Blogger Widgets

Sunday, March 24, 2013

KOPLO ELIKIZA NNKO ALIYEFARIKI KWA KUGONGWA NA GARI WAKATI WA MSAFARA WA RAIS KIKWETE AZIKWA ... SHUHUDIA MAZISHI YAKE HAPA HATUA KWA HATUA


Marehemu WP2492 Koplo Elikiza Nnko (46) enzi za uhai wake.
Marehemu Elikiza alizikwa katika makaburi ya Mbweni jijini Dar es Salaam Alhamisi wiki iliyopita ambapo mazishi yake yalihudhuriwa na mamia ya wakazi wa Dar wakiongozwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Said Mwema.(Picha GPL)
Watoto wa marehemu wakiuaga mwili wa mama yao.
Wafanyakazi wenzake na marehemu wakiwa wamebeba picha na msalaba wakati mwili ukipelekwa kwenye gari.
Mwili wa marehemu ukipelekwa kwenye gari tayari kwa safari ya kuelekea makaburini.
Askari wakijiandaa kutoa heshima za kijeshi kwa mwili wa marehemu Elikiza.
Mwili wa marehemu ukiingizwa kaburini.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Said Mwema, akiweka udongo kwenye kaburi la marehemu Elikiza Nnko.
Watoto wa marehemu wakiweka udongo katika kaburi la mama yao.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Said Mwema, akiweka shada la maua kaburini.

0 comments:

Post a Comment