Blogger Widgets

Sunday, February 17, 2013

UMESIKIA ALICHOSEMA HALIMA MDEE KUHUSU BUNGE KUONDOLEWA LISIONEKANE LIVE? KAMA BADO, SOMA HAPA

 
Mbunge wa Kawe Halima Mdee (Chadema)

Najua kama umekua karibu na media katika siku za karibuni, stori kuhusu uongozi wa bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kutangaza mpango wa kutaka bunge lisiwe linaonekana live kwenye TV utakua umeisikia.
Ni maoni mengi ya Watanzania yametolewa huku asilimia kubwa ikionekana kupinga huo mpango ambao lengo lake ni kukwepa kuonekana kwa wabunge wanaovunja kanuni kwa kuropoka na kufanya vurugu.
Kwenye hii post ni maoni maalum ya mbunge wa Kawe Halima Mdee ambae namkariri akianza kwa kusema “mmhh… kwanza ni hoja ya kipuuzi sana na muhimu ikaeleweka kwamba bunge ni moja kati ya mihimili mitatu ya dola, kinachoonekana kutaka kufanyika ni muhimili mwingine wa dola kutokutaka umma ujue ukweli kwa kutumia watumishi wa bunge kwa mantiki ya katibu wa bunge kwa sababu yeye ndio ametoa hilo tamko ili kuzuia Watanzania wasipate taarifa ambazo tokea bunge limeanza kurushwa live wamekua wakizipata tofauti na ambavyo walikua wanapewa hizo taarifa katika mazingira ambayo sio ya wazi”
Kwenye sentensi nyingine Mh Mdee amesema “nasema hivyo kwa sababu kupitia bunge Watanzania wamejua mikataba mibovu ya madini, wamejua EPA, wamejua Richmond, Buzwagi, wamejua jinsi gani fedha zinavyotengwa kwa ajili ya bajeti zimekua zikitumika vibaya sana kupitia CAG report ambazo zimekua zinajadiliwa live, Serikali imeona inaumbuka na ikaamua sasa kupitia katibu wa bunge na kina Lukuvi, tunataja majina ya watu sababu tuna uhakika na tunachokisema na juzi imeumbuka, sasa wanatafuta statergy ya kuficha”
“Kama mlikua mnafatilia bunge la juzi mmeona kwamba wameweka sheria kusema kwamba mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG taarifa yake akiisoma haitajadiliwa hadi mwaka tena mwingine upite waende tena kuedit na kuleta majibu ya uongo, kwa hiyo kuna mrundikano wa vitu vingi ambavyo Serikali inaona mambo yakiendelea hivi inawezekana 2015 wakifika watakua wamechoka, sasa wanazuiaje? kwa kuleta vitu vya ajabu ajabu… kwa hiyo waache wananchi wajue nini kinachoendelea, kuna kanuni za bunge kama Mbunge anakiuka kanuni” – Halima Mdee
chanzo: millard Ayo

0 comments:

Post a Comment