busara zake na kutangaza kusitisha shughuli za Bunge kabla mambo hayajawa mabaya maana kulikuwa na kila dalili za kuanza kushikana mashati baada ya baadhi ya wabunge wa Chama hicho kuanza kufoka kwa sauti kubwa ndani ya Bunge, bila kufuata utaratibu.

REST IN PEACE NGWAIR - PICHA ZA MATUKIO YANAYOENDELEA AFRIKA KUSINI ULIPO MWILI WA MAREHEMU ALBERT MANGWEA

Muonekano wa nje wa hospitali ya St Hellen Joseph, ulipokuwa mwili wa marehem Albert Mangwea

Millard akifanya mahojiano na mmoja wa watanzania walioko Soth Africa

Nje ya mochwari ya Serikali Hillbrow Johannesburg ulikohamishiwa mwili wa Ngwea ni Watanzania wakiongozwa na Kinje Ngomale Mwiru wakitazama sample ya majeneza mbalimbali ili wajue la kununua, hapa walikua na mfanyabiashara wa kampuni ambayo pia huwa inashughulika na kusafirisha miili ambapo gharama yake ni zaidi ya milioni nne na nusu.



Millard Ayo akifanya interview na mmoja wa Watanzania nje ya hospitali alikolazwa M2TheP.

Wednesday, May 29, 2013

Nu-joint Mwakalukwa akiwashirikisha Gentriez na Mwiro wanakwambia ngoma inaitwa "NENDA" sikiliza na ku-download hapa

Ni mkono toka kwa Mwakalukwa akiwashirikisha Gentriez toak wanene entertainment na Mwiro toka meccaCheka wanakwambia "NENDA" mkono umepikwa pande za noizmekah studios Arusha kwa DefXtro sikiliza HAPA kwa mawasiliano zaidi check na mwaka kupitia +255 718 441 699 keep supporting Tazanian Music

Toka New Way Music, Record label inayomilikiwa na producer Mosco "I jus Wanna Dance"



Toka New Way Music, Record label inayomilikiwa na producer Mosco wanakuja vijana watatu wakishirikiana na mwanadada Eslyne katika ngoma yao mpya inayoitwa "I jus Wanna Dance" ilorekodiwa katika studio za noizmekah chin ya Defxtro, Hii ngoma iwaendee club maniacs wote around tha world,Tunajipanga kushoot video yake anyday soon..kusikiliza I jus Wanna Dance bofya HAPA na endelea kusupport Tanzanian Music.For more info check na +255 718 402 868

Vanking akiwa amemshirikisha mwanadada toka Uganda anayekwenda kwa jina Renez na wimbo wa "Nivute" ANGALIA HAPA

Anakuja Kijana Vanking akiwa amemshirikisha mwanadada toka Uganda anayekwenda kwa jina Renez na wimbo wa "Nivute" ilosukwa pande za noizmekah studios Arusha, Ngoma ni mahadhi ya dancehall kuisikiliza download HAPA na kwa mawasiliano zaidi check na Vanking kupitia +255 713 367 162 

Anakuja MTC,na ngoma mpya kwa jina "Hapa Hafungwi Mtu" SIKILIZA NA KU-DOWNLOAD HAPA

Anakuja MTC,na ngoma mpya kwa jina "Hapa Hafungwi Mtu" inayozungumzia zaidi mateso na athari wanazopata washtakiwa wa kesi za kusingiziwa ikiwemo dhuluma,kupoteza mali, kufungwa kwa tuhuma ambazo hawakuhusika. Ikiwa ni real life experience,MTC anatarajia kuja na Album kamili January 2014. Hapa hafungwi mtu imerekodiwa katika studio za Noizmekah na ni single ya utambulisho na ujio mpya wa MTC anayemiliki Studio ya YABISI RECORDS, "Uwongo umejitenga kwenye Ukweli na sasa Yabisi Society itakuwepo tena Mtaani kama zamani,Hakipotei kitu" asema MTC..Pata kusikiliza ngoma HAPA na kwa mawasiliano zaidi check na +255 757 160 464 au +255 763 282 697 Support Tanzanian Hiphop

