Blogger Widgets

Monday, February 18, 2013

SABABU ZA DRAKE KUZUIWA NA MABAUNSA KUINGIA CLUB, SOMA HAPA UJUE NI KWANINI

.
Mtandao wa TMZ umeripoti kwamba rapper Drake alizuiwa kuingia kwenye club moja ya usiku huko Hollywood Marekani weekend iliyopita.
Sababu hasa ni kwamba hasimu wake, staa mwenzake ambae mwaka jana walirushiana chupa kwenye club moja ya usiku, mwimbaji Chris Brown tayari alikua ameshaingia ndani kwenye club hiyo hivyo mabaunsa walifanya kile walichoelekezwa cha kutoruhusu hizo sura mbili kuingia kwenye club hiyo kwa wakati mmoja.
Rihanna, Drake na Chris Brown, hii picha ilipigwa kabla hawajagombana.


Club nyingi sasa hivi zinahofia kuwaruhusu wawili hao kuwepo sehemu moja ili kuepuka yaliyotokea kwenye club waliyorushiana chupa ambayo ilifungwa kwa muda, pamoja na watu mbalimbali kudai fidia za kuumizwa kwenye ugomvi wa mastaa hao wawili ambao inaaminika ulikua ni wa kumgombania Rihanna.

0 comments:

Post a Comment