Blogger Widgets

Saturday, February 9, 2013

FAHAMU WASIFU WA MAREHEMU BABA ASKOFU DR. THOMAS LAIZER NA RATIBA YA MAZISHI YAKE ARUSHA.


 Hatimaye mwili wa askofu wa Kanisa la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi yaKaskazini Kati,Marehemu Askofu Dk. Thomas Laizer unatarajiwa kuzikwa Ijumaa ya wiki ijayo Februari 15, 2013. 

Taarifa iliyotolewa na Kamati ya Mazishi ya KKKT na Familia ya Marehemu, iimeeleza kuwa Marehemu atazikwa katika eneo la Kanisa Kuu mjini Kati Arusha. Aidha taarifa hiyo inasema kuwa waumini na Washirika wa Kanisa Kuu na makanisa yote ya KKKT nchini, Wananchi, ndugu jamaa na marafiki watapata fursa ya kutoa heshima zao za mwisho kwa Mwili wa marehemu kuanzia siku y Alhamisi mchana ya Februari 14, 2013.

 Taarifa hiyo iliongeza kuwa Mwili wa Askofu Laizer utalala Kanisani hapo hadi Ijumaa ya Mazishi. Marehemu Askofu Thomas Laizer aliyezaliwa Machi 10, 1945 katika Kijiji cha Kitumbeine Wilayani Longido na baade kupata elimu yake ya msingi hadi darasa la nane Longido na kumaliza mwaka 1965. 

Askofu Laizer, aliendelea na masomo yake ya juu ndani na baade kujiunga na masomo ya Theolojia katika chuo cha Makumira na baade kuongeza masomo nchini Marekani. Marehemu wakati wa uhai wake alikuwa Mwinjilisti, Mchungaji katika makinisa mbalimbali nchini na baade kuwa Mkuu wa Jimbo na Mkuu wa Sinodi na baade kuwa Rais wa sinodi kabla ya kusimikwa rasmi kuwa Askofu wa Kwanza wa Dayosisi ya Arusha ambayo kwa sasa ni Dayosisi ya Kaskazini Kati.

0 comments:

Post a Comment