Blogger Widgets

Wednesday, February 20, 2013

BAADA YA KANISA KUCHOMWA MOTO ZNZ, HIKI NDICHO WALICHOSEMA MCHUNGAJI NA MLINZI

.
Baada ya hili kanisa la Pool of Siloam Kianga Zanzibar kuchomwa moto saa 9 usiku wa kuamkia february 19 2013, Mchungaji msaidizi wa kanisa hilo Penuel Elisha amesema sio rahisi kujua kwa haraka aliyehusika na hilo tukio japokua kumekuwepo na historia ya mgogoro kati ya kanisa hilo na msikiti uliopo karibu na eneo hilo.

Namkariri Elisha akisema “tukio lilivyokua, majira ya saa kumi na dakika 34 nilipigiwa simu na mchungaji mwenzangu aitwae Israel akaniambia kanisani kwetu kumeshavamiwa na mlinzi anapigwa mawe, nikachukua hatua ya haraka kuna mchungaji wetu mgeni ambae ni mkuu wa kanda nikamuamsha nikamwambia tumeshavamiwa, nilikua na namba ya polisi mmoja wa Mwera ambae alietusaidia kwenye tukio lililopita la mwaka 2011, nikampigia akapokea na kuchukua hatua za haraka sana”

Kwenye sentensi nyingine naendelea kumkariri mchungaji huyu akisema “nakumbuka mwaka 2011 walikuja watu zaidi ya 80 wakiwa na nyundo na sururu wakalibomoa hili kanisa lakini jana yake uongozi wa Msikiti wa Kianga ulituita kwenye nyumba ya Sheha wakawa wanadai kwamba tunadai hatimiliki, uhalali wa kujenga kanisa hapa”

Mlinzi wa kanisa hilo ambae alikuepo wakati wa tukio amesema “mi nilikua nimekaa nyumba ya kisima cha kanisa, walivyopita nikatoka kule nikaingia humu ndani badae wakarudi wakanurishia mawe nikatoka nikakimbia kuwaamsha jamaa kwamba nimevamiwa, nikampigia mchungaji simu”

Mpaka sasa Jeshi la Polisi Zanzibar limesema linachunguza chanzo cha huo moto uliounguza sehemu ya kanisa hilo la POOL OF SILOAM lililopo Kianga nje kidogo ya mji wa Zanzibar, naibu Mkurugenzi wa makosa ya jinai Zanzibar Yusuf Ilembo amesema hilo tukio linahitaji uchunguzi wa kina ili kufahamu waliohusika ambapo mpaka sasa hakuna aliekamatwa.

0 comments:

Post a Comment