DULLAH WA PLANET BONGO APATA MTOTO WA KIKE USIKU HUU

Tarehe 29 mwezi wa 5 itakuwa ni tarehe isiyosahaulika kwa mtangazaji nguri wa kipindi cha PLANET BONGO ya EATV bwana Abdallah Ambua au almaaruf kama Dullah Planet baada ya mke wake kipenzi Amina Kagambo kufanikiwa kujifungua salama mtoto wao wa kwanza katika Hospitali ya Mikumi mnamo wa Majira ya saa tatu na nusu usiku huu... Mtoto huyo ni wa kike wamemtunuku jina la Tamirah this is diamond inawapongeza na inawatakia wanandoa hawa Upendo na mafanikio mema katika kumlea na kumkuza binti yao kipenzi....




SOMA RIPOTI HII HUWENDA NDIO CHANZO CHA KIFO CHA ALBERT NGWAIR

Albert Mangwair a.k.a Mimi a.k.a Ngwair a.k.a Cowboy enzi za Uhai Wake
--
Albert Mangwair a.k.a Mimi a.k.a Ngwair a.k.a Cowboy ni msanii wa Hip Hop ya Bongo kutoka mkoani Dodoma.
Alihamia jijini Dar es Salaam, Tanzania ambako alikokutana na mtayarishaji mahiri wa mziki P Funk 'majani' au Kinywele Kimoja, na kuanza kufanya naye kazi. Hiyo ilikuwa ni mwaka 2003 ambapo alitoa kibao cha kwanza kiitwacho 'Ghetto Langu,' nyimbo ilimpatia umaarufu mkubwa. Mangwair pia aliwahi kushinda tuzo ya Kilimanjaro Music Awards kama mwana Hip Hop Bora wa mwaka 2005. Mwaka wa 2007 akatokea kwa wimbo wa kimya kimya akiwa na wana chemba. Katika Kimya Kimya anapagawisha. Marehemu kwa sasa Ngwair anatesa na nyimbo inayotamba kwa jina Washamba. Alifariki jana 28/05/2013.
-----
Taarifa ya Ripoti Kutoka Helen Joseph Hospital - Auckland Park, Johannesburg, South Africa.
Helen Joseph Hospital - Auckland Park, Johannesburg, South Africa.

The Medical report from Helen Joseph hospital, Dr. Shirley Radcliffe confirming that; Albert Mangwair died from: “Alcohol toxicity” after drinking too much, Over-exhaustion and drugs overdose.

The inquest heard that Albert 28, collapsed in his friend's home had been more than five-times the legal S.A drink-drive limit with 416mg of alcohol per 100 millilitres of blood in his system.

Dr. Radcliffe described the reasons for ICU admission included hypoxemia and one of his friend found “two empty vodka bottles in the car” and he had been suffering from the eating disorder (Bulimia) for several months before his death and endless partying session with little or no resting.



Sample taken from his stomach showed poly-drug cocktail and he overdosed Heroin, Cocaine 'crack' and cannabis 0.08gms was also found in his blood, and his death was caused by massive heart attack and respiratory failure followed by sudden heart stop...and end up dead within seconds.



*Ripoti hii kwa Mujibu wa Self Kabelele

DAR_ES_SALAAM: Msiba wa Ngwair upo Mbezi Beach, Taratibu za mazishi zaanza



WAKATI rafiki wa msanii Albert Mangwea, M To The P naye amefariki dunia asubuhi ya leo nchini Afrika Kusini, familia ya marehemu tayari imeanza taratibu za mazishi. Nyota wa Bongo Fleva, Albert Mangwea maarufu kama Ngwair, alifariki dunia jana jioni akiwa nchini Afrika Kusini.

 Inadaiwa Ngwair alifariki dunia kutokana na kuzidiwa na matumizi ya dawa za kulevya na wakati mwili wake unakimbizwa hospitali ya St Hellen Joseph, rafiki yake naye, msanii pia M To Te P alikuwa katika hali mbaya, pia kwa utumiaji wa dawa za kulevya. 

