Blogger Widgets

Monday, March 18, 2013

HUYU HAPA YULE MWANAUME AMBAYE ANATARAJIWA KUFANYIWA OPARESHENI ILI KUWEKEWA UUME...

 
Historia mpya inakaribia kuandikwa duniani baada ya mwanaume ambaye anajulikana kwa jina Andrew Wardle, kutoka Stalybridge, Greater Manchester huko Uingereza ambaye alizaliwa bila uume, kufanya mpango wa kutengenezewa na kuwekewa kiungo hicho kwa njia ya oparesheni.

Mwanaume huyu ambaye kwa sasa anaumri wa miaka 39, anatarajiwa kuwa mwanaume wa kwanza kabisa duniani kufanyiwa oparesheni kama hii na ajabu zaidi ni kwamba, kiungo hiki kitatengenezwa kutoka sehemu ya mkono wake.
 
Andrew Wardle Katika mahojiano yake na mtandao wa The Sun, Wardle mwenyewe anasema kuwa, hakuwahi kufikiria kutokea kwa siku ambayo anaweza kupata kiungo hiki muhimu kwa mwanaume na ambacho kinafanya kazi sawasawa, na endapo itakuwa ni ya mafanikio, ataanza kuishi kama mtu wa kawaida. Madaktari kutoka chuo kikuuu cha London tayari wameshakiri ugumu wa zoezi ili lakini wamesema kuna uwezekano mkubwa wa kufanikiwa.
Katika hali yake aliyokuwa nayo sasa, Wardle anadai kuwa amekwishawahi kulala na zaidi ya wanawake 100, na asilimia 20% tu ya wanawake hawa ndio alioweza kuwaambia ukweli.
Wardle kwa sasa anafanya kazi kama mlinzi, mpishi na mhudumu na katika historia yake, amekwishapata matukio mbalimbali ya kunyanyaswa kutokana na hali yake na kupoteza marafiki kadhaa wa kike, na amekwishakuwa akijihusisha na matumizi ya madawa ya kulevya kama kitu cha kumfariji.

0 comments:

Post a Comment