Taarifa kutoka Afrika Kusini, zimesema swahiba huyo wa Ngwair naye amefariki dunia. Kaka wa marehemu Ngwair, Kenneth Mangwea amesema msiba upo Mbezi Beach, Goigi mjini Dar es Salaam na taratibu za kuirejesha miili ya marehemu nyumbani zimeanza. Tayari vifo vya wasanii hao wawili vimeanza kuzalisha maswali magumu, kubwa likiwa ni utumiaji wa dawa za kulevya pekee ndio umesababisha vifo vyao, au kuna mambo yaliyojificha.

 Kimuziki, Ngwair aliibukia mkoani Dodoma ambako alikuwa katika kundi moja na Dark Master, Noorah na Mez B na amekuwa akishirikiana na M To The P tangu akiwa msanii anayechipukia baada ya kuhamia Dar es Salaam.

 Baada ya kuja Dar es Salaam, Ngwair akapata dili Bongo Records chini ya mmiliki wa studio hizo, Petter Matthysse ‘P Funk’ aliyemuinua zaidi kimuziki na kumfanya awe miongoni mwa wanamuziki nyota nchini. 

Wimbo wake wa kwanza kutamba ni Gheto Langu mwaka 2003 ambao ulimpatia umaarufu kabla ya kutoa albamu yake ya kwanza a.k.a Mimi mwaka 2003 ambayo ilimpatia mafanikio makubwa na kubadili maisha yake. Hata hivyo, mafanikio hayo yalimlevya na kujitumbukiza kwenye utumiaji wa dawa za kulevya, hivyo kujikuta akishindwa kufanya kazi ya muziki kwa usanifu na kuanza taratibu kufilisika hadi kuuza mali zake zote, ikiwemo gari aina ya Jeep. 

Ngwair kutoka kwenye kupanga nyumba nzima maeneo ya Sinza, Dar es Salaam akajikuta anarejea kuishi katika ‘magheto’ ya washkaji zake sehemu mbalimbali Dar es Salaam. Mwaka 2010, Athumani Tippo, mmiliki wa maduka ya Zizzou Fashions alijaribu kumuinua tena msanii huyo baada ya kumchukua kwenye lebo yake na kumuwezesha kutoa albamu ya pili, Nge. Hata hivyo, Nge haikufanya vizuri sana na kuzidi kumchanganya msanii huyo hivyo kutopea kwenye dimbwi la utumiaji wa dawa za kulevya na ‘kuharibika zaidi’. 

Mafanikio yake zaidi ni kushinda tuzo ya Kilimanjaro Music Awards kama mwana Hip Hop Bora wa mwaka 2005. Mwaka 2003, msanii Wayne Wonder aliyekuja kutumbuiza kwenye Fiesta aliondoka na CD ya wimbo Mikasi ya Ngwair baada ya kuvutiwa na kibao hicho alichowashirikisha Mchizi Mox na Ferooz. 


Ngwair alijaribu sana kumuinua kimuziki M, lakini pamoja na ukweli kwamba alikuwa ana kipaji, lakini hakufanikiwa, ingawa aliwahi kutoa albamu. Pumzikeni kwa amani. Mbele yenu, nyuma yetu. RIP.

Lady Jaydee, Mwana FA, Izzo B na wasanii wengine waahirisha show zao kwa heshima ya Albert Mangwea


Takriban masaa 17 toka habari za msiba wa mwana chemba, Albert Mangwea aliyefariki jana (May 28) huko Africa Kusini kusambaa, tayari wadau wakiwemo wasanii wa muziki wa kizazi kipya wamechukua hatua za kumpa heshima marehemu kwa kuahirisha shughuli za kiburudani zilizokuwa zifanyike weekend hii.
l-600x400
Kati ya show kubwa zilizokuwa zifanyike weekend hii ni pamoja na show ya “The Finest” ya Hamis Mwinjuma a.k.a Mwana FA ambaye ametangaza kuahirisha show hiyo na kuisogeza hadi June 14 kama mazishi yatakuwa tayari yamefanyika. “Sina uhakika,but I’ll pick June 14th kama brother tutakuwa tushampumzisha,” ametweet.

Show nyingine kubwa iliyoahirishwa ni ya “Miaka 13 Ya Lady Jaydee” ambayo sasa haitafanyika tena (May 31). Lady Jaydee alikuwa akizungumza asubuhi ya leo kupitia kipindi cha Power Jams cha East Africa na kusema haitafanyika mpaka pale watakapotoa taarifa zaidi.

Show zingine zilizokuwa zifanyike weekend hii ni pamoja na ya Kikosi cha Mizinga wakiongozwa na Kalapina ambayo nayo haitafanyika tena kama ilivyokuwa imetangazwa hapo awali.

Naye Khalid Mohamed a.k.a TID jana kupitia akaunti yake ya facebook alielezea maamuzi yake ya kuahirisha show yake aliyokuwa aifanye Maisha Club jana usiku (May 28) pamoja na show alizokuwa afanye Bukoba weekend hii.

Mwana hip hop Izzo Business aliyetarajia kufanya show weekend hii mkoani Mbeya alitweet juu ya mabadiliko yaliyotokana na msiba huu. “Naomba radhi kwa wote waliosubiria show yangu tar 31 / 5 / 2013 The vibe nimehairisha show kutokana na msiba wa ngwea taarifa zaidi zitatoka,” alitweet jana usiku.

Ukiachilia mbali wasanii ambao wameahirisha kufanya show zao kupisha msiba huu mkubwa kwa tasnia ya muziki wa kizazi kipya Tanzania, wapo wasanii wengine ambao walipanga kutoa nyimbo pamoja na videos wiki hii.

Ben Pol ni kati ya wasanii hao ambaye alikuwa anatarajia kuachia rasmi video ya wimbo wake mpya wa Jikubali (June 1). “Sidhani kama ninayo raha ya kutoa video yangu mpya wiki hii, naomba radhi, nitapisha shughuli za mazishi ya ndugu yangu #restInPeace Albert ametangaza kuahirisha kutoa video hiyo,” aliandika.

Naye rapper wa kampuni ya Weusi John Simon a.k.a Joh Makini ameahirisha kutoa wimbo wake mpya aliopanga kutoa alhamis (May 30) na sasa haitatoka mpaka pale atakapotoa tarehe mpya. Joh alitegemea pia kufanya show club 77 ambayo ameisogeza mbele. Alitweet “Kutokana na msiba huu mzito nimesogeza mbele kuachia ngoma yangu mpya pamoja na show yangu club 71 tegeta mpaka nitakapowatangazia tena.”

R.I.P ALBERT MANGWEA.

PICHA 2 INTERVIEW YA MWISHO YA ALBERT MANGWEA


theHOODinfotainment inapenda kutanguliza salamu za Pole kwa 
Familia ya Albert Mangwair
a.k.a Cowbama.........Ni huzuni iliyogubika ndani yao na ndani 
ya tasnia ya muziki wa Tanzania
kwa ujumla.....Ni ghafls na msiba wa kushtusha miongoni mwa watanzania 
wengi ndani na nje ya Tanzania waliokuwa wakifatilia muziki
wa marehemu Albert Mangwea kiujumla.....
Zifuatazo ni picha Mbili za marehemu Albert Mangwair alizopiga
 kwenye Interview yake ya mwisho kabisa
aliyofanyiwa na Mwanadada Fatna ndani ya kipindi cha HOTMIX cha EATV.....
Ngwair alipata kufunguka juu ya muziki wake na Collabo yake aliyofanya
 na mwanamuziki
chipukizi Mirror....Pia aliweza kuzungumzia mustakjabari wa 
muziki wa hip hop nchini Bongo
Pia aliweza kuweka wazi kuwa aliamua kuweka kambi nchini 
South Africa na kufanya muziki
International zaidi.......
Ingawa akufunguka juu ya vibao ambavyo alivyokuwa amerokedi nchini South Africa
huko ambapo Mauti yalipomkuta Siku ya jana.....

TAARIFA YA KIFAMILIA KUHUSU MAZISHI YA NGWEA NA JINSI MWILI HUO UTAKAVYOLETWA TANZANIA

Baba Mdogo wa Marehemu Mzee Mangweha ambaye yuko Mbinga Songea kikazi, amesema kuwa wamekubaliana na kaka yake mkubwa yaani baba mkubwa wa Ngwair, David Mangweha ambaye naye yuko Songea kuwa watu watakutanika Mbezi kwa msiba na pia mapokezi yatafanyika hapa Dar es salaam Mbezi Beach.
  
Ingawa bado kikao cha familia nzima hakijafanyika lakini baba huyo mdogo amesema wanaweza kulazimika kuzika Morogoro sehemu ambayo baba yake alizikwa.

Baba huyo mdogo alisema kuwa kesho ndo watarudi Dar es Salaam pamoja na kaka yake yaani baba mkubwa wa marehemu.
 
Kuhusu mwili kuletwa hapa Tanzania kutoka Afrika Kusini baba mdogo amesema kuwa mpaka sasa hawajajua jinsi gani mwili huo utafika hapa lakini kuna ndugu zao ambao tayari washaanza kufanya taratibu za kuwasiliana na ubalozi wa Afrika Kusini ili kujua ni jinsi gani mwili huo utafika hapa.

Kama kutakuwa na mabadiliko yeyote watakapowasili kesho baba mdogo na baba mkubwa baada ya kikao cha familia watatoa taarifa

"SITAKI KUSIKIA NYIMBO ZA NGWEA ZIKIPIGWA CLOUDS FM..WAO NDO WALIOMFANYA AANZE KUVUTA BANGI ILI KUONDOA MAWAZO"...P FUNK



Muda mfupi uliopita djchoka amepokea simu kutoka kwa Producer mkongwe hapa bongo anayejulikana kwa jina la P Fuck Majani na kumuuomba aipokee msg hii hapa chini na kuwaomba watanzania walijue hili na baadae atatoa barua rasmi.

Tuesday, May 28, 2013

Nay Wa Mitego atoa siri ya kwanini huvaa viatu vya pair mbili tofauti!

nay

Kuwa na ‘unique identity’ ni moja ya technics nzuri kibiashara kwa msanii sababu inafanya atambulike kirahisi na kwa haraka miongoni mwa wasanii wengi.
Hakuna ubishi kuwa baba kijacho Nay Wa Mitego is running the game right now, kupitia hit song aliyoshirikiana Diamond Platnumz.
Nay amekuja na style yake ya kuvaa viatu viwili vya pair mbili tofauti na ndivyo anavyoonekana mara zote anapokuwa popote iwe ni kwenye show au mtaani. Kama bado unashangaa au hujaelewa ni hivi, mfano anakuwa na pair mbili za viatu lets use Adidas na Puma, pair moja iwe nyeupe na nyingine nyeusi, mguu mmoja anavaa Adidas nyeupe na mguu mwingine anavaa puma nyeusi, that’s his new swag, sio uchawi lakini!!
Kris-Kross
Akiielezea style yake hiyo ya uvaaji viatu kupitia kipindi cha Hot Mix cha EATV Nay amesema “navaa hivi nikimaanisha binadamu hatufanani, wewe huwezi kuwa sawa na yule na mi siwezi kuwa sawa na wewe that’s the big point”.
Wapo wasanii wengine wa nje na hapa Tanzania ambao wamewahi kujaribu kufanya vitu vya kuwatofautisha na wengine. Mfano kwa nje kundi la Kriss Kross wao style yao ilikuwa ni kugeuza jeans mbele kuwa nyuma na nyuma kuwa mbele.
Mpoto
Hapa Tanzania mwana mashairi Mrisho Mpoto ana aina yake ya mavazi anayovaa muda mwingi yanayomtambulisha na pia mara kadhaa huwa anatembea peku bila viatu.

HIKI NDICHO ALICHOKISEMA ADAM MCHOMVU BAADA YA KUANDIKWA MATUSI KATIKA WALL YAKE YA FACEBOOK

Naomba kuchukua nafasi hii kuomba radhi kwa yeyote aliyekwazika kwa maneno machafu yaliyoandikwa kwa wall yangu, na pia naomba nieleweke kwamba sihusiki na chochote kupost au kuandika chochote kuhusu kikwete foundation na picha za jdee ukiwa naked, sina ugomvi na yeyote naheshimu hisia za kila mtu nikiamini kila mtu Anamaamuzi yake.. Aliyeamua kutumia jina langu kufanya hao najua sasa unajiskia vizuri baada ya matusi mengi niliyotukanwa.. Maisha hayaishii hapa siku zinaenda na ukwali utafahamika siku moja ... Mchana mwema !!
16Like ·  ·